brand udom
Member
- Dec 19, 2014
- 40
- 14
Ingawa dhamira yangu inaniambia Lowasa sio msafi. Kwa nini Lowasa ni fisadi? Kelele za Chadema ndizo zilizofanya Lowasa atambulike kama fisadi rejea List of shame ambamo Kikwete na Mkapa wamo. Ila kelele za baadhi ya wanaccm wanaompinga Lowasa ndizo zilizoaminisha umma kuwa Lowasa ndiye fisadi peke yake nchini.
Mashabiki na vikundi mbalimbali vya CCM vilivyokuwa vikimuunga mkono Lowasa kabla na baada ya kumchukua fomu ya urais kupitia ccm, viliwaaminisha watu kuwa Lowasa si fisadi .
Leo hii Lowasa amehamia Chadema. Hatuwasikii tena waliokuwa wakimtuhumu kuwa ni fisadi. Kadhalika wale wa CCM waliokuwa wakimuunga mkono na kumpa sifa kedekede, leo hii nao eti wanampinga na kumwita fisadi.
Huu ni ugeugeu wa wanasiasa, wao wanasema siasa ni mchezo mchafu, mchafue mwenzio ili wew uwe safi.
Ila mimi binafsi naamini Lowasa ni fisadi anayetakiwa kuwa gerezani, kama alisingiziwa mimi sijui, Kama aliacha ufisadi mimi sijui. Lakini nitampa kura yangu maana naamini yupo kwenye mikono salama.
Kwa nini ni Lowasa?
1.Yeye ni fisadi na watu wengi wameamini kuwa ni fisadi, hivyo naamini Lowasa hawezi kwenda Ikulu ili kuthibitisha ufisadi wake, bali kuwathibitishia wabaya wake kuwa yeye ni tumaini jipya la nchi hii.
2.Lowasa anautendaji uliotukuka, kabla ya kuwa waziri mkuu na kuhusishwa na ufisadi wa Richmond hakuna mahali pengine popote alipoonekana kuwa ni fisadi, bali ulionekana utendaji wake uliotukuka kwa uchache alisimamia vizuri wizara ya mifugo kwa kujenga marambo mengi karibu nchi nzima (kwa jamii ya wafugaji), alisimamia vizuri na kuwezesha marekebisho ya sheria ya matumizi ya maji ya ziwa Victoria ambayo sasa hivi yanatumika hadi Shinyanga, alisimamia ujenz wa shule za kata kwa mafanikio na pia alitekeleza na kuisimamia ujenz wa chuo cha UDOM nk.
3.Wengi wanaompinga Lowasa ni wale walioko/waliokuwa kwenye mtiririko wa uongozi wa nchi hii, ambao kwa namna moja au nyingine wanaogopwa kugawanyika na vyombo vyote vya sheria, Ulinzi na usalama na hata takukuru (untouchables) mfano marais wastaafu. Mimi naamini kwa kuwa Lowasa hatokuwa na maslahi na watu hao akiingia Ikulu anaweza kuwafungulia kesi na kisha kuwafirisi Mali wale wote watakaobainika walitumia vibaya ofisi za umma kipindi cha uongozi wao.
NB: Kesho nitaeleza kwa nini UKAWA ni chaguo sahihi na ni mikono salama kwa mustakabali wa Taifa hili.
Mashabiki na vikundi mbalimbali vya CCM vilivyokuwa vikimuunga mkono Lowasa kabla na baada ya kumchukua fomu ya urais kupitia ccm, viliwaaminisha watu kuwa Lowasa si fisadi .
Leo hii Lowasa amehamia Chadema. Hatuwasikii tena waliokuwa wakimtuhumu kuwa ni fisadi. Kadhalika wale wa CCM waliokuwa wakimuunga mkono na kumpa sifa kedekede, leo hii nao eti wanampinga na kumwita fisadi.
Huu ni ugeugeu wa wanasiasa, wao wanasema siasa ni mchezo mchafu, mchafue mwenzio ili wew uwe safi.
Ila mimi binafsi naamini Lowasa ni fisadi anayetakiwa kuwa gerezani, kama alisingiziwa mimi sijui, Kama aliacha ufisadi mimi sijui. Lakini nitampa kura yangu maana naamini yupo kwenye mikono salama.
Kwa nini ni Lowasa?
1.Yeye ni fisadi na watu wengi wameamini kuwa ni fisadi, hivyo naamini Lowasa hawezi kwenda Ikulu ili kuthibitisha ufisadi wake, bali kuwathibitishia wabaya wake kuwa yeye ni tumaini jipya la nchi hii.
2.Lowasa anautendaji uliotukuka, kabla ya kuwa waziri mkuu na kuhusishwa na ufisadi wa Richmond hakuna mahali pengine popote alipoonekana kuwa ni fisadi, bali ulionekana utendaji wake uliotukuka kwa uchache alisimamia vizuri wizara ya mifugo kwa kujenga marambo mengi karibu nchi nzima (kwa jamii ya wafugaji), alisimamia vizuri na kuwezesha marekebisho ya sheria ya matumizi ya maji ya ziwa Victoria ambayo sasa hivi yanatumika hadi Shinyanga, alisimamia ujenz wa shule za kata kwa mafanikio na pia alitekeleza na kuisimamia ujenz wa chuo cha UDOM nk.
3.Wengi wanaompinga Lowasa ni wale walioko/waliokuwa kwenye mtiririko wa uongozi wa nchi hii, ambao kwa namna moja au nyingine wanaogopwa kugawanyika na vyombo vyote vya sheria, Ulinzi na usalama na hata takukuru (untouchables) mfano marais wastaafu. Mimi naamini kwa kuwa Lowasa hatokuwa na maslahi na watu hao akiingia Ikulu anaweza kuwafungulia kesi na kisha kuwafirisi Mali wale wote watakaobainika walitumia vibaya ofisi za umma kipindi cha uongozi wao.
NB: Kesho nitaeleza kwa nini UKAWA ni chaguo sahihi na ni mikono salama kwa mustakabali wa Taifa hili.