Kwanini baadhi ya Wanaume hawapati HIV?

Kwanini baadhi ya Wanaume hawapati HIV?

Usher-smith MD

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2015
Posts
9,575
Reaction score
12,368
Ni mara chache sana inatokea katika wanandoa kuwa mmoja ana VVU na mwingine hana. Ila kama ikitokea, Mara nyingi ni kuwa mwanamke anao na Mwanamme hana. (Ila mara nyingi kama Mwanamme ana VVU mwanamke atapata).

Maambukizi ya VVU hutokea/ huongezeka kwa sababu ya michubuko kwenye via vya uzazi wakati wa tendo.

Ila Maambukizi hupungua
1. Maandalizi mazuri wakati wa tendo
2. Kinga CD4 ya yule aliyeathirika kuwa juu
3. "Viral Load" kuwa chini
NK

Ila kwasababu michubuko ndio "key fact"
Kwahiyo kama una kibamia ni sahihi kusema inapunguza "chance" ya michubuko na kupelekea kutopata kirahisi VVU ama Vipi ?!!!! Maana kama Una Mashine kama ya "Mudy" sidhani kama utaepuka michubuko ila kama Una "Le Kibamiaz u know" I naweza kuwa ndio ponea yako.

Mifano hai ya visa 3 vilivyotea Bongo:
Wa kwanza Wameishi miaka 15, wa pili Wameishi miaka 8 na wa tatu Wameishi miaka 2 na kuzaa watoto ila Wanaume wote hawana maambukizi
Link hii chini







Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inategemeana na Cell za Mwili zinanguvu kiasi gani na Pia Mshaambiwa Sex ni Dakika 8 tu yatosha.

Cell hupambana sana kuvishinda virusi
 
Viungo vya ke na me ni tofauti. uke uko very exposed kupata maambukizi kwa sababu kuta za mle ndani ni laini na rahisi kuchubuka...sasa ngoz ya uume ni ngumu labda ndani ya kale katundu ambapo ni kasehemu kadogo kama 2% ya kiungo lakini uke 99% ni soft tissue.
 
Ni kweli kwamba unaweza kupata dalili za HIV ukakaa zaidi ya mwaka na vipimo vikaonesha negative?

Sent using Jamii Forums mobile app
Dalili za ugonjwa fulani sio uthibitisho wa ugonjwa husika. Uthibitisho hupatikana kwa vipimo, tena vya uhakika na vilivyofanywa kwa ufanisi.

Dalili nyingi za magonjwa zinaendana. Kwa mfano, kuna msemo maarufu sana siku hizi kuwa sio kila homa ni malaria, unaweza ukawa na homa ukiwa na typhoid, n.k.

Muda mwingine dalili huwa zinakuwa ni matokeo ya saikolojia tu. Unakuta umejamiiana bila kondom, unaamini umeathirika. Hapo utaanza kuona hadi dalili kabisa.

Kwahiyo, inawezekana kabisa ukawa na dalili kama za UKIMWI lakini usiwe na UKIMWI.
 
Viungo vya ke na me ni tofauti. uke uko very exposed kupata maambukizi kwa sababu kuta za mle ndani ni laini na rahisi kuchubuka...sasa ngoz ya uume ni ngumu labda ndani ya kale katundu ambapo ni kasehemu kadogo kama 2% ya kiungo lakini uke 99% ni soft tissue.
Hii Sio sababu ya kisayansi!! Acha wenye taaluma yao waje
 
Ni kweli kwamba unaweza kupata dalili za HIV ukakaa zaidi ya mwaka na vipimo vikaonesha negative?

Sent using Jamii Forums mobile app
No hapana..

Kuna kitu wadudu wote wa magonjwa wanacho kinaitwa "window period" yaan toka pale upate vvu mpaka vipimo vionyeshe kwa usahihi majibu.. sasa hapa kuna vipimo vya aina 2 kwa vvu.

1. kipimo maarufu tunachotumia "bioline" na mwenzake "unigold" hizi zitagundua maambukizi baada ya wiki 6 kwa usahihi wa 95% mpaka miezi 3 kwa usahihi wa 99.9%

2. Kipimo ghali kidogo ambacho kinatumika kwa watoto wachanga kwa tanzania ila mtu yyt anaweza kukipata kinaitwa "vvu PCR" hii inagundua maambukizi mapema sana kati siku 4 - wiki 4

Lakini concept yako naweza kuigeuza ikawa kweli tukisema "unaweza kua na vvu na ukakaa mpaka miaka 10 bila kuwa na dalili"

Vvu isipogundulika na kutibiwa ina pitia stages 3 na stage ya pili kitaalamu wanaiita "Latent stage" maana yake una vvu lakini huonyeshi dalili mathalani kwenye mwili mdudu anafanya uharibifu taratibu hii latent period inaweza ikadumu kwa wastani wa miaka 10 na wengine zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dalili za ugonjwa fulani sio uthibitisho wa ugonjwa husika. Uthibitisho hupatikana kwa vipimo, tena vya uhakika na vilivyofanywa kwa ufanisi.

Dalili nyingi za magonjwa zinaendana. Kwa mfano, kuna msemo maarufu sana siku hizi kuwa sio kila homa ni malaria, unaweza ukawa na homa ukiwa na typhoid, n.k...
EeeeeEeE huuuuu Mungu mkubwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom