Paul Alex
JF-Expert Member
- Jul 14, 2012
- 4,240
- 9,527
Tofauti na ile alama ya dole gumba ambayo kimsingi haina maana, alama ya vidole viwili inayotumiwa na Chadema na wadau wengine wengi katika harakati mbalimbali duniani, ina maana kubwa mbili kulingana na ilivyotumika.
July 10,2017 katika mahakama ya hakimu mkazi kisutu au Kwa kujua au kutojua, Halima Mdee alifikisha ujumbe wa aina mbili kwa kutumia alama ya vidole viwili almaarufu kama V- for victory!
Kwanza kabisa Halima alinyanyua mkono wa kulia akaonyesha alama ya vidole viwili huku kiganja cha mkono huo kikiwa kimemuangalia yeye (the inner palm of the hand facing the signer).
Alama hii ikitumika hivi inamaanisha dhihaka,kukashifu au kutusi (an insult).
Mara ya pili, ndani ya sekunde kadhaa, Halima alinyanyua mkono wa kushoto akionyesha tena alama ya vidole viwili huku kiganja cha mkono huo kikiwa kimeielekea hadhira (the inner palm of the hand facing outward).Alama ya vidole viwili ikitumika hivi inamaanisha ushindi, umoja na upendo!
Ningepata nafasi ya kuonana na Halima moja kwa moja ningemuuliza kinagaubaga juu ya ujumbe aliokuwa anafikisha.
Ila pia najua kuwa Halima ni member wa JF na si vibaya akitutoa tongotongo juu ya nini hasa na nani hasa!!!
July 10,2017 katika mahakama ya hakimu mkazi kisutu au Kwa kujua au kutojua, Halima Mdee alifikisha ujumbe wa aina mbili kwa kutumia alama ya vidole viwili almaarufu kama V- for victory!
Kwanza kabisa Halima alinyanyua mkono wa kulia akaonyesha alama ya vidole viwili huku kiganja cha mkono huo kikiwa kimemuangalia yeye (the inner palm of the hand facing the signer).
Alama hii ikitumika hivi inamaanisha dhihaka,kukashifu au kutusi (an insult).
Mara ya pili, ndani ya sekunde kadhaa, Halima alinyanyua mkono wa kushoto akionyesha tena alama ya vidole viwili huku kiganja cha mkono huo kikiwa kimeielekea hadhira (the inner palm of the hand facing outward).Alama ya vidole viwili ikitumika hivi inamaanisha ushindi, umoja na upendo!
Ningepata nafasi ya kuonana na Halima moja kwa moja ningemuuliza kinagaubaga juu ya ujumbe aliokuwa anafikisha.
Ila pia najua kuwa Halima ni member wa JF na si vibaya akitutoa tongotongo juu ya nini hasa na nani hasa!!!