Kwanini Lowassa anaiponda CHADEMA?

Masaburi masaburi masaburi harufu chaaffuuuuuuuu!!!
 
Nguvu ya UMA ielekee kwa huyu jambazi mkuu arudishe pesa zetu katika mfumo wa ukusanyaji kodi badala ya kuzihonga kutafuta kura 2015.
 
Huyu si alipongeza yale maandamano ya egypt huyu tena akatoa na wito viongozi waache kujilimbikizia mali?kweli nimeamini watu waongo wanaongoza kwa kusahau haraka,si ajabu alishasahau kama aliwahi kusema hivyo huko nyuma.
 

Well said mkuu;tupime hoja ya mtu sio kuanza kuleta mizani za kina Ndugai
 

Hahahahahaaaaaaaa...naona limekupata mwenyewe hapo kwenye red
 
Mtu aliumwa na nyoka akiona jani tu hushituka vivyo hivyo kwa fisadi akiona mandamo ya wazalendo tumbo joto. Na bado ngoja uchaguzi ufike awamu hii hakuna wizi wa kura kila mtu atapata zake za halali kura zitalindwa mpaka pumzi ya mwisho na atakayecheza na kura ajiandae kumtokea yale ya Kenya ys kins Kenyatta na wenzake
 
Toa haki za watu uone kama utamuona mtu barabarani!
 
Kwasababu kwenye ile LIST OF SHAME ya CDM yeye (Lowasa) yumo. Hivyo anafanya "pre-emptive strike"
kama atabahatika kupeperusha bendera ya CCM 2015.
 
acheni ushabiki wa vyama,hivi kweli wengine kazi yao iwe ni kujenga nchi na wengine kazi yao kutumia walivyozalisha wenzao bila kutoka jasho, kumbukeni sasa hivi kila mtu amechoshwa na ugumu wa maisha.Lakini msile mkajisahau maana mwisho wake mbaya
 


lazima tufike mahala tujiulize maswali mengi juu ya huyu mtu, kwa nini kipindi hiki anakuja kasi kupitia makanisa kwenda ikulu? Anatafuta nini mtu mwenye mali yote yenye maelezo yasiyojitosheleza? Leo tumesahau baada ya kusota kutokana na makosa yake kibao na washirika wake? Migogoro ya ardhi imeisha aliyosababisha, leo mmesahau? Mmesahau mmesahau leo ufisadi alioufanya? Hamjiulizi kwa nini na kwa nini ikulu anapalilia?tuwe na akili jamani huyu ni nyoka tona swira!hafai hafai hafai kuwa kiongozi wa hii nchi!msithubtu hata siku moja nawaambia watanzanai!
 
Maendeleo hayaletwi na mtu mmoja mmoja kuchangia mabati na vyumba vya madarasa,hakuna nchi duniani iliyowahi kuendelea kwa harambee,huyo tajiri anayejitolea kila harambee yupo ,yeye utajiri wake alichangiwa na nani?ni vizuri kujitolea lakini asione kuwa anasaidia sana jamii ki hivyo.
 

Asante kwa hoja.Tatizo ni hao walalahoi wengi wao bado hawajaamka toka usingizi.Ebu jaribu kuangalia kwenye mjumuiko wa harambee hiyo wenye nazo ni wangapi na bado wengi wa walalahoi waliohudhururia nao wanapiga vigelegele.
Hata hivyo tatizo kubwa lililopo nayo nikuwa viongozi wa nyumba hizi za Ibada nao wamegeuka na kufanya shughuli tofauti na masuala ya imani na kukemea maofu.Ebu fikiria unamwalika mtu kama Lowasa kwenye nyumba ya Ibada pamoja na tuhuma zote zinazomzunguka na ambavyo yeye mwenye hajaoata kujitokeza na kujitetea hata kama si mahakamani.
 
Kwa hiyo kwa akili yako unataka kutuambia kuwa viwanda vyetu vimekufa kutokana na maandamano?

Viwanda vyetu vimekufa kutokana na Uongozi na usimamizi mbovu. CCM daim ni "CHUKUA CHAKO MAPEMA' na kwa kudhihirisha hili turudi nyuma kidogo tutafakari kuhusu MRADI WA MABASI YA WANAFUNZI" hapa DSM kwenye miaka ya 90's

Mradi uliopewa jukumu la kusimamiwa na UVCCM, hatimaye haukudumu ule mradi kwani "MTOTO WA NYOKA NI NYOKA'

Wale vijana walikumbuka kuwa Wazee wao "WANA CHUKUA CHAKO MAPEMA" nao vijana wakachukua. Mwishowe hata mabati ya yale mabasi hakuna sijui nani alichukua hadi mabati kufanya SCREPER.

Hivyo endapo uongozi wa Serikali utabadilika na kuwekwa watu wenye msimamo na uchungu wa nji kweli kwa nini tuwe na maandamano???????

Endapo kama Madaktari watapewa haki zao kwanini wagome kufanya kazi na kuuwa wagonjwa wetu tulio maskini, kwani viongozi hawatibiwi katika Hospitali zetu na hata hii migomo wanaisikia katika vyombo vya habari. Mtoto akiumwa anapanda ndege kutibiwa nje ya nji.

Endapo wafanya kazi wote watapewa haki zao kwa nini wagome, walimu hakuna kugoma watoto wetu watasoma bila hofu. Lakini walimu wanaogoma na wa shule zetu za walalahoi, watoto wa wakubwa hawasomi shule hizo. Hivyo hawaathiriki na migomo ya Waalimu.

MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…