# UKAWA na chadema mmekosa demokrasia ya kweli ndani ya chama, kama mlishindwa kuteua mgombea uraisi kwa kufuata misingi ya kidemokrasia ndani ya UKAWA, mnathubutu vipi kuja kwangu kuniomba kura? Kwa sababu hii siwezi kuwapa kura yangu. Kama alliance imekosa demokrasia, sidhani kuwa mnaweza kuongoza nchi kidemokrasia.
# Kile mlichokuwa mnaimba kila siku majukwaani, mkiongozwa na Dr. Slaa, Lissu, Mnyika na wengine kuhusu ufisadi ambao limekuwa kero kwa wananchi walio wengi, huku mkiaminisha umma kuwa baadhi ya viongozi ndani ya CCM ni mafisafi papaa, leo hamuwezi tena kuwasema, bali mmeungana nao. Hilo ni dhahiri kuwa mpo kimaslahi na sio kulipigania taifa. Ndio wale wale tu hakuna tofauti. Sioni sababu ya kuwapa kura yangu.
# UKAWA haina sera, zaidi ya kuongea kuitoa CCM madarakani, sioni sera wala mkijinadi kwa sera. We need to know what you'll do to the people of this nation, tuna kero nyingi...hatutaki hadidhi za kuuchukia umasikini huku hamna strategies za kuuondoa umasikini.
# Nina wasiwasi na afya ya mgombea wa UKAWA, Mimi sio Mungu lakini ni dhahiri kuwa kiafya Lowassa hayuko sawa, haruwezi kuweka mtu ambaye afya yake ni tatizo, nchi inagitani kiongozi mwenye afya imara ili atumie nguvu, busara, uwezo na ajili zake zote kutuongoza. Kwa sababu hiyo pia, siwezi kumpa kura yangu.