Kwa mwanamke dhambi iliingia ulimwenguni na kwake ikaondolewa; kwa CCM Nchi ikafanywa maskini

SANCTUS ANACLETUS

JF-Expert Member
Mar 5, 2016
3,337
4,665
Leo Rais Magufuli anatarajia kutueleza jinsi CCM na Serikali yake walivyofanikiwa kushirikiana na wezi na majambazi wa kigeni kutuibia rasilimali za nchi yetu.Anatarajia kutuambia tumeibiwa kwa kiasi gani toka 1998.

Maandiko Matakatifu yanatuhabarisha kuwa dhambi iliingia ulimwenguni kwa niia ya mwanamke na kwa njia ya mwanamke yule yule dhambi ikaondolewa.Ni Bikra Maria aliyeokoa jahazi kwa kumzaa Yesu Kristu.

Tanzania kwa kupitia lichama la CCM na Serikali yake kwa miaka takribani 30 tumefanywa maskini wa kutupwa.Tumefanywa "mabuzi" npaka basi!

Tafakari ninayoileta ni je:kupitia CCM hii hii na Serikali yake, Magufuli atafanikiwa completely kutuondosha kutoka katika "dhambi" waliotuingiza CCM? Dhambi ya "kupoozeshwa" kiuchumi.

Ninamkubali "Yesu Magufuli" lakini je ataweza kuimaliza kazi hii kikamilifu?

Yesu yule wa ukweli alihitimisha kazi kwa kumpandia shetani hadi kuzimu na kushugjhulika naye huko.Je,kwa report ya leo Raisi Magufuli ataweza kushuka kuzimu na wale wote "mashetani" waliosaidiana na wezi na maharamia wa uchumi wetu ili akawazamishe huko maisha yao yote?Ataweza kulifanya neno litimie la kwamba kwa CCM na Serikali yake nchi yetu ilifukarishwa lakini kwa Magufuli tokea CCM hiyo hiyo na Serikali yake nchi itakombokewa toka kwenye dhambi ya "ubuzi" wa rasilmali zetu?

Karibuni kwa mjadala.
 
Back
Top Bottom