Kwa Tanzania Wezi, malaya na wauza unga ndiyo watu maarufu

Patriot

JF-Expert Member
Feb 11, 2008
5,698
4,693
Ndugu wa-TZ wenzangu, watu wamekuwa wakishangiliwa kutokana na umaarufu wao. Hii siyo tabia iliyoanza awamu ya nne, ni tangu awamu ya pili. Wakati wa mzee rukhsa tuliposhuhudia maeneo ya wazi ktk jiji la Dar yakivamiwa na kujengwa majumba ya kuishi au vituo vya mafuta na hata nyumba za ibada. Viwanja vya shule vilivamiwa kwa mtindo huo huo bila hata serikali kuzuia hali kama hiyo. Kwa ufupi waliokuwa wakiendesha vitendo hivyo ni watu ambao ktk jiji hili la Dar, wanaeleweka kama watu maarufu.

Watu maarufu ktk nchi yetu ni wale wanaofanya vitendo vya hovyo na kwa kiasi kikubwa wakiungwa mkono na wanasiasa waovu. Hiyo ndiyo hali iliyotufikisha hapa tulipo kiasi kwamba kila anayeitwa ni maarufu ni katika kundi la wezi, malaya au wauza mihadarati.

Tanzania hatuna mgunduzi maarufu, au mjenga hoja kama tuonavyo akina P.L.O. Lumumba hapo Kenya. Hatuna tena mwandishi maarufu wa vitabu kama walivyo akina Soyinka au Ngugi wa hapo Kenya. Magazeti maarufu ni yale yanayoandika juu ya umalaya au kutumia picha zao kama biashara. Haya yote ni kwa sababu baadhi ya wanaoendesha jamii, wanasiasa, wameamua kuwa ni watu wa hovyo; ni malaya, ni wezi, ni wauza madawa.

Ukisema hayo wanakuuliza una ushahidi? Lakini ni aibu nchi nzima kumfahamu binti kwa sababu tu anaonekana kila siku ukurasa wa juu wa gazeti. Akikamatwa Afrika kusini kwa madawa, kiongozi wa serikali anafuatilia kumuokoa, ikiwa ishara kwamba wanafahamiana kwa wizi, umalaya au kuuza madawa hayo.

Mmoja wetu aliyejulikana kwa jina la mama Terry aliwahi kuhusisha umalaya unaoendeshwa dodoma na kuwepo kwa Bunge. Akatishiwa na kutaka kuhukumiwa kwa hilo. Lakini, huo ndo ukweli! Tuna watu wasiofaa ktk jamii ambao tumewapa nafasi ya kutulinda ktk jamii na wanadai wawe ni mfano wa kuingwa na waitwe waheshimiwa! Nchi inahitaji kubadilika kwa nguvu yoyote ile. Haitoshi kuwafukuza watumishi waovu, hata wanasiasa wenye upuuzi huu waondolewe kabisa ktk majukwaa ili ifahamike kwamba wao siyo mfano wa kuigwa.

Naomba tuchangie tumpe rais uelekeo wa kunyoosha nchi badala ya kutetea watu tuliodhani ni maarufu.
 
You have a very relevant topic to the situation Tanzania is in now. What do we do to get out of this mess? Of course everything starts from good leadership. To instill good leadership, there are a lot of stumbling blocks to overcome as witnessed under the current leadership. However, we must press on despite these challenges. And, patriotic people must come out to educate the masses on the right path to take. This isn't everyone's cup of tea but it's a war worth fighting.
 
You have a very relevant topic to the situation Tanzania is in now. What do we do to get out of this mess? Of course everything starts from good leadership. To instill good leadership, there are a lot of stumbling blocks to overcome as witnessed under the current leadership. However, we must press on despite these challenges. And, patriotic people must come out to educate the masses on the right path to take. This isn't everyone's cup of tea but it's a war worth fighting.
Nimekuelewa lakini andika kwa kiswahili ili watu wakuelewe zaidi!!
Ni kweli ulichokiandika lakini tumtangulize Mungu zaidi maana vita hii ni Kali sana
 
Kwa hiyo hujui kiswahili?
You have a very relevant topic to the situation Tanzania is in now. What do we do to get out of this mess? Of course everything starts from good leadership. To instill good leadership, there are a lot of stumbling blocks to overcome as witnessed under the current leadership. However, we must press on despite these challenges. And, patriotic people must come out to educate the masses on the right path to take. This isn't everyone's cup of tea but it's a war worth fighting.
 
Ndungu wa-TZ wenzangu, watu wamekuwa wakishangiliwa kutokana na umaarufu wao. Hii siyo tabia iliyoanza awamu ya nne, ni tangu awamu ya pili. Wakati wa mzee rukhsa tuliposhuhudia maeneo ya wazi ktk jiji la Dar yakivamiwa na kujengwa majumba ya kuishi au vituo vya mafuta na hata nyumba za ibada. Viwanja vya shule vilivamiwa kwa mtindo huo huo bila hata serikali kuzuia hali kama hiyo. Kwa ufupi waliokuwa wakiendesha vitendo hivyo ni watu ambao ktk jiji hili la Dar, wanaeleweka kama watu maarufu.

Watu maarufu ktk nchi yetu ni wale wanaofanya vitendo vya hovyo na kwa kiasi kikubwa wakiungwa mkono na wanasiasa waovu. Hiyo ndiyo hali iliyotufikisha hapa tulipo kiasi kwamba kila anayeitwa ni maarufu ni katika kundi la wezi, malaya au wauza mihadarati.

Tanzania hatuna mgunduzi maarufu, au mjenga hoja kama tuonavyo akina P.L.O. Lumumba hapo Kenya. Hatuna tena mwandishi maarufu wa vitabu kama walivyo akina Soyinka au Ngugi wa hapo Kenya. Magazeti maarufu ni yale yanayoandika juu ya umalaya au kutumia picha zao kama biashara. Haya yote ni kwa sababu baadhi ya wanaoendesha jamii, wanasiasa, wameamua kuwa ni watu wa hovyo; ni malaya, ni wezi, ni wauza madawa.

Ukisema hayo wanakuuliza una ushahidi? Lakini ni aibu nchi nzima kumfahamu binti kwa sababu tu anaonekana kila siku ukurasa wa juu wa gazeti. Akikamatwa Afrika kusini kwa madawa, kiongozi wa serikali anafuatilia kumuokoa, ikiwa ishara kwamba wanafahamiana kwa wizi, umalaya au kuuza madawa hayo.

Mmoja wetu aliyejulikana kwa jina la mama Terry aliwahi kuhusisha umalaya unaoendeshwa dodoma na kuwepo kwa Bunge. Akatishiwa na kutaka kuhukumiwa kwa hilo. Lakini, huo ndo ukweli! Tuna watu wasiofaa ktk jamii ambao tumewapa nafasi ya kutulinda ktk jamii na wanadai wawe ni mfano wa kuingwa na waitwe waheshimiwa! Nchi inahitaji kubadilika kwa nguvu yoyote ile. Haitoshi kuwafukuza watumishi waovu, hata wanasiasa wenye upuuzi huu waondolewe kabisa ktk majukwaa ili ifahamike kwamba wao siyo mfano wa kuigwa.

Naomba tuchangie tumpe rais uelekeo wa kunyoosha nchi badala ya kutetea watu tuliodhani ni maarufu.
Mbn mimi maalufu lakini sio Malaya wala siuzi unga!?
 
Kama msingi ukiharibika,mwenye haki atafanya nini?Tunachoshuhudia ni uharibifu wa msingi,fikra mbaya,ibada mbovu,anayewaza sahihi na kutenda hivyo anaonekana ndiye mbaya.Back to our origin tumeshapotea,Tuanze upya.
 
Huu ni ukweli mkuu......na kingine watz tunapenda starehe mno, pesa za fasta na maisha ya hali ya juu kuliko kujishughulisha kitu kinachopelekea kutafuta njia ya mkato kupata hela nyingi kwa muda mfupi ambapo ni deal haram
 
Mkuu umeeleza ukweli mtupu. Taifa limekuwa la ajabu ajabu tu. Hoja za msingi hakuna kila mahali kumegeuka udaku, ukihoji kidogo unaambiwa watu wanrelax, cheka kwa afya nk. Magrupu ya watsapp yanaishia kutuma picha na video za kijinga jinga tu kwa kigezo cha kurefresh. Ukituma video yenye kujifunza watu wakigundua hawaidowlod ama wanaifuta mara moja lakini video za hovyo hukaa muda mrefu.

Ukijaribu kuangalia vipindi vya television habari zao ni zile zile. Skendo ya mtu fulani, mara mapenzi mubashara toka asubuhi hadi usiku, mara shilawadu, sijui chereko nk. Hatuna vipindi vya maana vyenye kuleta fikra mbadala na changamoto za maana kwa vijana. Yani vitu hovyo hovyo ndio vimepewa kipaumbele halafu vile vya maana vimepotezewa, hii ni AIBU kwa taifa. Leo hii wawasilishaji mada wazuri kama kina P.LO Tanzania hakuna. Maprofesa wetu sijui hata wanaushashi gani kwa jamii.

Sijui tuanzie wapi lakini tunapaswa kubadilika. Hapa JF tu hoja za maana zinamichango midogo kuliko hoja nyepesi nyepesi. JF ijaribu kuwa mfano mzuri kwenye hili. Tuwe chachu ya mabadiliko tunayotamani kuyaona.

JF, We go beyond information sharing........
 
MKUU UMEGUSA MAHALI NYETI KABISA,
UKWELI NI KUWA JAMII YA KITANZANIA IMESHAOZA KIMAADILI, KUANZIA JUU KABISA MPAKA CHINI KABISA.
CHUKUA MFANO WA ZINAA, NAKUMBUKA WAKATI TUNAKUA BINTI AMA MWANAMKE KUPATA MTOTO NJE YA NDOA ILIKUWA NI MOJA YA MATUKIO ADIMU KABISA NA AIBU KUBWA KWA FAMILIA HUSIKA. LAKINI LEO NI TUKIO LA KUJISIFIA MBELE YA JAMII KIASI WATOTO WA NJE YA NDOA NI WENGI KULIKO WA HALALI.
WAZAZI TUMEKOSA UADILIFU NA HURUMA KWA WATOTO NA MATOKEO YAKE UTU UMEKUA NI MSAMIATI WA KALE, MUNGU SASA HIVI NI PESA NA MALI.
WATOTO SASA HIVI WANALELEWA NA WASAIDIZI WA KAZI ZA NYUMBANI AMA SHULE ZA BWENI, NA KUTAHAMAKI WASHAKUWA WATU WAZIMA WENYE ELIMU BORA YA DARASANI LAKINI WAKIKOSA KABISA ELIMU YA UTU, UADILIFU NA MAADILI.
MATOKEO WANAKUJA KUWA VIONGOZI KWENYE JAMII KWA USHAWISHI WA MUNGU PESA.
HIVYO TUSITEGEMEE VIONGOZI HAWA KUWAHURUMIA WANANCHI KWANI HAWAJUI KITU KINACHOITWA UADILIFU WALA HURUMA KWA WATU NA JAMII ZAIDI YA FAMILIA ZAO.
 
Back
Top Bottom