Elections 2010 Kwanini mbio za kuwania Urais 2015 zilianza 2010??

KakaKiiza

JF-Expert Member
Feb 16, 2010
11,578
8,600
Kinachoonekana kwa sasa CCM nivikumbo kama mtu anavyokuwa anapita kwenye msongamano wawatu wengi akiwa ameitwa mbele jinsi anavyokuwa anapangua watu ili akaitike wito!!Mzee mengi Kauli yake ya jana ina usiri mkubwa sana!Makundi ya kuwania kiti cha urais 2015 yalianza kipindi cha uchaguzi 2010!Haya tunayoyaona ya UVCCM ninyuma yapazia Aiwezekani Katibu Mkuu Wa CCM asiseme kitu!Nakataa au hata Mwenyekitikuita kikao cha dharula!!Kuna Jambo zito UVCCM haiwezi kuwa na uthubutu wakumsema Waziri Mkuu Mstaafu,Halafu Katibu Mkuu Wa CCM akakaa Kimya,Mkamo mwenyekiti Naye akakaa kimya kama simwenyekiti kutoa kalipio kali kwa UVCCM!!Leo UVCCM wamekuwa na meno yakung'ata aliyewafuga!!Je UVCCM wanapewa nanani kiburi??Wanafanya kwa maslahi ya nani ili awe rais 2015??
 
Hata CCM wenyewe hawajui ni nani hasa anayesababisha vurugu zote hizo maana wanaotaka urais katika chama hicho ni wengi mno. Imagine EL bado hajakata tamaa na yuko busy kujisafisha arejee ulingoni na inasemekana ana nguvu kweli. RA huenda naye safari hii akaamua kuingia madarakani manually baada ya kuona "remote controlled rule" yake imesababisha mambo yake mengi kuwa hadharani. Usimsahau mzee 6 maana naye uropokaji wake una jambo. Membe yeye alidanganywa na nafasi ya Mambo ya Nje akidhani ndiyo tiketi ya urais utakumbuka alivyokuwa anajipendekeza kwenye jumuiya za kidini ktk maswala ya OIC na Mahakama ya Kadhi. Hayo yalikuwa maandalizi.
Kuna wazee wanaoona walidhulumiwa na wanamtandao enzi hizo nao wanataka nafasi zao kama Mh. Fredrick. Pia kuna watu kama Magufuli, Mwakyembe nk. ambao kimsingi wananchi wengi wanawaona kama majembe halisi.
Mimi ninachohisi wengi hawaaminiani na hawajui nini kinakusudiwa na Mwenyekiti wao. Angalia kauli za watu kama Mzee Makamba yaani unaona kabisa ni Katibu lakini hajui anachokitaka wala afanye nini ili kumfurahisha mwajiri wake.
 
Nadhani sababu kubwa ya kujadili kwa kasi urais wa 2015 ni udhaifu wa rais aliyeko madaraka. Watu wamepoteza matumaini na uwezo wake wa uongozi and therefore wanajaribu kuweka nguvu kwa yule ajaye with hope that atakuwa na uwezo wa kukabiliana na changamoto zinazowasumbua wananchi, manake huyu wa sasa hajui kwa nini watu ni maskini na kwa hiyo hana uwezo wa kukabiliana na mfumuko wa bei, hana uwezo wa kupunguza umaskini nk
 
Tunakaribia kuwa kama Kenya.Maanake walipomaliza tu uchaguzi walianza kampeni,ili kuthibitisha ile kauli kwamba mwanzo wa uchaguzi mmoja ni mwisho wa uchaguzi mwingine

Hili jambo huwa lina-paralyse shughuli za maendeleo.Watu wanafanya kazi kwa kuangalia on how are they going to score political credits only
 
Hata CCM wenyewe hawajui ni nani hasa anayesababisha vurugu zote hizo maana wanaotaka urais katika chama hicho ni wengi mno. Imagine EL bado hajakata tamaa na yuko busy kujisafisha arejee ulingoni na inasemekana ana nguvu kweli. RA huenda naye safari hii akaamua kuingia madarakani manually baada ya kuona "remote controlled rule" yake imesababisha mambo yake mengi kuwa hadharani. Usimsahau mzee 6 maana naye uropokaji wake una jambo. Membe yeye alidanganywa na nafasi ya Mambo ya Nje akidhani ndiyo tiketi ya urais utakumbuka alivyokuwa anajipendekeza kwenye jumuiya za kidini ktk maswala ya OIC na Mahakama ya Kadhi. Hayo yalikuwa maandalizi.
Kuna wazee wanaoona walidhulumiwa na wanamtandao enzi hizo nao wanataka nafasi zao kama Mh. Fredrick. Pia kuna watu kama Magufuli, Mwakyembe nk. ambao kimsingi wananchi wengi wanawaona kama majembe halisi.
Mimi ninachohisi wengi hawaaminiani na hawajui nini kinakusudiwa na Mwenyekiti wao. Angalia kauli za watu kama Mzee Makamba yaani unaona kabisa ni Katibu lakini hajui anachokitaka wala afanye nini ili kumfurahisha mwajiri wake.
Nikweli ila sasa huu mtandao wa Ridhiwan je unwezekana unahusika na hizi vurugu za UVCCM??Ndiyo maana makamba hawezi kuthubutu kusema chochote kwakujua mkulu anamkono wake??Kwani kama katibu hajasema basi Kwa nini Mwenyekiti asemikitu chochote auhajui kinachoendelea UVCCM??hebu tuliangalie kwa mapana!!
 
Back
Top Bottom