Kwani watanzania tunajikwaa wapi katika soka??

wakushanga

JF-Expert Member
Nov 4, 2010
552
92
Ni jambo la kusikitisha sana kuona Tanzania inaendelea kufanya vibaya katika kila nyanja ya michezo, siku si nyingi timu ya wanawake imetolewa kwenye mashindano ambayo ingewapa nafasi ya kucheza katika mashindano ya Africa. timu ilipo ondoka hapa tuliambiwa imejiandaa vizuri na itaibuka kidedea lakini kilichotokea wote tunajua. navisingizo chungu nzima vimeshaanza kutolewa.

kama hiyo haitoshi timu ya taifa ya wanaume chini ya kocha wa kibrazili maximo haikuweza kufika mbalia katika kila mbio iliyojaribu kufurukuta na kunyume chake kujikuta ikiendelea kupiga marktime, nasasa tuna kocha mpya mzungu ambaye naye kama maksimo tunamlipa mijihela chungutele!!!!. Sinashaka kwa %92 hatafanya lolote na huenda yakawa yaleyale ya mwenzetu mblazili.

mwezi mmoja uliopita nilisikia katika habari za michezo cha itv, mmoja wa washauri wa bench la ufundi na kocha wa makipa akisema Rais anadanganywa. kwa kuambiwa timu zimejiandaa vizuri na kumbe hua ni adithi za abunuasi.

sasa wana JF mnaonaje tusitishe mipango ya kuwaleta hawa makocha na hizi hela za kuwalipa hawa makocha wa kigeni tununue madawati ya shule za msingi ambazo watoto wanakaa chini tukianzia za kule Mpwapwa Dodoma, pamoja na kukarabati majengo ya shule za msingi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom