Sun is Sun
JF-Expert Member
- Mar 13, 2024
- 1,152
- 1,696
Nina hoja ya msingi kuhusu jinsi baadhi ya mitandao ya mikopo ya simu inavyokiuka makubaliano ya ulipaji. Kwa mfano ukikopa tarehe 15 mwezi huu, makubaliano yanaonyesha kwamba malipo yanapaswa kufanyika tarehe 21. Hata hivyo kabla ya tarehe hiyo kufika, tayari wateja wanaanza kupigiwa simu, kutumiwa ujumbe wa vitisho, na kukumbushwa kwa njia ya matusi na kejeli.
Swali langu ni,. Kama tumekubaliana tarehe ya mwisho ya kulipa ni tarehe 21, kwa nini wanachukua hatua kabla ya muda huo kufika? Hii ni kinyume na makubaliano ya kimkataba.
Ni kweli Watanzania wengi tunakumbwa na changamoto za kifedha na tunategemea mikopo hii kwa matumizi ya dharura lakini haimaanishi kwamba watoaji wa mikopo watunyanyase au kuvunja sheria na makubaliano waliyojiwekea wenyewe.
Naomba Serikali kupitia mamlaka husika kama TCRA, BOT au mamlaka ya kulinda watumiaji wa huduma za kifedha ifuatilie mwenendo huu wa kampuni zinazotoa mikopo kwa njia ya simu hasa zile zinazoenda kinyume na makubaliano ya ulipaji.
Ninaomba wanajamii wenye uzoefu kama huu wachangie labda maoni yetu yatafika huko juu.
Kiranga[/USER], DR Mambo Jambo,
Swali langu ni,. Kama tumekubaliana tarehe ya mwisho ya kulipa ni tarehe 21, kwa nini wanachukua hatua kabla ya muda huo kufika? Hii ni kinyume na makubaliano ya kimkataba.
Ni kweli Watanzania wengi tunakumbwa na changamoto za kifedha na tunategemea mikopo hii kwa matumizi ya dharura lakini haimaanishi kwamba watoaji wa mikopo watunyanyase au kuvunja sheria na makubaliano waliyojiwekea wenyewe.
Naomba Serikali kupitia mamlaka husika kama TCRA, BOT au mamlaka ya kulinda watumiaji wa huduma za kifedha ifuatilie mwenendo huu wa kampuni zinazotoa mikopo kwa njia ya simu hasa zile zinazoenda kinyume na makubaliano ya ulipaji.
Ninaomba wanajamii wenye uzoefu kama huu wachangie labda maoni yetu yatafika huko juu.
Kiranga[/USER], DR Mambo Jambo,