Kwanini DSE inaenda kwa kusuasua? Je, kuna uhusiano kati ya umadhubuti wa Serikali katika kusimamia Ardhi na Maendeleo na Ushamiri wa DSE?

Kamukhm

JF-Expert Member
Aug 30, 2015
2,799
4,200
Soko la hisa la DSM (DSE) linaendelea kukua kwa kujikongoja ukilinganisha na Masoko ya Nairobi(NSE), Johannesburg(JSE) na Kigali (RSE); wakati uwekezaji nchini ukiendelea kukua steadily. Shida ni Nini?

Kwa wale wataalamu wa maswala ya Masoko ya Dhamana, Je, hakuna uhusiano wowote kati ya ongezeko la uwekezaji na ukuaji wa masoko ya mitaji na dhamana!?

Mawazo binafsi.

Taratibu Dhaifu za kimamlaka katika kusimamia miliki, za Ardhi na vibali vya uendelezaji miji zinachangia kwa sehemu kubwa kuondoa mazingira rafiki kwa wawekezaji wazawa na wageni, kwa ujumla.

Mfano; katika eneo la Ardhi, swala la Serikali kufuta miliki, kila inapojisikia hasa kwenye maeneo yenye uvamizi, inaathiri "Imani" Kati ya wawekezaji na Mifumo ya Usimamizi wa Serikali; ambayo nadhani inayo athari ya moja kwa moja na hali ya uwekezaji nchini.

Kuna scenario nyingi ambazo ukizifikiria unakosa majibu;

Mtanzania anadunduliza pesa anajinyima.. ananunua ekari 500 kwa ajili ya Kilimo. Serikali inammilikisha baada ya kukamilisha taratibu zote. Anaanzisha Kampuni anaingia ubia na kampuni nyingine kukuza mtaji wanaanza uzalishaji na kusogeza miundombinu muhimu Kama maji, umeme na Barabara.

Hapo eneo hilo ambalo awalo lilikuwa shamba pori; linaanza kupata thamani, mara (Kupe) wanaanza kuvamia. Miaka mitano tayari wamejaa.

Mwenye mali anafika awaondoe kupanua operation, Wananchi Hawa(kupe) wanakimbilia kwa viongozi wa kisiasa, ghafla muwekezaji analazimishwa kugawa sehemu ya Ardhi yake, (aliyonunua kihalali na kuaminishwa na serikali kuwa anaweza kuitumia kwa miaka 66/99) kwa wananchi bure(kisa tu ni wapiga kura).

Hii inahuzunisha na Inaathiri uzalishaji na mipango ya baadae ya makampuni na uwekezaji kwa ujumla.

Nadhani hii kutokuwa na hakika ya kesho kwa uwekezaji hasa kwenye eneo la Ardhi na kutokuwa na mifumo inayoweza kutabirika kunayo athari ya moja kwa moja na ukuaji wa soko la dhamana na mitaji nchini.

Kwa Kenya katika hili wametuacha sana, Kama ilivyo kwa South Afrika na Rwanda nao wameamka na tunaona toka wametoka kwenye vita wanapiga kasi nzuri na ni kwa kusimimamia mifumo sio kudekezana.

Mwisho: Naomba kusikia kutoka kwa wajuvi, manguli wa mada hii. Lakini kwa wale watetezi wa kupe nitoe Rai..ukivamia shamba la mtu au kiwanja huo ni wizi. Flat out. Ukitetea ujue unatetea wizi.

Ahsanteni.
 
Mkuu nadhani ungetenganisha isue za soko la hisa na matatzo ya ardhi...kwakuaniza heb nitajie kampuni moja wapo iliyokua listed kwenye soko la hisa yenye matatzo ya ardhi yake kuvamiwa?
 
Soko la hisa la DSM (DSE) linaendelea kukua kwa kujikongoja
Hii takwima kama haukupewa na National Bureau of Statistics - NBS - basi hizi ni PROPAGANDA chafu. Unafanya uzandiki (subversion) dhidi ya taifa lako. Sasa sijui ni nani anakutumia.
 
Hii takwima kama haukupewa na National Bureau of Statistics - NBS - basi hizi ni PROPAGANDA chafu. Unafanya uzandiki (subversion) dhidi ya taifa lako. Sasa sijui ni nani anakutumia.
1) Kwanini umefanya assumption kuwa ninatumika!?

2) Je ni kweli tunafanya vizuri Sana kuliko Masoko niliyoyataja!?

Kwa dhana ya kutumika nikuondoe shaka, Sio kila anayehoji anatumika; sote tunataka kujenga. Na sio kujenga kwingine; hapana, ila ni kujenga hili hili taifa Kuu na Teule la Tanzania.

Since you seem to have more knowledge on the matter. Enlighten me on the second question. Please.
 
Mkuu nadhani ungetenganisha isue za soko la hisa na matatzo ya ardhi...kwakuaniza heb nitajie kampuni moja wapo iliyokua listed kwenye soko la hisa yenye matatzo ya ardhi yake kuvamiwa?
Mh. Gobole ukisoma Sura ya kwanza kabisa ya Sera Ya Taifa ya Maendeleo ya Makazi inafafanua makazi ni Nini. Kwa lugha rahisi kabisa Makazi ni sehemu ambapo Shughuli za kibinadamu hufanyika kwa mpango na utaratibu maalumu.

Hii inamaanisha makazi sio pale unapolala tu, ni unakopita, unakolima, unakouza, unakopumzika na kuzalisha kwa njia nyinginze zote.

Kuzungumza juu ya DSE na Makazi ambayo hujengwa juu ya Ardhi Ni swala Muhimu. Na linahitaji uangalizi mzuri.
 
Shida ni yule Mkurugenzi mtendaji wa pale Soko la hisa (DSE) , kama yeye mwenyewe anashindwa kujiongeza na kuisaidia DSE kukua basi hafai kuwepo pale maana inaonekana dhahiri kua uwezo wake ndo umeishia pale.
Mkuu kwa hiyo unahisi Ni utendaji wa ndani ya DSE ndio Changamoto Kubwa!?
 
Mkuu naona unachanganya mambo...km unataka tuzungumzie issue ya ardhi na makazi lets talk abt it kwenye uzi tofauti na km unataka tuzungumzie kuhusu soko la hisa then tuyazungumzie ktk uzi wake unajitegemea...haya mambo yana uhusiano mdogo sana.
Mfano issue ya mimi kutaka kununua au kuuza hisa za crdb au vodacom zinahusiana nn na migogoro ya ardhi kati kule mkuranga?what's the connection btn those 3 entities?
 
Umesema Rwanda wametuzidi kwenye uwekezaji wa ardhi Sasa kwanini usijaribu kuchukua ardhi miaka 66 huko Kigali uwekeze
Henry Sijui kama tunaelewana .. Ni Kama you are just attacking.. why!?

Kwann nihamie Rwanda na kwetu kupo!? Kuhoji kwenu ni kosa!?
 
Mkuu naona unachanganya mambo...km unataka tuzungumzie issue ya ardhi na makazi lets talk abt kwenye uzi tofauti na km unataka tuzungumzie kuhusu soko la hisa then tuyazungumzie ktk uzi wake unajitegemea...haya mambo yana uhusiano mdogo sana.
Mfano issue ya mimi kutaka kununua au kuuza hisa za crdbt au vodacom zinahusiana nn na migogoro ya ardhi kati kule mkuranga?what's the connection btn those 3 entities?
Tatizo umeangalia trading peke yake. Je umeangazia na Listing!? Uwezo wa makampuni yetu wazawa kuorodheshwa kwenye soko la hisa!?

Lile Ni soko la mitaji na Dhamana. Ukiuziwa share za Vodacom unanunua kwa sababu ya uimara wake.. unaweza kusemaje kwa biashara zinazotegemea Ardhi nchini Kama mashamba makubwa ya ngano nk ambayo yako prone na uvamizi, despite being titled!?

Lakini hata utoaji wa vibali vya Huduma mbalimbali hauzingatii uhitaji wa soko nchini(vinatolewa tu yaani ukiomba tu unapewa). Kwa kifupi mfumo wetu wa kujiendesha hauko organised matokeo yake huwezi kupredict kesho ya biashara yoyote maana Masoko hayalindwi. Hence no security.

Sasa mitaji hii tunayotaka kuikuza kwa fedha za Umma wa Watanzania zitakuwa zinatumika kupanua uwekezaji ma Kampuni ya kigeni tu!? Kwann tusijiboreshe ili fedha za Umma wa kitanzania zitumike kuinua biashara za ndani pia!?
 
Tatizo umeangalia trading peke yake. Je umeangazia na Listing!? Uwezo wa makampuni yetu wazawa kuorodheshwa kwenye soko la hisa!?

Lile Ni soko la mitaji na Dhamana. Ukiuziwa share za Vodacom unanunua kwa sababu ya uimara wake.. unaweza kusemaje kwa biashara zinazotegemea Ardhi nchini Kama mashamba makubwa ya ngano nk ambayo yako prone na uvamizi, despite being titled!?

Lakini hata utoaji wa vibali vya Huduma mbalimbali hauzingatii uhitaji wa soko nchini(vinatolewa tu yaani ukiomba tu unapewa). Kwa kifupi mfumo wetu wa kujiendesha hauko organised matokeo yake huwezi kupredic kesho ya biashara yoyote maana Masoko hayalindwi. Hence no security.

Sasa mitaji hii tunayotaka kuikuza kwa fedha za Umma wa Watanzania zitakuwa zinatumika kupanua uwekezaji ma Kampuni ya kigeni tu!? Kwann tusijiboreshe ili fedha za Umma wa kitanzania zitumike kuinua biashara za ndani pia!?
Unaweza kunipa mfano mmoja wa kampuni iliyokua listed ktk soko la Rwanda au Kenya inayotegemea ardhi?

Anyway issue ya kuuza na kununua shares kwa watanzania ni swala mtambuka na sidhani km linahusiana sana na ardhi km unavyotaka kutuaminisha.

1. Elimu, watu wengi hawana Elimu ya hii kitu,wanaiskia na kuipuuzia...

2.Return ni ndogo hivyo kuwakatisha watu tamaa

3.Ubinafsi na hii inaanzia ktk kufungua kampuni unakuta mtu au Share holders wawili au watatu wamejimilikisha shares zote...na hawauzi ht moja thus why siku wakifariki their companies dies with them, wapo radhi mfungue kampuni nyingine ila sio kukuuzia hisa on their existing companies

4. Watanzania wengi ni wakwepaji wa kodi na janja janja, wana hofia wakilist biashara yao DSE hesabu zao zitakua public info, and they cant afford that.

5. DSE hawajitangazi wala kutangaza fursa zilizopo..hawapigii watu simu km ilivyo Marekani na inchi nyingine za Ulaya na Asia..Kifupi wapo wapo tu

6. Issue ya watu kuvamia ardhi za wawekezaji Uchwara linatokana na watu kuchukua ardhi kubwa bila kuifanyia kazi, mostly coz wanaenda kuikopea bank then wanaitelekeza then huku nyuma watu wanavamia..Am sure km wako site all the time then its easy to spot uvamizi na kuuzuia mapema bt hili la kujimilikisha ardhi unaenda kukopea pesa bank na pesa uliyokopea huirudishi ktk ardhi uliyoikopea, unatokomea 10yrs down the line ndo unarudi site migogoro haiwezi kuisha.
 
Unaweza kunipa mfano mmoja wa kampuni iliyokua listed ktk soko la Rwanda au Kenya inayotegemea ardhi?

Anyway issue ya kuuza na kununua shares kwa watanzania ni swala mtambuka na sidhani km linahusiana sana na ardhi km unavyotaka kutuaminisha.

1. Elimu, watu wengi hawana Elimu ya hii kitu,wanaiskia na kuipuuzia...

2.Return ni ndogo hivyo kuwakatisha watu tamaa

3.Ubinafsi na hii inaanzia ktk kufungua kampuni unakuta mtu au Share holders wawili au watatu wamejimilikisha shares zote...na hawauzi ht moja thus why siku wakifariki their companies dies with them, wapo radhi mfungue kampuni nyingine ila sio kukuuzia hisa on their existing companies

4. Watanzania wengi ni wakwepaji wa kodi na janja janja, wana hofia wakilist biashara yao DSE hesabu zao zitakua public info, and they cant afford that.

5. DSE hawajitangazi wala kutangaza fursa zilizopo..hawapigii watu simu km ilivyo Marekani na inchi nyingine za Ulaya na Asia..Kifupi wapo wapo tu

6. Issue ya watu kuvamia ardhi za wawekezaji Uchwara linatokana na watu kuchukua ardhi kubwa bila kuifanyia kazi, mostly coz wanaenda kuikopea bank then wanaitelekeza then huku nyuma watu wanavamia..Am sure km wako site all the time then its easy to spot uvamizi na kuuzuia mapema bt hili la kujimilikisha ardhi unaenda kukopea pesa bank na pesa uliyokopea huirudishi ktk ardhi uliyoikopea, unatokomea 10yrs down the line ndo unarudi site migogoro haiwezi kuisha.
Bwana Gobole hakuna uchumi unaoelea. Kila kitu at some point will be tied to land. Ukiwa na mfumo mzuri wa kusimamia Ardhi na Makazi unaadvantage kubwa ya kukuza uwekezaji.

Wawekezaji uchwara nao Kama ulivyowadescribe Ni zao la taratibu Dhaifu za usimamizi wa Maendeleo ya Ardhi na Makazi. Ila hata watu kuvamia mashamba na viwanja ni udhaifu mkubwa.

Biashara za Ujenzi, manufacturing, usafirishaji, hata mawasiliano ya simu za viganjani yote yanategemea Ardhi kwa kiasi fulani na mifumo ya Usimamizi wa uendeshaji wa biashara.

Leo ukiflood soko na kampuni nyingine kumi na tano za mawasiliano nchini automatically kuna makampuni yatasuffocate..na hata Yale makubbwa unayoyaamini Kama Vodacom yataathirika ..Aina hii ya athari inaweza kuwa zao la moja kwa moja la utaratibu duni wa Usimamizi wa Miji.

Mf. Ni China na India. India wamekuwapo for decades Kama moja ya vituo vikubwa vya Masoko ya hisa...China aliyeanza as late as 1992 amekuja na kupita.. maana India pamoja na ukubwa anachangamoto Kama hizi za kutokuwa organised kwenye Usimamizi wa ardhi na muendelezo wake.
 
Unaweza kunipa mfano mmoja wa kampuni iliyokua listed ktk soko la Rwanda au Kenya inayotegemea ardhi?

Anyway issue ya kuuza na kununua shares kwa watanzania ni swala mtambuka na sidhani km linahusiana sana na ardhi km unavyotaka kutuaminisha.

1. Elimu, watu wengi hawana Elimu ya hii kitu,wanaiskia na kuipuuzia...

2.Return ni ndogo hivyo kuwakatisha watu tamaa

3.Ubinafsi na hii inaanzia ktk kufungua kampuni unakuta mtu au Share holders wawili au watatu wamejimilikisha shares zote...na hawauzi ht moja thus why siku wakifariki their companies dies with them, wapo radhi mfungue kampuni nyingine ila sio kukuuzia hisa on their existing companies

4. Watanzania wengi ni wakwepaji wa kodi na janja janja, wana hofia wakilist biashara yao DSE hesabu zao zitakua public info, and they cant afford that.

5. DSE hawajitangazi wala kutangaza fursa zilizopo..hawapigii watu simu km ilivyo Marekani na inchi nyingine za Ulaya na Asia..Kifupi wapo wapo tu

6. Issue ya watu kuvamia ardhi za wawekezaji Uchwara linatokana na watu kuchukua ardhi kubwa bila kuifanyia kazi, mostly coz wanaenda kuikopea bank then wanaitelekeza then huku nyuma watu wanavamia..Am sure km wako site all the time then its easy to spot uvamizi na kuuzuia mapema bt hili la kujimilikisha ardhi unaenda kukopea pesa bank na pesa uliyokopea huirudishi ktk ardhi uliyoikopea, unatokomea 10yrs down the line ndo unarudi site migogoro haiwezi kuisha.

Ila pia hakuna mfumo wa kukuza hizi biashara. Tunajenga uchumi wa wachuuzi ambao sio mbaya Ila kwa kipindi Cha mpito tu... Isiwe ndio foundation ya uchumi wa Taifa.

Bad enough tumeshaanza kuingiwa na hiyo katika vinasaba vyetu. Unaweza kuiona kila mahali. Umimi, uharibifu na kutokuwa na Malengo zaidi ya tumbo na mahitaji yetu ya kila siku.

Aspirations za Watanzania kukua zaidi na kufanya vitu vikubwa ni ndogo. Na Kama Taifa hatuna dira moja.. unaanza kushangilia Kamali kabla ya kuzalisha..

Kwann mifumo isiboreshwe, Usimamizi madhubuti ili Watanzania wenyemawazo na Biashara zao wadhaminike kwenye soko la mitaji ili hizi elfu tano za betting watu wanunue hisa ambazo zina assurance kwenye returns!?
 
Gobole
Ukiangalie Masoko Makubwa Duniani yakiwepo ya London, Paris na NY yamejengwa juu ya mfumo madhubuti wa uendeshaji miji katika nchi husika.

Wapishi wote wa Cheni za Migahawa mikubwa huko.ughaibuni huenda wanaweza kabisa kupika wanavyoviuza! Lakini sio kufanya biashara hiyo.. maana mmchakato wake upo very regulated; ndio maana unaweza kununua hisa hata ya biashara ya mgahawa ughaibuni..sio lazima iwe tech/oil&mining company.

Na hapa(kwenye kujiendesha) ndipo uchawi mabeberu walipouficha. Na constantly funding us to stay informal and unpredictable.

Kwenye mashamba ya wine huko ufaransa haimaanishi wanatembea na bunduki wanalinda hapana.. Ila ikitokea unavamizi; basi wakienda Serikalini kushitaki, haki yao hurejeshwa. Ndio maana hata winery zinakuwa listed kwenye Masoko ya Hisa.

Sisi hapa je tunaweza kulist mashine za kutengeneza tambi!? Au Kuuza unga wa Mahindi!? Je za Kahawa!? Pareto!? Mbao!? Avocado!? Mashamba ya Mifugo!? Kama hakuna security ya Ardhi inaleta Changamoto kubwa.

Lakini hata biashara ndogo Kama local food joints zingeweza kukua na kupanuka Kama tusingeruhusu parasitic investments.. kila investment iwe based on research sio ukiona Juma Foods anauza nanyie kumi mnataka kuanzisha mkahawa UD eneo Lile lile matokeo yake wote mnakufa maana supply inakuwa kubwa kuliko demand.

Kwa mtindo huo sio Juma wala hao kumi wengine watakuwa na nguvu ya kukuomba wewe Gobole na mimi kuweka pesa zetu maana hawana hakika na Biashara hiyo. Sasa katika hali Kama hiyo unadhani ni Sahihi kulaumu DSE pekee!?
 
Back
Top Bottom