Kwanini Elon musk?

Joined
Mar 23, 2025
Posts
16
Reaction score
8
Matajiri Dunia imewashuhudia wengi lakini Mimi nikiacha habari ya Tajiri na mfalme sulemani.

Niseme habari ya Tajiri mwingine wa aina yake kwa mtazamo wangu.Yaani Elon Musk.

Mtazamo wangu unazingitia mambo yafuatayo:

Moja namna anajiweka karibu na jamii. Jinsi ambavyo anautafsiri utajiri(kama utumishi kwa wanadamu na sio ubwana)-hapa Kuna hoja ya uwepo wake katika serikali inayopingwa na kuchukiwa na watu wa mlengo wa kushoto yaani maglobalist-yaani serikali ya Donald Trump.

Si hapo TU kukubali kwake kuongoza kitengo hiki kipya cha (D.O.G.E).

Natazama kwa Sasa ni kama anakwenda anticlockwise na maglobalist. Kitendo Cha Cha kuruhusu matumizi ya akili badala Yale waliokaririshwa vyuoni. Hapa anahusika na wanafanyakazi wake.
Naomba Leo niseme haya!
 
Mkuu, malengo ya syndicate ya Elon na wahuni wenzake ni meusi kuliko unavyodhani.

Kamwe katu usiipime nia ya mtu kwa kigezo tu cha kujificha kwenye huduma za jamii.

Ni kweli utawala wa Trump unafanya vizuri kwa sasa, licha ya kelele nyingi za wapinzani na waliokamatika plus vitisho na hasara za Tesla anazopata Elon.

Nadhani kumwelewa Elon vizuri ni lazima mtu aelewe movie kama The Blacklist - Raymond Reddington anaiteka serikali ili kusaidia kupambana na maadui wake na kuendelea kutanua kwa uhuru ufalme wake wa kihalifu.

Huyo ndiye Elon Musk.

Kuna mabwanyenye wachache wanaitaka Marekani yote na dunia nzima iwe mikononi mwao, bila kubugudhudhiwa na yeyote.

Maamuzi watakayofanya wao ndiyo maamuzi ya wote - wanafanya maamuzi kwa niaba ya umma.

Hili ndilo lengo lao kubwa namba moja - utii usio na swali katika jambo lolote waamualo!

Unadhani kwa nini kuna harakati za kuhamia Sayari ya Mars?

Kama tuna uwezo wa kuifanya sayari nyingine kudumisha uhai, kwa nini tusiifanye dunia (inayosemekana kuelekea kufa) iweze kuendelea ku-support uhai?

Hivi si kwamba kuna mpango wa siri wa ^kuisafisha^ dunia???

Elon Musk ni nani na anafanya kazi chini ya mwavuli na kanuni na malengo gani hasa?

Haya ndiyo maswali ya msingi kwetu kujiuliza kwa kina.
 
Hapa 🙏.Tunapanua mada na kuipa jina The New world Order!
 
Kule kufananisha Suleiman na hii kondom ni taarifa tosha kwamba vibaraka wa kiakili tunao wengi sana.
 
Pale akili kiazi inapolazimisha kuzungumza mambo makubwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…