Kwanini ni lazima Lowassa astaafu ?

technically

JF-Expert Member
Jul 3, 2016
11,975
48,843
Hoja kumi kwanini Lowassa anatakiwa kupumzika kama si kuachana na siasa.

1: Lowassa amezeeka umri wake ni miaka 68 kwa sasa kwa waafrika afya yetu haiwezi kuendana na changamoto za kupigania maslai ya upinzani.

2: Kashifa yake ya ufisadi wa Richmond hata kama hajapelekwa mahakamani hiyo haimfanyi asiwe fisadi.

3: Utajiri wake wenye utata ambao ameupata toka enzi za baba wa taifa mwalimu nyerere.

4: Uwezo wake wa kutengeneza mtandao kama alivyofanya ccm anaweza Fanya pia chadema.

5: Kuwepo kwa vijana waaminifu na waadirifu ndani ya chadema kama Tundu Lissu na John Mnyika wanaweza kupeperusha bendera ya chadema .

6: Kuchangia kuwapoteza baadhi ya vijana uchaguzi uliopita hasa wapigania ufisadi kama Kafulila na Wenje kwani wafuasi wangeweza kutumia nguvu ya umma kulazimisha ushindi uliopatikana lakini Lowassa alichangia kwa namna moja baada ya kuwaambia watu watulie.

7: Kushindwa kupigania maslai ya Zanzibar kwa Seif hata baada ya kushinda imekuwa kama utapeli kwani nguvu ya umma ingeusika sasa hivi tungelikuwa tutaongea mambo mengine

8: Kusalitiwa kwake na watu aliowaacha ccm sasa kama kuna watu waliachwa ili walinde ushindi wake huko huko ilikuwaje wakamsaliti na kushindwa kuwa na interijensia ya kutosha mpaka Kituo cha ukawa cha kukusanya matokeo kikavamiwa na police.

9: Marafiki wa Lowassa wamepungua na kupotea kabisa baada ya kushindwa uchaguzi.

10:Uwezo wa Lowassa kujieleza ni Mdogo mno na ndio ulichangia asichaguliwe mwaka 2015 hivyo ningeomba astaafu siasa aache kuwaza uchaguzi 2020 ambapo atakuwa na miaka 73 uwezo wake wa kujieleza utakuwa umepungua maradufu

Kiufupi pumzi imekata kabisa lazima tuwe wakweli.
 
Jihadhari na kauli zako. Waulize nani hii na noniino. Wako wapi? Shauri yako
 
Back
Top Bottom