Kwa wanaojua hii kitu (rupia)

Kwa wanaojua hii kitu (rupia)

G.25

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2013
Posts
1,788
Reaction score
1,966
Wakati niko mdogo niliwai kusikia watu/mtu akipata rupia anakuwa tajiri sana, sasa mwezi uliopita nilikuwa nasimamia mgodi wa moonston Songambele ya matui.

Wakaja watu 2 kijijini wantafuta rupia, nikashangaa xana! kila nilivojaribu kuwauliza husu hizo rupia hawajawai kuziona! lakini wanasema huwa zinakuwa kwenye masanduku walioacha wajerumani na kwa hali ya kawaida huwezi kuyaona mpaka upitie kwa wazee wa matmbiko au waganga wa jadi! Sasa jamani hii kitu rupia ni kweli ipo? Ni nani anaekuwa ananunua? halafu inathamani gani?

Kwa yeyote anaejua zaidi niasaidie kujua hii kitu"
 
Wakati niko mdogo niliwai kusikia watu/mtu akipata rupia anakuwa tajiri sana, sasa mwezi uliopita nilikuwa nasimamia mgodi wa moonston Songambele ya matui. Wakaja watu 2 kijijini wantafuta rupia, nikashangaa xana! kila nilivojaribu kuwauliza husu hizo rupia hawajawai kuziona! lakini wanasema huwa zinakuwa kwenye masanduku walioacha wajerumani na kwa hali ya kawaida huwezi kuyaona mpaka upitie kwa wazee wa matmbiko au waganga wa jadi! Sasa jamani hii kitu rupia ni kweli ipo? Ni nani anaekuwa ananunua? halafu inathamani gani? Kwa yeyote anaejua zaidi niasaidie kujua hii kitu"

Hiyo ni mali mkuu wananunua wajerumani. na sio rupia tu kuna vitu kibao ambavyo ukivipata unakuwa tajiri. Sema rupia zina hela nyingi sana.
MI NAWAFAHAMU JAMAA WA KIJERUMANI WANAONUNUA.
 
jidanyanye ucfanye kaz we jidanyanye sana
 
rupia nyng imetengenezw kw dhahabu uzito gm7.wengi sna wanatumia kw mambo ya ushirikina.kupata rupia halisi nikazi sna
 
kifupi,rupia ni pesa ya wajeruman ilitumika zamani na imetengenezwa kitamadun(kichawi) ucjalibu kununua,ww chimba gemstons
 
ni uzushi ni njia ta kutapeli watu hela wafanyakazi wengi waliyopata kinua mgongo walishalizwa sana hela......hakuna kitu kama hicho ndy ni ya mjerumani lakini ina uzuahi sana g 25.....bora u deal na moonstone hyooooio....rupia utapoteza muda wako bure
 
fanya kazi kwa bidii na maarifa achana na imani za kishirikina, mimi ninayo rupia yenye picha ya simba wawili wanaangalia mnazi, ninayo zaidi ya miaka 9 sasa lakini bado sijapata mtu wa kumuuzia, wanachotaka kufanya hao jamaa ni kwamba watakuahidi kuwa ukiipata watakupa pesa nyingi sana harafu watamtuma mtu kwako akuuzie waliyonayo kwa bei ya mamilioni kadhaa na wewe kwa sababu unajua ina soko utanunua lakini ukiisha inunua tu hutawaona tena hao jamaa, unakuwa umetapeliwa kisayansi kwa maana hata ukiwaona utawakamata kwa kosa gani.
 
mkuu kwa hiyo kwenye huo mgodi ulikuta masanduku ya rupia? ni pm nikuoneshe njia
 
Search humu kuna thread inaelezea hii makitu kwa undani zaidi.
Achana na haya mambo ni utapeli mtupu!
 
fanya kazi kwa bidii na maarifa achana na imani za kishirikina, mimi ninayo rupia yenye picha ya simba wawili wanaangalia mnazi, ninayo zaidi ya miaka 9 sasa lakini bado sijapata mtu wa kumuuzia, wanachotaka kufanya hao jamaa ni kwamba watakuahidi kuwa ukiipata watakupa pesa nyingi sana harafu watamtuma mtu kwako akuuzie waliyonayo kwa bei ya mamilioni kadhaa na wewe kwa sababu unajua ina soko utanunua lakini ukiisha inunua tu hutawaona tena hao jamaa, unakuwa umetapeliwa kisayansi kwa maana hata ukiwaona utawakamata kwa kosa gani.
yapo mengi usiyoyajua kuhusu rupia ya mjerumani,ukweli upo na uongo upo,kama unayo tuwasiliane mi nakupeleka sokoni kisha uje hapa utoe ushuhuda,kuna mengi sana na story za kuvutia kuhusu mali za mjerumani.
 
kweli uchawi,majamaa walishindwa kufukua sanduku la rupia wanakuta joka kubwa limezunguka sanduku mpaka leo somewhere in Tanzania
 
mi hyo kitu nshawahi kusikia na ilikuwa inafanywa na rafiki yangu, kweli kuna masanduku yanatafutwa na huwezi kulipata kiurahisi na yanapatikana huko maporini ambako wajerumani waliyaacha enzi zao nasikia humo ndani kuna utajiri sana na huwezi kulipata kiurahisi hadi uwe na mtu anayeweza kutamka maneno fulani(hasa ukiwa na mjerumani) hivihivi huwezi kulichukua. ila mi naona ushirikina unahusika hapo nasikia hata wakubwa wengi wa nchi wanafight kuyapata hayo masanduku na baadhi wamefanikiwa, na huo utajiri utakaoukuta humo nasikia unamasharti hizo pesa utakazozipata hutakiwi kufanyia starehe wala kudhurumiana.
na kuhusu hizo sarafu, ni kweli zinatafutwa sana sema upatikanaji wake ndo shida kwasababu kuna alama nyingi sana wanazoziangalia.

ni hayo tu ninayoyajua kuhusu hiyo kitu
 
hiyo nshawahi kuisikia eti hapo hadi uende na mtaalam anaeweza kuongea maneno yao ndo huyo nyoka atatoweka.
 
Hamna lolote utalizwa tu, wapo coins collectors wanakusanya mahela ya zamani kwa ajili ya kumbukumbu, lakini ukiambiwa zinatumika kwenye mazingara unatengenezewa usawa wa kutandikwa mapesa!
 
Hamna lolote utalizwa tu, wapo coins collectors wanakusanya mahela ya zamani kwa ajili ya kumbukumbu, lakini ukiambiwa zinatumika kwenye mazingara unatengenezewa usawa wa kutandikwa mapesa!
mkubwa kutapeliwa kupo kila kwenye masuala mengi yanayohusu fedwa,ila ukweli upo hiyo biashara ipo na itaendelea kuwepo ila kama hujui kitu uliza tu na utaelimishwa juu ya mambo haya ya mjerumani lakini si mchezo .
 
mkubwa kutapeliwa kupo kila kwenye masuala mengi yanayohusu fedwa,ila ukweli upo hiyo biashara ipo na itaendelea kuwepo ila kama hujui kitu uliza tu na utaelimishwa juu ya mambo haya ya mjerumani lakini si mchezo .

Treasures zipo, ukiniambia dhahabu iko sehemu nitakuelewa, lakini usiniambie sijui rupia sijui birika la mjerumani hamna lolote, coin pekee ya mjerumani ambayo inatafutwa sana ni 15 Rupia ya mwaka 1916 iliyotengenezwa Tabora, na hiyo ni kwa sababu ilitengenezwa kwa dhahabu, hata hivyo bei yake haizidi 10M!! Haya matakataka mengine sijui ya 1897 hata mimi naweza kukuletea idadi yoyote unayotaka, hayana ishu wanatumia matapeli tu kwa sababu ya upatikanaji wake mgummu.
1897.jpg
 
Kwa hiyo ndo mntaka kutuaminisha kuwa Wajerumani ni washirikina!
 
Back
Top Bottom