Kwa kashfa hizi za kuhusishwa na biashara ya mihadarati, Freeman Mbowe jiuzulu Uenyekiti CHADEMA

Kada wa CHADEMA

JF-Expert Member
Feb 27, 2016
289
615
Usisubiri mpaka ugongewe mlango wa kukuambia toka. Jipime mwenyewe na uondoke kabla hujafukuzwa kwa mawe. Najua wapo watakaokutetea kwa kusema hizo ni tuhuma tu. ila niwaambie kitu, kutuhumiwa ni kubaya zaidi kuliko kukutwa ukitenda.

Kwa mtu mwenye akilo timamu, hawezi kuendelea kubeba dhamana ya kuongoza chama huku akiwa na tuhuma lukuki na nyingi zikithibitika kuwa za kweli. Ilianza tuhuma ya kupanga jengo la NHC na kuishi bila ya kulipa pango na hivyo kudaiwa zaidi ya bilioni 13. Ilianza kama tetesi ila Mahakama ikapigilia msumari wa mwisho. Hatimaye vifaa vyote pale Bilicanaz vikatolewa nje kwa aibu.

Zikaja kashfa za kufanya biashara kupitia Hotel bila ya kulipa kodi. Hadi hivi sasa Mwenyekiti wangu Mbowe anadaiwa kiasi kikubwa cha kodi. Awali ilionekana ni uzushi. Ila kadri siku zinavyoenda ukweli unajulikana na Mbowe amekumbwa na aibu tele.

Kashfa hiyo haijapoa linaibuka kasheshe jingine la kutuhumiwa kuharibu vyanzo vya maji huko wilqyq ya Hai na hivyo kusababisha ukame. Kashfa hizi ni visible. Kila mtu anaona na ameridhia. Mwenyekiti wangu ni mharibifu wa mazingira.

Sasa limeibuka hili la kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya. Wapo wapuuzi humu wanamtetea eti kwamba anaonewa kwa maslahi ya kisiasa. Upuuzi wa hali ya juu. Wale waliokuwa wanatembelea pale Bilicanaz Club watakubaliana nami kuwa kilikuwa ni kijiwe muhimu cha mihadarati. Mbowe alikuwa anajua na ndio ilikuwa inampatia kipato kikubwa. Wasanii wengi wameharibiwa na Mbowe kupitia Bilicanaz Club.

Hizi ni kashfa kubwa sana. Ifike wakati Mbowe uone aibu. Si vema kwa Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni kuwa na rundo la kashfa namna hii. Huaminiki tena katika jamii. Watu wanakuangalia kwa wasiwasi na kijicho upande. Wanaokuambia kuwa unahujumiwa kisiasa hawakutakii mema.

Jiuzulu baba kabla jina lako halijachafuka sana. Kujiuzulu si ujinga. Ni namna ya kutunza heshima na hakika utakumbukwa kwa mchango wako ndani ya chama chetu. Ila ukiendelea kung'ang'ania basi uwe tayari pia kupokea na matokeo yake. Yawe Hasi ama Chanya.
 
Nitashangaa sana MBOWE akigombea nafasi ya M/KITI wa chama tena......hii ni sambamba na WAJUMBE watakao mpigia kura MBOWE kurudi kwenye hii nafasi nao itabidi TUWASHANGAE....

Maana jamaa ana tuhuma LUKUKI SANA kupita hata hao wanaoitwa MAFISADI..........

Hizi tuhuma tu ambazo hajawai hata siku moja kuomba kuwa CLEARED zinatosha kabsa kumweka pembeni
 
Mwenyekiti na katibu mkuu ccm wao wanatuhumiwa kwa madawa na ujangili nawao wajiuzulu.
Huwezi kuhalalisha uozo kwa kuangalia upande wa pili. Chama chetu kinajinasibu ni cha kidemokrasia. Demokrasia gani hii ya kutuhumiwa kila aina ya uozo? Mbowe amejiondokea uhalali wa kuwa kiongozi katika chama chetu. Aondoke atuachie chama. Tutaficha wapi sura zetu kwa aibu hii ya mwenyekiti wetu?
 
Dhambi ya kusitisha Operesheni UKUTA itawaandama!. Madhila yote haya yanayowakuta ni kwa sababu Wenye nguvu wamesmell uoga na ukunguru wa kufa mtu kwa wanaojiita Makamanda yaani Mwenyekiti na kamati kuu yake!!

Sasa Chickens are coming home to roost! , Watapigika sana mpaka watakaposema enough is enough, je guts hizo wanazo?
 
Nitashangaa sana MBOWE akigombea nafasi ya M/KITI wa chama tena......hii ni sambamba na WAJUMBE watakao mpigia kura MBOWE kurudi kwenye hii nafasi nao itabidi TUWASHANGAE....

Maana jamaa ana tuhuma LUKUKI SANA kupita hata hao wanaoitwa MAFISADI..........

Hizi tuhuma tu ambazo hajawai hata siku moja kuomba kuwa CLEARED zinatosha kabsa kumweka pembeni
Mbowe akihombea tena na kushinda inabidi wanachama wote wa CHADEMA tupimwe akili
 
Mbowe akihombea tena na kushinda inabidi wanachama wote wa CHADEMA tupimwe akili
Si kugombea na KUSHINDA hapa ajenda kuu iwe ni sura mpya zipambane na sura mpya YA CCM.....MAANA HAPA KINACHOIGHARIMU CHADEMA NA UPINZANI NI KUKOSEKANA FIKRA MPYA KUPAMBANA NA FIKRA MPYA........
Ndio maana kila jambo watakalo lianzisha kupambana na SURA MPYA (CCM)..wao wanaishia kupigwa vibaya......
 
Pilipili usoila inakuwashia nini? Uliona sehemu yiyote anaowaongoza wamelalamika? Nadhani hivi vituko vyote ni ili ajiuzuru kwa hili utasubiri sana
Maadili ni jambo la msingi sana katika uongozi wa siasa. Mbowe kwa kashfa hizi amekosa maadili
 
Si kugombea na KUSHINDA hapa ajenda kuu iwe ni sura mpya zipambane na sura mpya YA CCM.....MAANA HAPA KINACHOIGHARIMU CHADEMA NA UPINZANI NI FIKRA MPYA KUPAMBANA NA FIKRA MPYA........
Ungejishughulisha na CCM ya CDM Tuache Wenyewe
 
Back
Top Bottom