Kwanini hatukufundishwa haya?


Mambo mengi ya kudhalilisha taifa huwa hayafundishwi popote pale, iwe marekani, Ulaya au wapi. chukua mfano wa vita ya ndani ya marekani, inafundishwaga? Tazama Biafra Nigeria, inafundishwa? hapa Kenya tu kina Ochuka (marehemu) walipofanya jaribio kumpindua Moi yanasemwa? jifunze hayo!! Mambo kama hayo ni wewe kutafuta mwenyewe, si kuwekwa katika silabasi. Mbona vitabu vinavyoelezea vipo? Kumbuka kesi ya uhaini ilikuwa ikichapishwa gazetini miaka ya 80s. Pia vitabu kama KwaHeri Ukoloni, Kwa Heri Uhuru cha Harith Ghassany vinaelezea kasoro za watawala wetu n.k.
Shida ni kuwa hatutafuti habari, zipo hotuba kibao za Nyerere kuhusu hayo. Hata mitandaoni taarifa mbona zipo?
Ebu soma ndugu yangu, tafuta habari, rejea hotuba za Mwl.
Kumbuka mwaka 1964 sababu ilikuwa wanajeshi kudai Uafrika uwekwe haraka jeshini sio kuendelea na maofisa wazungu.
Mwaka 1983 hali mbaya ya uchumi, na kwa mujibu wa NY Times baadhi ya Wahaya waliungana na wengine kula njama ya kuangusha serikali. Pia wakati huo kulikuwa na mapinduzi ktk nchi nyingi tu za Afrika.
 
wakuu wa mada hii binafsi ningependa kujua kuhusu hili jaribio la la mapinduzi la 1982.

Jaribio liliratibiwa na liliratibiwa kwa mujibu wa walioshtakiwa baadae kina Lugakingira, Ngaiza, Hatty MacGhee, na walishirikishwa maofisa fulanifulani jeshini na majina yanafahamika mkuu, Sababu ilikuwa nchi kuwa katika hali ngumu kiuchumi, pia kumbuka nyakati hizo Afrika kupinduana ilikuwa kama fasheni.
 
Kiujumla Historia ya Tanganyika imepuuzwa na watawwala. Iko wapi historia ya akina Abdallah Kassim Hanga, Iko wapi historia ya akina Tuntemeke Sanga, akina Tumbo, akina Oscar Kambona??
wana historia gani hawa? tofauti na wewe na mimi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…