Kwanini huwa hivi

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,783
Reaction score
830,933
Mnapokuwa kwenye furaha ya mapenzi huitana majina yote mazuri na yenye kuvutia lakini mkikosana kidogo tuu yale majina huyeyuka na kuanza kuitana wewe nanihii au we we fulani kwanini?
Itaneni yaleyale hata kama mmeudhiana kwakuwa hasira ikiisha mtaendelea na mapenzi yenu kama kawa
 
Domo alisema:

'kweli wapendanao ndo maadui zikitimia'

kuna watu hawawezi kufake.
 
Tatizo ni jinsi ya kuachana, wengi tunaachana kimabavu mabavu tu ndio maana tunaishia kuitana kauli chafu chafu tena na kuibuliana madhaifu ambayo tuliyafumbia macho kipindi kile cha mahusiano yetu...

Wengi wa wapenzi ambao wako kwenye mahusiano huwa ni vigumu sana kuambiana madhaifu nyeti wanapokuwa kwenye relation, tabu huja pale wanapokuwa wameachana hasa kwa mmoja kumtenda mwenzie vibaya, hapo ndipo mambo yanaibuka tena ya soni kabisa!

I suggest, kama binti huna mpango nae, haina haja ya kuishi nae miaka mingi sana, huko ni kupotezeana muda tu!
 

Asante kutufundisha unafiki.
 
Ni kawaida kwa binadamu kutoa maneno yasiyofaa akikasirika, na baada ya muda hasira zikiisha hurudi katika hali yake.
 
Ni kawaida kwa binadamu kutoa maneno yasiyofaa akikasirika, na baada ya muda hasira zikiisha hurudi katika hali yake.

Na katika vitu ninavyo-avoid na kugombana na mtu kwa kurushiana maneno. Unaweza ukamwambia mtu hata kitu ambacho hukutegemea kama utakisema. Na mara nyingi kile kitu mtu anachokuambia akiwa amekasirika, huwa kipo akilini mwa huyo mtu. Yani huwa anakiwaza, sema tu alikuwa hajakwambia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…