Kwenye maisha ya binadamu wakati mwingine mtu hulazimika au huamua kuingia kwenye mahusiano na mtu mwingine kwa mara moja tu. Mahusiano haya ambayo hayana lengo la kuishia kuwa wanandoa hufanywa kwa kificho au kwa bayana kufuatana na hali (Status) aliyonayo mtu.
Lakini kinachokera kwenye mahusiano haya ni mzigo wote wa kuyastawisha kubebwa na mwanaume. Kama ni kwenda "Guest" basi mlipaji ni mwanaume, kama ni makulaji na manywaji (Manywewa) shuluba itamkuta mwanaume, na mambo kadha wa kadha na zaidi ya hapo mwisho wa siku ni mwanamke atakayeondoka na hela za Mwanaume. Kwa nini??
Hivi ni mwanaume pekee ndiye anayefaidika na raha inayopatikana, yeye mwanamke hasikii chochote au ndiyo kusema "mwana mwenye kilanga" haliliwi?