Kwa wale tunaonyoa nywele saluni za kiume tueleze kero zetu hapa

kethika

JF-Expert Member
Oct 16, 2015
630
472
Mimi ni mmoja wa watu waonyolea nywele saloon za kiume ila nakerwa na yafuatayo kwenye saloon hizo

1. Kuulizwa kila siku ninayoenda kunyoa kama nataka scrub. Ingekuwa ni mara ya kwanza au ya pili hata ya tatu na ya nne isingekuwa taabu. Mtu unaenda saloon hiyo hiyo mara hata ishirini na hujawahi ku scrub tena unawaeleza kwanini hutaki hiyo scrub lakini hawaishi kukuuliza utadhani ndio masharti waliyopewa na mganga wao. Isitoshe ukikataa wanakasirika.

2. Kusiginwa na matiti ya hao wasichana wanaokuosha. Kifupi niliamua nisiwe nakubali kuoshwa. Ila pia ukifanya hivyo wananuna na baadae wanaungana na hao wakaka wanaonyoa . Unajua sio wote tuoweza kueleza kuwa hatutaki kusiginwa na hayo matiti. Ila inakera. Isitoshe mtu anakuona kabisa kuwa umeoa lakina atafanya hivyo hata mbele ya mkeo uliyeenda nae saloon.

3. Vile vitaulo vya kukuoshea. Mm. Jamani msikasirike wengine tukikataa kuoshwa maana. Kitaulo kitaulo ??????. Mngekuwa mnavichemsha basi.

4. Hizo apron unazofunikwa wakati unanyolewa. Ni bandika bandua. Kama saloon ingekuwa mpya tungesema mtaji mdogo. Saloon ina miaka na miaka hujaweza kununua hata vifaa vya usafi? Apron hiyo hiyo ?????.

5. Hili tu ni swali najiulizaga. Hivi wale wadada wanaoosha watu na kuwafanyia scrub bila kuvaa vitu vya kuwalinda sio hatari kwa afya zao na za wale wanaowahudumia?

Njooni wengine na kero zenu hapa tuwaelimishe hawa ndugu maana yawezekana hawajui na wengi wao wamo humu.
 
Niliwahi nyanyuliwa na wife juujuu toka Saloon mpaka home.Nimeoa mjaluo wa Rorya,wanawake wa Kijaluo wana wivu sana manina.

Ilikuwa weekend,yeye katoka kanisani,nikamwambia nipitie hapa saloon mitaa fulani.Ile anafika pale saloon mi ndio namalizia kunyoa.Mke wangu huwa hasuki,ananyoa nywele fupifupi...Maana kwa asili ni Mjaluo-Msabato,sema mimi nilimbatizisha Katoliki na masacrament yote kapokea.Mambo ya Maranatha hakuna tena,anapiga Cocacola na kambale kama kawa.

Sasa sababu ya mazoea ya kisabato,huwa hasuki kabisa.Kwa hiyo alipoingia pale saloon mi nikawa nimemuona ktk kioo nikatulia.Wale jamaa wa Saloon wakajua anataka na yeye kupunguza nywele.Wakanza kufanya harakaharaka ni wampe huduma.

Kidogo mi nikanyanyuka,dada wa Saloon akaanza kunipukuta,mara kushika kidevu anafuta,mara vidole masikioni kutoa nywele...Nimekaa kidogo yule dada kaleta kopo kaanza kunipaka sijui ku-scrab.Hapo namcheki wife via kioo amekaa anatazama mchezo.

Ngoma ikawa pale kwenye kushikwa shikwa,mara shingo mara kidevu,mara sikio mara kichwa.Ile raha raha mi nafumbafumba macho.Nikasikia sauti huko nyuma,We Baba Olutu,huko ni kunyoa au kurembwa?Maana dada wa saloon ana nyonyo la maana,ananiinamia huku ananiongelesha.Naguswaguswa na nyonyo lainiii...Hazikufika dakika kumi nikaona nanyanyuliwa kwenye kiti na kuvutwa kuwa baba twende nyumbani ntakuosha mwenyewe...Kama ndio hivi,naweza mwenyewe...Kuepusha shari nikalipa na kuondoka na dawa kichwani nikaingia kwa gari mpaka home.....Sijawahi rudi tena ile saloon!!
 
Mimi ni mmoja wa watu waonyolea nywele saloon za kiume ila nakerwa na yafuatayo kwenye saloon hizo
1. Kuulizwa kila siku ninayoenda kunyoa kama nataka scrub. Ingekuwa ni mara ya kwanza au ya pili hata ya tatu na ya nne isingekuwa taabu. Mtu unaenda saloon hiyo hiyo mara hata ishirini na hujawahi ku scrub tena unawaeleza kwanini hutaki hiyo scrub lakini hawaishi kukuuliza utadhani ndio masharti waliyopewa na mganga wao. Isitoshe ukikataa wanakasirika.

2. Kusiginwa na matiti ya hao wasichana wanaokuosha. Kifupi niliamua nisiwe nakubali kuoshwa. Ila pia ukifanya hivyo wananuna na baadae wanaungana na hao wakaka wanaonyoa . Unajua sio wote tuoweza kueleza kuwa hatutaki kusiginwa na hayo matiti. Ila inakera. Isitoshe mtu anakuona kabisa kuwa umeoa lakina atafanya hivyo hata mbele ya mkeo uliyeenda nae saloon.

3. Vile vitaulo vya kukuoshea. Mm. Jamani msikasirike wengine tukikataa kuoshwa maana. Kitaulo kitaulo ??????. Mngekuwa mnavichemsha basi.

4. Hizo apron unazofunikwa wakati unanyolewa. Ni bandika bandua. Kama saloon ingekuwa mpya tungesema mtaji mdogo. Saloon ina miaka na miaka hujaweza kununua hata vifaa vya usafi? Apron hiyo hiyo ?????.
5. Hili tu ni swali najiulizaga. Hivi wale wadada wanaoosha watu na kuwafanyia scrub bila kuvaa vitu vya kuwalinda sio hatari kwa afya zao na za wale wanaowahudumia?

Njooni wengine na kero zenu hapa tuwaelimishe hawa ndugu maana yawezekana hawajui na wengi wao wamo humu.
Sio "Saloon" ni "Salon"
 
Kinyozi kujifanya Kila story anajua. Usishangae ukasikia anasema Madrid ameingia fainal na Juve worldcup.
Wale wadada ving'ang'anizi balaa scrub sitaki, basi dawa ya mba, nayo sitaki, nikuoshe basi nywele sitaki, njoo basi kidogo nikufute sitaki, Uso wako unamafuta njoo basi nifanyie nusu scrabu, sitakii, we kaka bahiriiii

Kutoka na kero inayodhaniwa ni customers care taratibu naanza kufuta vitengo baadhi ninapoenda kunyolewa saloon hizo..
Mtu akisema hatumii huduma flani wadada wa saloon waelewe
 
1) Mi naenda pale na hela iko fixed na budgeted, nishapanga Kunyoa Nywele 3,000 na Ndevu 2,000 jumla 5,000. Sasa mambo ya mhudumu anaeniosha baada ya kunyoa kung'ng'aniza sijui Scrub, Dawa ya Mba, Massage ya Kichwa, Steamer, etc ni kero sana. Tena anang'ng'aniza utafikiri anajua mfukoni nina kiasi gani. Ukimwambia una ratiba zingine haelewi, ukimwambia huna hela anakuambia hata tigopesa we rusha tu.

2) Kero ya pili ni zile Box za kuulia vijidudu wanziita sijui Sterilizer. Nyingi ni feki au zishakufa, wanaingiza kule mashine kama ushahidi tu ili kukuridhisha mteja. Magonjwa mengi jama siku hizi.
 
Sipendi kupakwa spirit/aftershave kwa mikono.
Nilitakaga kumzibua jamaa mmoja kwa hii kitu kwa sababu imeshanisababishia kuambukizwa mba sana.

Kintozi anashika bichwa lenye MBA analisugua na mikono yake haendi kunawa wala nini anakuja anamsugulia mikono MTU mwingine eti anakupaka spirit.
Unaambukizwa MBA na magonjwa kibao ya ngozi
 
Back
Top Bottom