Mkonowatembo
JF-Expert Member
- Sep 25, 2016
- 1,096
- 994
Inaonekana nyumbani kwako unawalaumu watoto kwa maamuzi yako mabovu.Naunga mkono hoja, ila tusimlaumu Maza, sio yeye, yeye anakoseshwa tuu.
Phttps://www.jamiiforums.com/threads/rais-samia-sio-malaika-ni-binadamu-anaweza-kukosea-tusimlaumu-kumshutumu-na-kumponda-kwa-makosa-ya-kukoseshwa-tumvumilie-tumpe-muda.1883239/
P
Lipo ni kundi la wahafidhina wanamuingiza maza chaka, Maza akiisha jaa kwenye 18 yao, 2025 watamtosa!.Nakubaliana na wewe P lkn kuna tatizo mahala. Haiwezekani kufanya teuzi kwa majaribio(sumu haionjwi).
kuna kundi fulani linalompotosha kwa manufaa yao.
Idd Amini alipokuwa anapanda ndege kukimbilia Libya,Mama anafanya kazi nzuri sana, na iliyotukuka.
wanainchi wanafurahia matunda ya matokeo ya mipango yake madhubuti sana, katika kuyafikia malengo ya serikali kwa wanainchi, lakini pia kufikia ndoto na matarajio ya wanainchi kwa serikali yao sikivu 🐒
Ndio ukweli wenyewe. Mobutu alikuwa akifanya hivyo hivyo.
Unavunja msingi wa civil service unaotegemea merit na utendaji. Unabomoa confidence ya watumishi hata wakiwa bora na makini sana. Kila mmoja wao anaishi na hofu ya kutoswa nje ya ajira wakati wowote. Wote wanajua maslahi yao yako mkononi mwako na utendaji wao si lolote wala chochote. Unawaaminisha wananchi kuwa unafanya hivyo kwa maslahi ya taifa.
Nilishangaa sana JPM alipoanza kufanya hivyo. Hasa pale alipovunja management za serikali za mitaa na kuteua vijana wasio na experience wengi toka UVCCM kuwa wakurugenzi wa halmashauri. Nikakumbuka mambo ya Mobutu na washauri wake.
Nimuda wake na Katiba inamruhusu kufanya hivyo, na washauri wake wamekubaliana, anaona inamsaidia kwenye uongozi wake, mwacheni apambanie muda wake kuongoza nchi si jambo dogo. Si dhani kama ni dhamira yake kufanya mabadiliko kila mara, changamoto inayoonekana hapa ni aina ya watu wanaomzunguka ni tofauti na matarajio yake.
Hakuna, cha sijui nani alifanya nini, wap na tai...Idd Amini alipokuwa anapanda ndege kukimbilia Libya,
Alitoa vitisho ambavyo wanajeshi wetu wangesikia wote wangekimbiana.
Nakuelewa unachokimaanisha, unaamua kufa na tai shingoni.
Sasa kwanini asitafute historia ya hao Wahafidhina kabla ya kufanya teuzi??? Mimi ningemshauri aachane na Uchawa kwani ndiyo unaochangia haya yote.Lipo ni kundi la wahafidhina wanamuingiza maza chaka, Maza akiisha jaa kwenye 18 yao, 2025 watamtosa!.
P
Umempaka mafuta mazuri kwa mgongo wa chupa!katika utamaduni wa kujitathimini, kujisahihisha na kuziba mipasuko na kudhibiti nyufa, kurekebisha kasoro na dosari za kiutendaji kwenye chama na serikali.
Chama Cha Mapinduzi chini ya kiongozi madhubuti, shupavu na mahiri sana wa waTanzania, Comrade Dr.Samia Suluhu Hassani, kimeendelea kuimarika na kuaminika zaidi kwa wanainchi, na zaidi sana ccm imeendelea kupendwa sana na kuvutia mamilioni ya wanainchi wapinzani, kuungana na DR.SSH katika kuwaongoza waTanzania, na kuwaletea wanainchi maendeleo ya kiuchumi kijamii na kisiasa kwa usawa na haki, bila kijali rangi ya mtu, dini ya mtu au mrengo wa kisiasa wa mtu.
viva comrade DR.SSH viva...
Kidumu Chama Tawala na Serikali ya Chama Cha Mapinduzi....
Hakuna, cha sijui nani alifanya nini, wap na tai...
Kazi lazima ifanyike...
ukweli usemwe bila mbambamba, Comrade Dr SSH ni mahiri na ni madhubut mno katika uongozi wa nchi. hayupo na hakuna wa kumtisha wala kumuyumbisha kwa namna yoyote ile.
waTanzania kwa umoja na kwa maelfu na mamilioni yao, wanamuunga mkono, wanampenda, wanamfurahia nae bila hiana anawapa tabasamu na anawafurahisha kwenye maji,elimu,afya, kilimo, biashara n.k
na uteuzi huu unalenga kuwafurahisha wanainchi zaidi
hakuna chupa yoyote hapa wala mgongo wake 🐒Umempaka mafuta mazuri kwa mgongo wa chupa!
hakuna chupa yoyote hapa wala mgongo wake
na huu ni mwanzo na haya anayofanya hivi sasa ni kwa uchache tu, japo mengi ni bayana na yanaonekana mchana kweupe
bila kumuonea mtu haya wala aibu, tutawaeleza waTanzania kinagaubaga mambo muhimu ambayo CCM chini ya Dr.SSH wanafanya kwa maslahi mapana ya waTanzania
ili hatimae wale wa porojo na stori za sijui nini, nao wakataliwe hadharini kwenye sanduku la kura, Lakini kidemokrasia
Kama jpm mliimwita mshamba huyu tumwiteje sasa maan serikali tu ameshindwa kuunda kwa miaka 3 kipi anakiweza kwa sasaToka Rais Samia ameingia madarakani amekuwa na mwendo wa panga pangua nyingi kutoka kwenye Chama hadi kwenye serikali yake, Panga pangua zake amekua akizifanya kwa mantiki ya kufanya maboresho na utendaji kazi lakini hakuna kinacho badilika.
Panga pangua zake nyingine hata masaa 24 hazichukui na sio tu mwaka, hii inaleta tafsiri ya kuwa hana imani na anao wateua, au hashauriwi vizuri au hana misimamo.
Kwenye Chama, Kashabadilisha makatibu wenezi 3, Makatibu wakuu wawili, Na ukiangalia baadhi yake ni zinalalamikiwa au zinatoka kwa aibu na maadili mabovu, na bado anao watengua baadae au hapo hapo anaenda kuwapa nafasi zingine tena kwenye utumishi wa umma, hii inatafsiri gani? Kwenye uongozi wake hakuna uwajibikaji?!? Hawachukuliwi hatua.
Nfani ya Chama Mwenyekiti ataenda kupoteza mvuto na ushawishi, na panga pangua hizi zinaenda kuharibu Chama na kukigawa na kukifanya kionekane cha kawaida zaidi mbele ya macho ya wanachama na wananchi.
Panga pangua Serikalini na vyombo vya ulinzi (Tiss) na mabosi wa mashirika, ambao humo humo mtu anashindwa hapa anapelekwa huku, mara ana shushwa hapa mara ana pandishwa hapa.
Maamuzi ya kuchukua hatua kwa mama ni kubadilishia watu vitengo na sio kuwa wajibisha kwa makosa au maovu wanayofanya, nafasi za teuzi zimekua hazina hadhi tena, zinapoteza mvuto na hii itaenda mpaka juu kwa anae teua ambae ni yeye.
Sitali kuamini washauri wake ndio wanamshauri hivi, Au tuseme wanamshauri kwani yeye hana utashi wa kujiamulia, kwa level yake ya uraisi haoni kama vitu haviendi, hao teuzi zake zina shida, hana njia mbadala au hatua au maamuzi mengine katika kuikuza nchi hii.
Tunaenda kwenye uchaguzi, Chama chake kina poteza ushawishi kwasababu ya yeye anapoteza ushawishi na mvuto kwa wananchi na chama chake.
Hii inaenda kuharibu nchi, Amiri Jeshi mkuu hana misimamo hana maamuzi yaliosimama.. hii ni hatari kwa nchi.
kama ambavyo Rais asivyobabaika na wakisoaji wake na wale wanamuhujumu kwa makundi...Unavyo ongea ni unanikumbusha kitabu kimoja cha Lelo Mmasi.. cha Mimi na Rais namna wapambe walivyokua wanamsifia Rais Costa wa Stanza… unajua kusifia ila unasifia kwenye hamna… unasema ukweli wa uongo.
Nakubaliana na wewe sanaa kwenye hili...hawa inabidi watolewe kwa mtu.....Ccm ilipoteza mvuto toka uchaguzi wa 2010, nguvu ya Dola ndio imebaki mbeleko pekee ya wao kutangazwa washindi kwa shuruti. Kwahiyo si kweli kuwa ccm ipoteza mvuto kutokana na hizi teuzi za rais, Bali ilishapoteza mvuto muda mrefu.
Katika mchezo huu wanaotoswa kabisa wapo lakini wachache sana. Lengo kuu la teua, tengua, hamisha ni kuwaaminisha wananchi kuwa Rais anafanya kazi kudhibiti watendaji wake.Sasa kaka, kweli unaona chini ya Uongozi wake kuna anae ogopa!? Huoni wanaotoswa baada ya miezi wana rudi tena, mbaya wanaotoswa ni kwa kashfa lakini wanarudi tena mfano Chongola.
Sidhani kama Mobutu ni mfano mzuri wa mfumo huu, hili linalofanyika liko mbali kabisa na unayo sema.. sioni vikifanana.. maana hao wanaobadilishwa badilishwa hamna kitu wanafanya wanapo toka.. Mfano Mhede au huyo Kindambwa, wamesha kaa nafasi ngapi!?