Kwa wenye ndoa na wanaotarajia kuingia pitieni hapa

Kingdom Finder

JF-Expert Member
Jan 25, 2012
1,119
1,388
Baada ya kukagua nyumba yao, wenye nyumba wanaweza kuchagua kuibomoa au kuirekebisha. JE, NDOA yako imefikia hatua hiyo? Huenda mwenzi wako amekosa kuwa mwaminifu au ugomvi wa kila mara umefanya uhusiano wenu usiwe wenye furaha. Ikiwa ndivyo, huenda ukajiambia, ‘Hatupendani tena’ au ‘Hatufaani’ au ‘Hatukujua tulichokuwa tukifanya tulipofunga ndoa.’ Huenda hata ukajiambia, ‘Labda ingefaa tutalikiane.’ Kabla ya kufanya uamuzi wa haraka wa kuvunja ndoa yako, fikiria. Mara nyingi talaka haimalizi mahangaiko ya maisha. Badala yake, inatatua tatizo moja, na kutokeza lingine.

Katika kitabu chake, The Good Enough Teen, Dakt. Brad Sachs anaonya hivi: “Wenzi wa ndoa wanaotalikiana huwazia kwamba kufanya hivyo kutafaa kabisa, yaani, talaka yao itawaondolea kabisa huzuni na ugomvi mkali, na badala yake wapate utulivu mwanana. Lakini kutarajia hilo ni sawa tu na kutarajia kuwa na ndoa kamilifu, haiwezekani.” Hivyo, ni muhimu kuwa na habari kamili na kuona talaka kihalisi. Maoni ya Biblia Kuhusu Talaka Biblia huona talaka kuwa jambo zito. Inasema kwamba Yehova Mungu huliona kuwa tendo la hila na chuki ikiwa mtu atamwacha mwenzi wake kwa sababu zisizo za maana, pengine akiwa na nia ya kumchukua mwenzi mwingine. (Malaki 2:13-16) Ndoa ni kifungo cha kudumu. (Mathayo 19:6)

Ndoa nyingi ambazo huvunjika kwa sababu zisizo na msingi zingedumu ikiwa wenzi wa ndoa wangesameheana zaidi.—Mathayo 18:21, 22. Wakati huohuo, Biblia inaruhusu sababu moja tu ya talaka na kufunga ndoa tena—mahusiano ya kingono nje ya ndoa. (Mathayo 19:9) Kwa hiyo, ukigundua kwamba mwenzi wako amekosa kuwa mwaminifu, una haki ya kuvunja ndoa hiyo. Wengine hawapaswi kukulazimisha ukubali maoni yao, na habari hii haikukusudiwa kukuambia kile unachopaswa kufanya.

Uamuzi utakaofanya utakuathiri wewe binafsi; kwa hiyo, uamuzi ni wako.— Wagalatia 6:5. Hata hivyo, Biblia inasema hivi: “Mtu mwerevu huzifikiria hatua zake.” (Methali 14:15) Kwa hiyo, hata ikiwa una msingi wa Kimaandiko wa kupata talaka, lingekuwa jambo linalofaa kufikiria kwa uzito yote yanayohusika. (1 Wakorintho 6:12) “Huenda mtu akafikiri kwamba anapaswa kufanya uamuzi wa haraka,” anasema David, anayeishi Uingereza. “Lakini baada ya kupitia talaka, ninaweza kusema kwamba mtu anahitaji wakati wa kufikiria jambo hilo.”

Acheni tuzungumzie mambo manne muhimu ambayo unahitaji kufikiria.

1. Matatizo ya Kifedha

Daniella, anayeishi Italia, alikuwa katika ndoa kwa miaka 12 alipogundua kwamba mume wake alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mfanyakazi mwenzake. Daniella anasema hivi: “Nilipogundua jambo hilo, mwanamke huyo alikuwa na mimba ya miezi sita.” Baada ya kutengana kwa muda, Daniella aliamua kumtaliki mume wake. “Nilijaribu kuiokoa ndoa yangu,” anasema, “lakini mume wangu hakuacha kuwa na uhusiano nje ya ndoa.” Daniella anahisi kwamba alifanya uamuzi unaofaa.

Lakini anasema hivi: “Mara tu tulipotengana, hali yangu ya kiuchumi ikawa mbaya. Nyakati nyingine nilikosa hata mlo wa jioni. Nilikunywa tu maziwa.” Maria, nchini Hispania, alipatwa na hali kama hiyo ya kiuchumi. “Mume wangu wa zamani hatupi msaada wowote wa kifedha,” anasema, “na inabidi nifanye kazi kwa bidii ili nilipe madeni aliyoacha. Pia nililazimika kuhama kutoka nyumba yetu kubwa hadi kwenye nyumba ndogo katika eneo lisilo salama.” Kama visa hivyo vinavyoonyesha, kuvunjika kwa ndoa kunaweza kuwaletea wanawake matatizo makubwa ya kifedha. Kwa kweli, uchunguzi uliofanywa tafadhali zingatia kwamba hakuna yeyote kati ya wale walionukuliwa anayesema kwamba alifanya uamuzi usiofaa. Hata hivyo, maelezo yao yanakazia baadhi ya matatizo ambayo mara nyingi hutokea miezi au hata miaka mingi baada ya ndoa kuvunjika.

Huko Ulaya katika kipindi cha miaka saba ulionyesha kwamba baada ya talaka, mapato ya wanaume huongezeka kwa asilimia 11 na yale ya wanawake hupungua kwa asilimia 17. “Wanawake fulani hupitia hali ngumu,” anasema Mieke Jansen, ambaye alisimamia uchunguzi huo, “kwa sababu lazima wawatunze watoto, watafute kazi, na pia wakabiliane na madhara ya kihisia ya talaka.” Gazeti Daily Telegraph la London lilisema kwamba kulingana na mawakili fulani, matatizo kama hayo “yanawafanya watu wafikirie kwa uzito kabla ya kuamua kutengana.”

Huenda hili likatokea: Mkitalikiana, huenda mapato yako yakapungua. Huenda pia ukalazimika kuhama. Ikiwa umepewa haki ya kuwalea watoto, huenda ikawa vigumu kujitegemeza na kuwaandalia watoto mahitaji yao kwa njia inayofaa.—1 Timotheo 5:8. ‘HAKI YA KILA MTOTO ANAPOZALIWA’ “Nilipokuwa na umri wa miaka mitano, baba yangu alikuwa na uhusiano wa kimapenzi wa muda mfupi na karani wake, na wazazi wangu wakatalikiana.
Wote wawili walinitunza vizuri. Walinihakikishia kwamba ingawa hawakupendana tena, bado walinipenda, na baada ya baba yangu kuanza kuishi peke yake upande ule mwingine wa mji, wote wawili waliendelea kuniandalia mahitaji yangu ya kimwili. “Miaka miwili baadaye, mama yangu aliolewa tena na tukahamia nga’mbo. Miaka kadhaa ilipita kabla ya mimi kumwona baba yangu. Nimemwona mara moja tu katika muda wa miaka tisa iliyopita. Hakuona nikikua, naye hawafahamu watoto wangu watatu—wajukuu wake—isipokuwa kupitia barua na picha ambazo mimi humtumia. Watoto wangu wamekua bila kuwa na uhusiano na babu yao.

“Nikiwa mtoto aliyelelewa na wazazi waliotalikiana, sikuwa na matatizo yoyote ambayo yangeonekana wazi nilipokuwa nikikua. Lakini ndani yangu nilipambana na hisia kali za hasira, kushuka moyo, na wasiwasi mwingi bila kujua ni kwa nini. Sikumwamini mwanamume yeyote. Nilipokuwa na umri wa zaidi ya miaka 30 ndipo tu niliposaidiwa na rafiki mmoja mkomavu kujua ni kwa nini nilikuwa na uhasama na nikaanza kuchukua hatua ya kuondoa hisia hizo. “Talaka ya wazazi wangu ilininyima haki ambayo kila mtoto huwa nayo anapozaliwa, yaani, kujihisi akiwa salama na kulindwa. Ulimwengu una ubaridi na unaogopesha, lakini mimi huona kwamba familia ni kama ukuta unaomkinga mtu dhidi ya mambo hayo, mahali ambapo watoto wanaweza kuhisi kwamba wametulia na kwamba wanatunzwa. Ukivunja familia, basi ukuta huo wenye kinga unaporomoka.”—Diane.

2. Matatizo ya Kuwalea Watoto

“Nilishtuka sana nilipogundua kwamba mume wangu hakuwa mwaminifu kwangu,” anasema Jane anayeishi Uingereza. “Pia, nilifadhaika sana nilipogundua kwamba alikuwa ameamua kutuacha.” Jane alimtaliki mume wake. Bado anaamini kwamba alifanya uamuzi unaofaa, lakini anakiri hivi: “Tatizo moja nililokabili ni kuchukua jukumu la kuwa mama na baba ya watoto wangu. Nililazimika kufanya maamuzi yote nikiwa peke yangu.” Graciela anayeishi Hispania, ambaye alitalikiana na mume wake anakabili tatizo hilohilo. “Nilipewa haki ya kumlea mwana wangu mwenye umri wa miaka 16,” anasema. “Lakini kipindi cha kubalehe ni wakati mgumu sana, na sikuwa nimejitayarisha vizuri kumlea mwana wangu nikiwa peke yangu. Nililia sana mchana na usiku. Sikuhisi kwamba nilikuwa mama mzuri.”

Huenda kukawa na matatizo zaidi wazazi wote wawili wanapopewa haki ya kulea watoto. Huenda ikabidi mjadiliane na mwenzi wako wa zamani kuhusu mambo yanayoweza kuzua ugomvi kama vile ratiba ya kumtembelea mtoto, pesa za kumtegemeza, na nidhamu. Christine, mama aliyetalikiana na mume wake huko Marekani anasema hivi: “Si rahisi kuwa na uhusiano mzuri na mwenzi mliyetalikiana. Hisia nyingi zinahusika, na usipokuwa mwangalifu, unaweza kuanza.

3. Jinsi Talaka Inavyokuathiri

Mark, anayeishi Uingereza anasema kwamba mke wake alikuwa na uhusiano nje ya ndoa zaidi ya mara moja. “Alipofanya hivyo mara ya pili,” Mark anasema, “singeweza kuvumilia wazo la kwamba anaweza kufanya hivyo tena.” Ingawa Mark alimtaliki mke wake, aligundua kwamba bado alikuwa anampenda. “Watu wanaposema mambo mabaya kumhusu, wanafikiri kwamba wananisaidia; lakini sivyo,” anasema. “Upendo hudumu kwa muda mrefu.” David, aliyenukuliwa hapo awali alihuzunika sana alipogundua kwamba mke wake alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamume mwingine.

“Sikuamini kabisa,” anasema. “Kwa kweli nilitaka sana kuishi pamoja naye na watoto wetu maisha yangu yote.” David aliamua kumtaliki lakini hilo lilimwacha akiwa na shaka kuhusu wakati wake ujao. “Nilijiuliza ikiwa kweli mtu angeweza kunipenda au ikiwa nikioa tena ndoa hiyo itaishia kwenye talaka,” anasema. “Sikujiamini tena.” Ikiwa wewe na mwenzi wako mmetalikiana, ni jambo la kawaida kwamba utapatwa na hisia mbalimbali. Kwa upande mmoja, huenda bado unampenda mtu huyo ambaye mlikuwa mwili mmoja. (Mwanzo 2:24).

Kwa upande ule mwingine, huenda ukamchukia. Graciela, ambaye alinukuliwa awali anasema: “Hata baada ya miaka kadhaa, huenda ukahisi kumtumia mtoto wako kupata kile unachotaka kutoka kwa mwenzi wako wa zamani.” Huenda hili likatokea: Huenda usipende mipango ambayo mahakama imeamua kuhusu kuwalea watoto. Ikiwa nyote wawili mmepewa haki ya kuwalea watoto, huenda mwenzi wako wa zamani asiwe na maoni yenye usawaziko kuhusu kuwatembelea watoto, kuwategemeza kifedha, na kadhalika.

4. Jinsi Talaka Inavyowaathiri Watoto

“Niliumia sana,” anasema José, baba aliyetalikiana na mke wake huko Hispania. “Niliumia hata zaidi nilipogundua kwamba mume wa dada yangu ndiye aliyekuwa mpenzi wa mke wangu. Nilitaka tu kufa.” José aligundua kwamba umechanganyikiwa, umeaibishwa, na hoi. Unapofikiria pindi zenye furaha mlizokuwa nazo, huenda ukawaza: ‘Alikuwa akiniambia kuwa hawezi kuishi bila mimi. Je, alikuwa akisema uwongo? Kwa nini mambo haya yalitukia?’” Huenda hili likatokea: Huenda bado ukawa na hasira na chuki kwa sababu ya jinsi mwenzi wako alivyokutendea vibaya. Nyakati nyingine, huenda ukalemewa na upweke.—Methali 14:29; 18:1. Wavulana wake wawili, wenye umri wa miaka miwili na minne, waliathiriwa pia na mwenendo wa mama yao. “Hawangeweza kuelewa hali hiyo,” anasema.

“Hawakuelewa kwa nini mama yao alikuwa akiishi na mjomba wao na kwa nini mimi, dada yangu na mama yangu tuliishi pamoja. Nilipotaka kwenda mahali popote, waliniuliza, ‘Utarudi saa ngapi?’ au walisema, ‘Baba, usituache!’” Mara nyingi watoto wanakuwa majeruhi waliosahauliwa katika uwanja wa vita vya talaka. Lakini namna gani ikiwa wazazi wote wawili wanazozana kila wakati? Katika kisa kama hicho, je, kweli talaka “itawafaidi watoto”?

Katika miaka ya hivi karibuni, wazo hilo limepingwa vikali—hasa wakati ambapo matatizo ya ndoa si mabaya sana. Kitabu The Unexpected Legacy of Divorce kinasema hivi: “Watu wengi wazima ambao wamenaswa katika ndoa zisizo na furaha watashangaa kujua kwamba watoto wao wanaridhika na jinsi hali ilivyo. Hawajali ikiwa Mama na Baba wanalala katika vitanda tofauti maadamu tu familia iko pamoja.”

Ni kweli kwamba watoto hujua wakati wazazi wanapozozana, na mkazo katika ndoa unaweza kuathiri sana akili na mioyo yao. Hata hivyo, ni makosa kukata kauli haraka kwamba talaka itawafaidi watoto. “Inaonekana kwamba ndoa inawapa wazazi msingi mzuri wa kutoa nidhamu inayofaa ambayo watoto hukubali, hata ikiwa ndoa hiyo ina matatizo,” wanasema Linda J. Waite na Maggie Gallagher katika kitabu chao, The Case for Marriage.

Huenda hili likatokea: Talaka inaweza kuwaathiri vibaya sana watoto wako hasa ikiwa huwatii moyo wawe na uhusiano mzuri na mwenzi wako wa zamani.—Ona sanduku “Nimenaswa Katikati.” Makala hii imezungumzia mambo manne unayopaswa kufikiria kabla ya kumtaliki mwenzi wako. Kama ilivyoelezwa awali, ikiwa mwenzi wako si mwaminifu, uamuzi ni wako. Hata hivyo, tambua kwamba unahitaji kutambua madhara ya uamuzi wowote utakaofanya. Fahamu ni matatizo gani utakayopata, na uwe tayari kukabiliana nayo.

Baada ya kufikiria jambo hilo, huenda ukaamua kwamba ni afadhali zaidi kujaribu kuboresha ndoa yako. Lakini je, kweli hilo linawezekana? “NIMENASWA KATIKATI” “Wazazi wangu walitalikiana nilipokuwa na umri wa miaka 12. Kwa kiasi fulani nilifurahi. Kulikuwa na utulivu na amani nyumbani kwa kuwa hakukuwa na ugomvi kati yao kama ilivyokuwa hapo awali. Lakini bado nilikuwa nimechanganyikiwa. “Baada ya talaka, nilitaka kuwa na uhusiano mzuri na wazazi wangu, na nilijaribu sana kutojihusisha katika mambo yao. Lakini haidhuru nilifanya nini, bado nilijihisi ni kama nimenaswa katikati.

Baba yangu aliniambia alikuwa na wasiwasi kwamba mama angefanya nimchukie. Hivyo, kila mara ilibidi nimhakikishie kwamba mama hakuwa akijaribu kufanya hivyo. Mama pia alikuwa na wasiwasi mwingi. Aliogopa kwamba nilikuwa nikisikiliza mambo mabaya ambayo baba alikuwa akisema kumhusu. Hali hiyo ilikuwa mbaya hivi kwamba singewaeleza wazazi wangu hisia zangu kwa kuwa sikutaka kuwaumiza. Kwa hiyo, tangu nilipokuwa na umri wa miaka 12 na kuendelea, sikumweleza yeyote jinsi nilivyohisi kuhusu talaka yao.”— Sandra.
 
Mwenyewe nimeshindwa nikaona nidondoshe maneno machache sijui kama nimepatia lengo la mtoa mada.
 
Daniella na Maria ni kama wenzao wanaopenda kukaa chini na kutegemea wanaume 150%, kabisa hata kukosa mlo mwenyewe DUH. Ila lazima walijifunza kujitafutia pesa zao.

Hii kitu kwa mwanamke anayevuta pesa, anajielewa na amejipanga haitamsumbua kabisa.

Mengine nitasoma baadae as nimeishia hapo.
 
Baada ya kukagua nyumba yao, wenye nyumba wanaweza kuchagua kuibomoa au kuirekebisha. JE, NDOA yako imefikia hatua hiyo? Huenda mwenzi wako amekosa kuwa mwaminifu au ugomvi wa kila mara umefanya uhusiano wenu usiwe wenye furaha. Ikiwa ndivyo, huenda ukajiambia, ‘Hatupendani tena’ au ‘Hatufaani’ au ‘Hatukujua tulichokuwa tukifanya tulipofunga ndoa.’ Huenda hata ukajiambia, ‘Labda ingefaa tutalikiane.’ Kabla ya kufanya uamuzi wa haraka wa kuvunja ndoa yako, fikiria. Mara nyingi talaka haimalizi mahangaiko ya maisha. Badala yake, inatatua tatizo moja, na kutokeza lingine.

Katika kitabu chake, The Good Enough Teen, Dakt. Brad Sachs anaonya hivi: “Wenzi wa ndoa wanaotalikiana huwazia kwamba kufanya hivyo kutafaa kabisa, yaani, talaka yao itawaondolea kabisa huzuni na ugomvi mkali, na badala yake wapate utulivu mwanana. Lakini kutarajia hilo ni sawa tu na kutarajia kuwa na ndoa kamilifu, haiwezekani.” Hivyo, ni muhimu kuwa na habari kamili na kuona talaka kihalisi. Maoni ya Biblia Kuhusu Talaka Biblia huona talaka kuwa jambo zito. Inasema kwamba Yehova Mungu huliona kuwa tendo la hila na chuki ikiwa mtu atamwacha mwenzi wake kwa sababu zisizo za maana, pengine akiwa na nia ya kumchukua mwenzi mwingine. (Malaki 2:13-16) Ndoa ni kifungo cha kudumu. (Mathayo 19:6)

Ndoa nyingi ambazo huvunjika kwa sababu zisizo na msingi zingedumu ikiwa wenzi wa ndoa wangesameheana zaidi.—Mathayo 18:21, 22. Wakati huohuo, Biblia inaruhusu sababu moja tu ya talaka na kufunga ndoa tena—mahusiano ya kingono nje ya ndoa. (Mathayo 19:9) Kwa hiyo, ukigundua kwamba mwenzi wako amekosa kuwa mwaminifu, una haki ya kuvunja ndoa hiyo. Wengine hawapaswi kukulazimisha ukubali maoni yao, na habari hii haikukusudiwa kukuambia kile unachopaswa kufanya.

Uamuzi utakaofanya utakuathiri wewe binafsi; kwa hiyo, uamuzi ni wako.— Wagalatia 6:5. Hata hivyo, Biblia inasema hivi: “Mtu mwerevu huzifikiria hatua zake.” (Methali 14:15) Kwa hiyo, hata ikiwa una msingi wa Kimaandiko wa kupata talaka, lingekuwa jambo linalofaa kufikiria kwa uzito yote yanayohusika. (1 Wakorintho 6:12) “Huenda mtu akafikiri kwamba anapaswa kufanya uamuzi wa haraka,” anasema David, anayeishi Uingereza. “Lakini baada ya kupitia talaka, ninaweza kusema kwamba mtu anahitaji wakati wa kufikiria jambo hilo.”

Acheni tuzungumzie mambo manne muhimu ambayo unahitaji kufikiria.

1. Matatizo ya Kifedha

Daniella, anayeishi Italia, alikuwa katika ndoa kwa miaka 12 alipogundua kwamba mume wake alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mfanyakazi mwenzake. Daniella anasema hivi: “Nilipogundua jambo hilo, mwanamke huyo alikuwa na mimba ya miezi sita.” Baada ya kutengana kwa muda, Daniella aliamua kumtaliki mume wake. “Nilijaribu kuiokoa ndoa yangu,” anasema, “lakini mume wangu hakuacha kuwa na uhusiano nje ya ndoa.” Daniella anahisi kwamba alifanya uamuzi unaofaa.

Lakini anasema hivi: “Mara tu tulipotengana, hali yangu ya kiuchumi ikawa mbaya. Nyakati nyingine nilikosa hata mlo wa jioni. Nilikunywa tu maziwa.” Maria, nchini Hispania, alipatwa na hali kama hiyo ya kiuchumi. “Mume wangu wa zamani hatupi msaada wowote wa kifedha,” anasema, “na inabidi nifanye kazi kwa bidii ili nilipe madeni aliyoacha. Pia nililazimika kuhama kutoka nyumba yetu kubwa hadi kwenye nyumba ndogo katika eneo lisilo salama.” Kama visa hivyo vinavyoonyesha, kuvunjika kwa ndoa kunaweza kuwaletea wanawake matatizo makubwa ya kifedha. Kwa kweli, uchunguzi uliofanywa tafadhali zingatia kwamba hakuna yeyote kati ya wale walionukuliwa anayesema kwamba alifanya uamuzi usiofaa. Hata hivyo, maelezo yao yanakazia baadhi ya matatizo ambayo mara nyingi hutokea miezi au hata miaka mingi baada ya ndoa kuvunjika.

Huko Ulaya katika kipindi cha miaka saba ulionyesha kwamba baada ya talaka, mapato ya wanaume huongezeka kwa asilimia 11 na yale ya wanawake hupungua kwa asilimia 17. “Wanawake fulani hupitia hali ngumu,” anasema Mieke Jansen, ambaye alisimamia uchunguzi huo, “kwa sababu lazima wawatunze watoto, watafute kazi, na pia wakabiliane na madhara ya kihisia ya talaka.” Gazeti Daily Telegraph la London lilisema kwamba kulingana na mawakili fulani, matatizo kama hayo “yanawafanya watu wafikirie kwa uzito kabla ya kuamua kutengana.”

Huenda hili likatokea: Mkitalikiana, huenda mapato yako yakapungua. Huenda pia ukalazimika kuhama. Ikiwa umepewa haki ya kuwalea watoto, huenda ikawa vigumu kujitegemeza na kuwaandalia watoto mahitaji yao kwa njia inayofaa.—1 Timotheo 5:8. ‘HAKI YA KILA MTOTO ANAPOZALIWA’ “Nilipokuwa na umri wa miaka mitano, baba yangu alikuwa na uhusiano wa kimapenzi wa muda mfupi na karani wake, na wazazi wangu wakatalikiana.
Wote wawili walinitunza vizuri. Walinihakikishia kwamba ingawa hawakupendana tena, bado walinipenda, na baada ya baba yangu kuanza kuishi peke yake upande ule mwingine wa mji, wote wawili waliendelea kuniandalia mahitaji yangu ya kimwili. “Miaka miwili baadaye, mama yangu aliolewa tena na tukahamia nga’mbo. Miaka kadhaa ilipita kabla ya mimi kumwona baba yangu. Nimemwona mara moja tu katika muda wa miaka tisa iliyopita. Hakuona nikikua, naye hawafahamu watoto wangu watatu—wajukuu wake—isipokuwa kupitia barua na picha ambazo mimi humtumia. Watoto wangu wamekua bila kuwa na uhusiano na babu yao.

“Nikiwa mtoto aliyelelewa na wazazi waliotalikiana, sikuwa na matatizo yoyote ambayo yangeonekana wazi nilipokuwa nikikua. Lakini ndani yangu nilipambana na hisia kali za hasira, kushuka moyo, na wasiwasi mwingi bila kujua ni kwa nini. Sikumwamini mwanamume yeyote. Nilipokuwa na umri wa zaidi ya miaka 30 ndipo tu niliposaidiwa na rafiki mmoja mkomavu kujua ni kwa nini nilikuwa na uhasama na nikaanza kuchukua hatua ya kuondoa hisia hizo. “Talaka ya wazazi wangu ilininyima haki ambayo kila mtoto huwa nayo anapozaliwa, yaani, kujihisi akiwa salama na kulindwa. Ulimwengu una ubaridi na unaogopesha, lakini mimi huona kwamba familia ni kama ukuta unaomkinga mtu dhidi ya mambo hayo, mahali ambapo watoto wanaweza kuhisi kwamba wametulia na kwamba wanatunzwa. Ukivunja familia, basi ukuta huo wenye kinga unaporomoka.”—Diane.

2. Matatizo ya Kuwalea Watoto

“Nilishtuka sana nilipogundua kwamba mume wangu hakuwa mwaminifu kwangu,” anasema Jane anayeishi Uingereza. “Pia, nilifadhaika sana nilipogundua kwamba alikuwa ameamua kutuacha.” Jane alimtaliki mume wake. Bado anaamini kwamba alifanya uamuzi unaofaa, lakini anakiri hivi: “Tatizo moja nililokabili ni kuchukua jukumu la kuwa mama na baba ya watoto wangu. Nililazimika kufanya maamuzi yote nikiwa peke yangu.” Graciela anayeishi Hispania, ambaye alitalikiana na mume wake anakabili tatizo hilohilo. “Nilipewa haki ya kumlea mwana wangu mwenye umri wa miaka 16,” anasema. “Lakini kipindi cha kubalehe ni wakati mgumu sana, na sikuwa nimejitayarisha vizuri kumlea mwana wangu nikiwa peke yangu. Nililia sana mchana na usiku. Sikuhisi kwamba nilikuwa mama mzuri.”

Huenda kukawa na matatizo zaidi wazazi wote wawili wanapopewa haki ya kulea watoto. Huenda ikabidi mjadiliane na mwenzi wako wa zamani kuhusu mambo yanayoweza kuzua ugomvi kama vile ratiba ya kumtembelea mtoto, pesa za kumtegemeza, na nidhamu. Christine, mama aliyetalikiana na mume wake huko Marekani anasema hivi: “Si rahisi kuwa na uhusiano mzuri na mwenzi mliyetalikiana. Hisia nyingi zinahusika, na usipokuwa mwangalifu, unaweza kuanza.

3. Jinsi Talaka Inavyokuathiri

Mark, anayeishi Uingereza anasema kwamba mke wake alikuwa na uhusiano nje ya ndoa zaidi ya mara moja. “Alipofanya hivyo mara ya pili,” Mark anasema, “singeweza kuvumilia wazo la kwamba anaweza kufanya hivyo tena.” Ingawa Mark alimtaliki mke wake, aligundua kwamba bado alikuwa anampenda. “Watu wanaposema mambo mabaya kumhusu, wanafikiri kwamba wananisaidia; lakini sivyo,” anasema. “Upendo hudumu kwa muda mrefu.” David, aliyenukuliwa hapo awali alihuzunika sana alipogundua kwamba mke wake alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamume mwingine.

“Sikuamini kabisa,” anasema. “Kwa kweli nilitaka sana kuishi pamoja naye na watoto wetu maisha yangu yote.” David aliamua kumtaliki lakini hilo lilimwacha akiwa na shaka kuhusu wakati wake ujao. “Nilijiuliza ikiwa kweli mtu angeweza kunipenda au ikiwa nikioa tena ndoa hiyo itaishia kwenye talaka,” anasema. “Sikujiamini tena.” Ikiwa wewe na mwenzi wako mmetalikiana, ni jambo la kawaida kwamba utapatwa na hisia mbalimbali. Kwa upande mmoja, huenda bado unampenda mtu huyo ambaye mlikuwa mwili mmoja. (Mwanzo 2:24).

Kwa upande ule mwingine, huenda ukamchukia. Graciela, ambaye alinukuliwa awali anasema: “Hata baada ya miaka kadhaa, huenda ukahisi kumtumia mtoto wako kupata kile unachotaka kutoka kwa mwenzi wako wa zamani.” Huenda hili likatokea: Huenda usipende mipango ambayo mahakama imeamua kuhusu kuwalea watoto. Ikiwa nyote wawili mmepewa haki ya kuwalea watoto, huenda mwenzi wako wa zamani asiwe na maoni yenye usawaziko kuhusu kuwatembelea watoto, kuwategemeza kifedha, na kadhalika.

4. Jinsi Talaka Inavyowaathiri Watoto

“Niliumia sana,” anasema José, baba aliyetalikiana na mke wake huko Hispania. “Niliumia hata zaidi nilipogundua kwamba mume wa dada yangu ndiye aliyekuwa mpenzi wa mke wangu. Nilitaka tu kufa.” José aligundua kwamba umechanganyikiwa, umeaibishwa, na hoi. Unapofikiria pindi zenye furaha mlizokuwa nazo, huenda ukawaza: ‘Alikuwa akiniambia kuwa hawezi kuishi bila mimi. Je, alikuwa akisema uwongo? Kwa nini mambo haya yalitukia?’” Huenda hili likatokea: Huenda bado ukawa na hasira na chuki kwa sababu ya jinsi mwenzi wako alivyokutendea vibaya. Nyakati nyingine, huenda ukalemewa na upweke.—Methali 14:29; 18:1. Wavulana wake wawili, wenye umri wa miaka miwili na minne, waliathiriwa pia na mwenendo wa mama yao. “Hawangeweza kuelewa hali hiyo,” anasema.

“Hawakuelewa kwa nini mama yao alikuwa akiishi na mjomba wao na kwa nini mimi, dada yangu na mama yangu tuliishi pamoja. Nilipotaka kwenda mahali popote, waliniuliza, ‘Utarudi saa ngapi?’ au walisema, ‘Baba, usituache!’” Mara nyingi watoto wanakuwa majeruhi waliosahauliwa katika uwanja wa vita vya talaka. Lakini namna gani ikiwa wazazi wote wawili wanazozana kila wakati? Katika kisa kama hicho, je, kweli talaka “itawafaidi watoto”?

Katika miaka ya hivi karibuni, wazo hilo limepingwa vikali—hasa wakati ambapo matatizo ya ndoa si mabaya sana. Kitabu The Unexpected Legacy of Divorce kinasema hivi: “Watu wengi wazima ambao wamenaswa katika ndoa zisizo na furaha watashangaa kujua kwamba watoto wao wanaridhika na jinsi hali ilivyo. Hawajali ikiwa Mama na Baba wanalala katika vitanda tofauti maadamu tu familia iko pamoja.”

Ni kweli kwamba watoto hujua wakati wazazi wanapozozana, na mkazo katika ndoa unaweza kuathiri sana akili na mioyo yao. Hata hivyo, ni makosa kukata kauli haraka kwamba talaka itawafaidi watoto. “Inaonekana kwamba ndoa inawapa wazazi msingi mzuri wa kutoa nidhamu inayofaa ambayo watoto hukubali, hata ikiwa ndoa hiyo ina matatizo,” wanasema Linda J. Waite na Maggie Gallagher katika kitabu chao, The Case for Marriage.

Huenda hili likatokea: Talaka inaweza kuwaathiri vibaya sana watoto wako hasa ikiwa huwatii moyo wawe na uhusiano mzuri na mwenzi wako wa zamani.—Ona sanduku “Nimenaswa Katikati.” Makala hii imezungumzia mambo manne unayopaswa kufikiria kabla ya kumtaliki mwenzi wako. Kama ilivyoelezwa awali, ikiwa mwenzi wako si mwaminifu, uamuzi ni wako. Hata hivyo, tambua kwamba unahitaji kutambua madhara ya uamuzi wowote utakaofanya. Fahamu ni matatizo gani utakayopata, na uwe tayari kukabiliana nayo.

Baada ya kufikiria jambo hilo, huenda ukaamua kwamba ni afadhali zaidi kujaribu kuboresha ndoa yako. Lakini je, kweli hilo linawezekana? “NIMENASWA KATIKATI” “Wazazi wangu walitalikiana nilipokuwa na umri wa miaka 12. Kwa kiasi fulani nilifurahi. Kulikuwa na utulivu na amani nyumbani kwa kuwa hakukuwa na ugomvi kati yao kama ilivyokuwa hapo awali. Lakini bado nilikuwa nimechanganyikiwa. “Baada ya talaka, nilitaka kuwa na uhusiano mzuri na wazazi wangu, na nilijaribu sana kutojihusisha katika mambo yao. Lakini haidhuru nilifanya nini, bado nilijihisi ni kama nimenaswa katikati.

Baba yangu aliniambia alikuwa na wasiwasi kwamba mama angefanya nimchukie. Hivyo, kila mara ilibidi nimhakikishie kwamba mama hakuwa akijaribu kufanya hivyo. Mama pia alikuwa na wasiwasi mwingi. Aliogopa kwamba nilikuwa nikisikiliza mambo mabaya ambayo baba alikuwa akisema kumhusu. Hali hiyo ilikuwa mbaya hivi kwamba singewaeleza wazazi wangu hisia zangu kwa kuwa sikutaka kuwaumiza. Kwa hiyo, tangu nilipokuwa na umri wa miaka 12 na kuendelea, sikumweleza yeyote jinsi nilivyohisi kuhusu talaka yao.”— Sandra.


WAKUU,
ATAKAYEPATA SAMARI YAKE ANIJUZE!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom