Wakati mkiendelea na zoezi la sensa nawaomba watanzania mje na mjibu swali hili ambalo nimedhani litatuongezea upeo wa kutafakari.
Uchumi umekua kama jinamizi ambalo linaondoa usingizi wa wananchi wengi wakubwa na wadogo. Wakiteswa na njaa, magonjwa, ukosefu wa huduma za jamii za msingi ikiwemo makazi duni na kazi zisizo na staha.
Elimu duni inayopelekea wahitimu kupoteza muda shuleni na gharama kubwa licha ya wakihitimu kumaliza elimu zao pasina kuwa na maarifa na ujuzi wenye manufaa unoweza kutatua changamoto za maisha. Hili pia ni zigo ambalo kama taifa hatuna jawabu.
Mmomonyoko mkubwa wa maadili unaolitafuna taifa. Sio vijana wala wazee wote hakuna wa kumfunga kengele mwenzie. Kiwango kikubwa cha utumiaji wa vilevi na madawa, ndoa kuvunjika, uzinzi na uchangudoa, utoaji mimba na mengine kama hayo yanazidi kuliteketeza taifa.
Uongozi mbovu na ufisadi bado vinazamisha meli yetu ya maendeleo na kama taifa simuoni mwenye akili wakutusaidia kushinda changamoto hizi. Hajui ni sifa zipi kiongozi anapaswa kuwa nazo, viongozi kutamani kutumikiwa na sio kutumika, rushwa Ili kuwa kiongozi na ubadhilifu wa Mali za umma ni matatizo ambayo jamii yetu bado inatapatapa pasina majawabu
Je, hatuna wenye akili katika jamii zetu wakutupa solution za changamoto hizi?
Historia inaweka kumbukumbu ya philosopher waliowahi kuishi na kwa matumizi mazuri ya akili zao walizisaidia jamii zao. Je sisi hatuna watu kama hawa wenye ufahamu na akili nzuri ya kuleta majawabu? Je jamii yetu inawatambua watu wa namna hii, je kuna mifumo ya kuwabaini na kuwawezesha kufanya kazi hii ya kufikiri na kuja na majibu ya kimikakati?
Wako wapi philosopher hawa ambao wataanzisha community schools Ili wawaendeleze follower wao. Usinishawishi kuwa hawa philosopher ni akina Mtume Mwamposa, Mtalemwa, Jo Davie, Mzee wa Upako au askofu Mwingila?
Nauliza tena je jamii zetu hazina watu wenye akili?
Karibuni.
Uchumi umekua kama jinamizi ambalo linaondoa usingizi wa wananchi wengi wakubwa na wadogo. Wakiteswa na njaa, magonjwa, ukosefu wa huduma za jamii za msingi ikiwemo makazi duni na kazi zisizo na staha.
Elimu duni inayopelekea wahitimu kupoteza muda shuleni na gharama kubwa licha ya wakihitimu kumaliza elimu zao pasina kuwa na maarifa na ujuzi wenye manufaa unoweza kutatua changamoto za maisha. Hili pia ni zigo ambalo kama taifa hatuna jawabu.
Mmomonyoko mkubwa wa maadili unaolitafuna taifa. Sio vijana wala wazee wote hakuna wa kumfunga kengele mwenzie. Kiwango kikubwa cha utumiaji wa vilevi na madawa, ndoa kuvunjika, uzinzi na uchangudoa, utoaji mimba na mengine kama hayo yanazidi kuliteketeza taifa.
Uongozi mbovu na ufisadi bado vinazamisha meli yetu ya maendeleo na kama taifa simuoni mwenye akili wakutusaidia kushinda changamoto hizi. Hajui ni sifa zipi kiongozi anapaswa kuwa nazo, viongozi kutamani kutumikiwa na sio kutumika, rushwa Ili kuwa kiongozi na ubadhilifu wa Mali za umma ni matatizo ambayo jamii yetu bado inatapatapa pasina majawabu
Je, hatuna wenye akili katika jamii zetu wakutupa solution za changamoto hizi?
Historia inaweka kumbukumbu ya philosopher waliowahi kuishi na kwa matumizi mazuri ya akili zao walizisaidia jamii zao. Je sisi hatuna watu kama hawa wenye ufahamu na akili nzuri ya kuleta majawabu? Je jamii yetu inawatambua watu wa namna hii, je kuna mifumo ya kuwabaini na kuwawezesha kufanya kazi hii ya kufikiri na kuja na majibu ya kimikakati?
Wako wapi philosopher hawa ambao wataanzisha community schools Ili wawaendeleze follower wao. Usinishawishi kuwa hawa philosopher ni akina Mtume Mwamposa, Mtalemwa, Jo Davie, Mzee wa Upako au askofu Mwingila?
Nauliza tena je jamii zetu hazina watu wenye akili?
Karibuni.