TEKNOLOJIA
JF-Expert Member
- Jan 6, 2014
- 4,305
- 2,563
Taifa letu la Tanzania hivi sasa lipo kwenye kipindi kigumu lakini muhimu cha kutengeneza mustakabali wake upya kupitia RASIMU ya Katiba mpya inayojadiliwa Bungeni ili hatimaye ije kuwa Katiba rasmi ya nchi. Rasimu ya Katiba ya Tume ya Jaji Warioba ina mambo mazuri sana ndani yake,Mambo ambayo yanatoa matumaini kwamba sasa taifa hili linaelekea kwenye njia iliyo sahihi kabisa kimaendeleo.Miongoni mwa mambo yanayovutia ndani ya rasimu ya Katiba mpya ni uwepo wa TUNU za taifa kama vile;Uadilifu na Uwazi (Vipengele hivi vimefutwa na wajumbe wa Katiba wanaotokea CCM)
1) Uadilifu-Kilikuwa ni kipengele muhimu sana kuwepo ndani ya Katiba mpya ijayo hasa kwa wakati huu ambao taifa limejawa na wanasiasa wasiokuwa waadilifu. Kipengele cha maadili kilikuwa kinawabana wanasiasa wote waliokuwa na matatizo ya kimaadili huko nyuma wasiweze kupata nafasi za uongozi za ngazi yoyote ile ndani ya nchi.Kwa mfano,Kuna baadhi ya wanasiasa walikumbwa na kashfa mbalimbali za ufisadi nchini kama vile EPA,KAGODA,MEREMETA,RADA,nk.Ha wa wote chini ya kipengele cha maadili walikuwa wameshapoteza sifa za kugombea nafasi yoyote ya ile uongozi hapa Tanzania.Lakini kwasababu Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimekuwa si Chama kinachopigania maslahi ya nchi tena bali ni ngazi inayotumiwa watu flani wenye tamaa ya madaraka na utajiri wa haraka kupanda kwenda kuvuna utajiri huo kwa manufaa yao binafsi kimeamua kukichomoa kipengele hicho kisiwemo kwenye Katiba mpya ijayo.Watu hawa wenye nguvu ya kifedha na ushawishi wa kisiasa ambao wamekiteka nyara Chama Cha Mapinduzi wameshaanza kampeni ya kukiondoa kifungu hiki cha maadili kwani kwao kinaonekana kuwa kizingiti kikubwa katika harakati zao kulihujumu hili taifa.
2) Uwazi-Kama kilivyokuwa kipengele cha maadili,Uwazi nao ni kipengele muhimu sana kinachofaa kuwemo ndani ya Katiba mpya ijayo (Hata hivyo nacho kimeng'olewa na WanaCCM) kwasababu kitaziba mianya ya Mikataba ya ajabu ajabu inayosainiwa na viongozi wa nchi ambayo huishia kuliingizia taifa hasara.Chini ya kipengele cha uwazi,Mikataba mingi ambayo serikali inasaini ingepaswa kupelekwa Bungeni kwa mijadala ya kina zaidi,Hii ingesaidia kudhibiti madudu yanayofanywa na serikali wakati wanaingia mikataba na Mataifa mengine au Makampuni ya kigeni.Uwazi usingeishia tu kwenye kuweka mikataba mbalimbali inayoingiwa na serikali hadharani bali ungejielekeza hadi kwa Waandishi wa habari ambao chini ya kifungu hiki wangeweza kupekuwa habari za ndani kabisa za viongozi na kuzianika hadharani ili umma wa Watanzania ufahamu kinachoendelea ndani ya nchi yao.
Chini ya utaratibu wa sasa waandishi wa habari wakiripoti habari za kichunguzi kwenye vyombo vya habari wanafunguliwa mashtaka sambamba na kuitwa wachochezi na watawala,Na hata baadhi ya vyombo vya habari kufungiwa kama ilivyokuwa kwa magazeti ya M.w.a.n.a.h.a.l.i.s.i na Mtanzania.Waandishi na Maripota wengi wanaofanya habari za kichunguzi wangeweza kulindwa na uwepo wa kipengele hiki.Si hivyo tu,Chini ya kipengele hiki vyombo vya habari vingekuwa na haki ya kikatiba ya kupata taarifa kutoka serikalini na kwenye matawi yake,Kwa kuwepo kwa kipengele hiki inamaama kwamba serikali ingekuwa inafanya shughuli zake katika mazingira ya uwazi zaidi sawa sawa na familia inayoishi kwenye nyumba ya vioo tupu ambapo watu wa nje wanaona kila kitu kinachoendelea ndani ya nyumba.
Kwasababu serikali ya CCM inachukia uwazi imewaagiza makada wake kwenye Bunge maalum la Katiba wakiondoe kipengele cha uwazi,Hii inamaanisha CCM kwa makusudi wameamua kulirudisha taifa kwenye zama za USIRI ambazo zimeligharimu taifa kiuchumi,kiusalama na kijamii. Ili taifa la Tanzania liweze kuwa kule kila mmoja wetu anatamani liwe kimaendeleo ni lazima CCM waondoke madarakani 2015,Hakuna njia.Ili CCM wang'oke madarakani ni lazima Vyama vya Upinzani viungane.
1) Uadilifu-Kilikuwa ni kipengele muhimu sana kuwepo ndani ya Katiba mpya ijayo hasa kwa wakati huu ambao taifa limejawa na wanasiasa wasiokuwa waadilifu. Kipengele cha maadili kilikuwa kinawabana wanasiasa wote waliokuwa na matatizo ya kimaadili huko nyuma wasiweze kupata nafasi za uongozi za ngazi yoyote ile ndani ya nchi.Kwa mfano,Kuna baadhi ya wanasiasa walikumbwa na kashfa mbalimbali za ufisadi nchini kama vile EPA,KAGODA,MEREMETA,RADA,nk.Ha wa wote chini ya kipengele cha maadili walikuwa wameshapoteza sifa za kugombea nafasi yoyote ya ile uongozi hapa Tanzania.Lakini kwasababu Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimekuwa si Chama kinachopigania maslahi ya nchi tena bali ni ngazi inayotumiwa watu flani wenye tamaa ya madaraka na utajiri wa haraka kupanda kwenda kuvuna utajiri huo kwa manufaa yao binafsi kimeamua kukichomoa kipengele hicho kisiwemo kwenye Katiba mpya ijayo.Watu hawa wenye nguvu ya kifedha na ushawishi wa kisiasa ambao wamekiteka nyara Chama Cha Mapinduzi wameshaanza kampeni ya kukiondoa kifungu hiki cha maadili kwani kwao kinaonekana kuwa kizingiti kikubwa katika harakati zao kulihujumu hili taifa.
2) Uwazi-Kama kilivyokuwa kipengele cha maadili,Uwazi nao ni kipengele muhimu sana kinachofaa kuwemo ndani ya Katiba mpya ijayo (Hata hivyo nacho kimeng'olewa na WanaCCM) kwasababu kitaziba mianya ya Mikataba ya ajabu ajabu inayosainiwa na viongozi wa nchi ambayo huishia kuliingizia taifa hasara.Chini ya kipengele cha uwazi,Mikataba mingi ambayo serikali inasaini ingepaswa kupelekwa Bungeni kwa mijadala ya kina zaidi,Hii ingesaidia kudhibiti madudu yanayofanywa na serikali wakati wanaingia mikataba na Mataifa mengine au Makampuni ya kigeni.Uwazi usingeishia tu kwenye kuweka mikataba mbalimbali inayoingiwa na serikali hadharani bali ungejielekeza hadi kwa Waandishi wa habari ambao chini ya kifungu hiki wangeweza kupekuwa habari za ndani kabisa za viongozi na kuzianika hadharani ili umma wa Watanzania ufahamu kinachoendelea ndani ya nchi yao.
Chini ya utaratibu wa sasa waandishi wa habari wakiripoti habari za kichunguzi kwenye vyombo vya habari wanafunguliwa mashtaka sambamba na kuitwa wachochezi na watawala,Na hata baadhi ya vyombo vya habari kufungiwa kama ilivyokuwa kwa magazeti ya M.w.a.n.a.h.a.l.i.s.i na Mtanzania.Waandishi na Maripota wengi wanaofanya habari za kichunguzi wangeweza kulindwa na uwepo wa kipengele hiki.Si hivyo tu,Chini ya kipengele hiki vyombo vya habari vingekuwa na haki ya kikatiba ya kupata taarifa kutoka serikalini na kwenye matawi yake,Kwa kuwepo kwa kipengele hiki inamaama kwamba serikali ingekuwa inafanya shughuli zake katika mazingira ya uwazi zaidi sawa sawa na familia inayoishi kwenye nyumba ya vioo tupu ambapo watu wa nje wanaona kila kitu kinachoendelea ndani ya nyumba.
Kwasababu serikali ya CCM inachukia uwazi imewaagiza makada wake kwenye Bunge maalum la Katiba wakiondoe kipengele cha uwazi,Hii inamaanisha CCM kwa makusudi wameamua kulirudisha taifa kwenye zama za USIRI ambazo zimeligharimu taifa kiuchumi,kiusalama na kijamii. Ili taifa la Tanzania liweze kuwa kule kila mmoja wetu anatamani liwe kimaendeleo ni lazima CCM waondoke madarakani 2015,Hakuna njia.Ili CCM wang'oke madarakani ni lazima Vyama vya Upinzani viungane.