Kwako labana

Kwako labana

KING ASSENGA

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2016
Posts
929
Reaction score
1,499
Nakuja kwako Mungu, shingoni yamenifika,
Naongea kwa uchungu, na machozi kadhalika
Wajua moyoni mwangu, hauwezi kufichika
Nisaidie Rabana, shingoni yamenifika,

Magonjwa yanitikisa, maumivu kadhalika
Nisamehe kwa makosa, kweli nimeadhibika
Huku usije nitosa, wanafiki wakacheka
Nisaidie Rabana, shingoni yamenifika

Elimu nadharaulika, kiuchumi kadhalika
Siniache nateseka, nani atanikumbuka
Kwako ninajisimika , Tumaini la hakika
Nisaidie Rabana, shingoni yamenifika

Malengo nikiyaweka , leo kesho yatibuka
Shida ghafla zaibuka, na magonjwa kadhalika
Kwa juhudi napigika, sio uzembe hakika
Nisaidie Rabana, shingoni yamenifika

Kuoa kwa tamanika, Eva bado namkumbuka
Kwa uchawi asifika, uchumba ukakatika
Hakubali kuachika, wanilinde Malaika
Nisaidie Rabana, shingoni yamenifika
 
Kazi nzuri kaka... ingawa upo na changamoto kidogo za kiuandishi!


Yote kwa yote kazi ni nzuri...
 
Back
Top Bottom