zimwilachi
Member
- Oct 22, 2016
- 40
- 23
Nini hatima ya maisha ya hawa vijana waliokuwa wakisoma kozi hizi:
· Higher Diploma in Secondary Education (3yrs)
· Ordinary Diploma in Primary Education (3yrs)
· Laboratory technician
Hizi ni kozi mpya zilizoanzishwa na serikali ya awamu ya nne ya Mh Kikwete kupitia wizara ya elimu, kozi hizi zilianzishwa kwa malengo ya kuongeza ufanisi wa walimu nchini kwetu hatimae kuzalisha walimu ambao watakua na uwezo ndani na nje nchi na kupelekea kunyanyua hali ya elimu kwa ujumla nchini mwetu. Hakika waliandaliwa wataalamu kwa ajili ya kuandaa mitaala ya hizi kozi na wataalamu hao wakalipwa pesa nyingi za kodi za wananchi.
Mama Ndalichako bila kufanya utafiti wowote juu ya kozi hizi mpya ameingia madarakani na kuzifutilia mbali kwa madai kwamba hazitambui na hii yote imechangia na maamuzi ya kukurupuka na kutafuta sifa kutoka kwa mkuu wa nchi. Mbaya Zaidi amefuta kozi hizo bila kutoa muongozo ni nini kifanyike kwa wanafunzi waliokua wanasoma kozi hizo na ikumbukwe kuwa tayari kuna wanafunzi ambao walikuwa mwaka wa pili wakiwa wamebakiza mwaka mmoja kumaliza kozi.
Vijana wapo mtaani hawajui nini hatima ya maisha yao Waziri akipigiwa simu hapokei ama akipokea anatupia mpira kwa katibu mkuu ambaye naye akipigiwa hana majibu ya kueleweka Zaidi ya kuambiwa kuna mchakato unaendelea, ni mchakato gani huo unaoendea karibu mwezi wa tatu sasa tangu mtangaze kufuta kozi hizi. Vijana wapo nyumbani hata hawajui hatma ya maisha yao na kufikia hatua kushidwa hata kuwaeleza wazazi nini kinachoendelea.
Mama Ndalichako (Waziri mwenye dhamana) tunaomba kujua hatma ya maisha ya hawa vijana. Kama mambo magumu achia ngazi tuu Mama!
Serikali ya viwanda
Mawazo huru.
· Higher Diploma in Secondary Education (3yrs)
· Ordinary Diploma in Primary Education (3yrs)
· Laboratory technician
Hizi ni kozi mpya zilizoanzishwa na serikali ya awamu ya nne ya Mh Kikwete kupitia wizara ya elimu, kozi hizi zilianzishwa kwa malengo ya kuongeza ufanisi wa walimu nchini kwetu hatimae kuzalisha walimu ambao watakua na uwezo ndani na nje nchi na kupelekea kunyanyua hali ya elimu kwa ujumla nchini mwetu. Hakika waliandaliwa wataalamu kwa ajili ya kuandaa mitaala ya hizi kozi na wataalamu hao wakalipwa pesa nyingi za kodi za wananchi.
Mama Ndalichako bila kufanya utafiti wowote juu ya kozi hizi mpya ameingia madarakani na kuzifutilia mbali kwa madai kwamba hazitambui na hii yote imechangia na maamuzi ya kukurupuka na kutafuta sifa kutoka kwa mkuu wa nchi. Mbaya Zaidi amefuta kozi hizo bila kutoa muongozo ni nini kifanyike kwa wanafunzi waliokua wanasoma kozi hizo na ikumbukwe kuwa tayari kuna wanafunzi ambao walikuwa mwaka wa pili wakiwa wamebakiza mwaka mmoja kumaliza kozi.
Vijana wapo mtaani hawajui nini hatima ya maisha yao Waziri akipigiwa simu hapokei ama akipokea anatupia mpira kwa katibu mkuu ambaye naye akipigiwa hana majibu ya kueleweka Zaidi ya kuambiwa kuna mchakato unaendelea, ni mchakato gani huo unaoendea karibu mwezi wa tatu sasa tangu mtangaze kufuta kozi hizi. Vijana wapo nyumbani hata hawajui hatma ya maisha yao na kufikia hatua kushidwa hata kuwaeleza wazazi nini kinachoendelea.
Mama Ndalichako (Waziri mwenye dhamana) tunaomba kujua hatma ya maisha ya hawa vijana. Kama mambo magumu achia ngazi tuu Mama!
Serikali ya viwanda
Mawazo huru.