Kwa hili! Dr. Mwakyembe umejiaibisha

Faru John II

Senior Member
Dec 27, 2016
134
135
Dr. Harrison Mwakyembe ametoa majibu alipoulizwa amefikia wapi kuhusu kuifanyia kazi ripoti ya Uchunguzi uliofanywa juu ya kinachoelezwa kuwa ni Uvamizi wa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam katika kituo cha habari cha Clouds Media Group (CMG).

Alipokuwa akitoa majibu Daktari huyu mwenye PhD ya sheria kama kawaida yake hakusahau kujinadi kuwa yeye ni gwiji na mkongwe ktk taaluma ya sheria ambapo hawezi kushughulika na Ripoti iliyokiuka misingi asili ya utoaji haki (RULES OF NATURAL JUSTICE). Mh. Waziri akaendelea kueleza kuwa ukitazama tu kamati ya Uchunguzi iliundwa na watu wenye interests(maslahi) na uchunguzi yaani Wanahabari pia msingi mwingine uliokiukwa kwa mujibu wake ni haki ya kusikilizwa ambapo alisema kamati yenyewe ilikiri kwa maneno yake kuwa haikuweza kumpata Mh. Mkuu wa mkoa.

KWANINI NIMEANDIKA MAKALA HII?

Jibu ni jepesi tu, Jibu lenyewe ni kuwa Rules of Natural Justice zina exceptions(ukomo). Ukomo wenyewe ni katika maeneo yafuatayo

(i)Haizingatiwi panapokuwa na haraka ya kuwepo uamuzi (emergency cases) mfano penye hati hati ya kupotea kwa amani na utulivu endapo maamuzi yatacheleweshwa.

(ii) Pale ambapo sheria haikutaja kuzingatiwa kwa misingi hiyo.

(iii) Pale ambapo kuzingatiwa kwa misingi hiyo kutahatarisha maslahi ya Umma.

(iv) Pale ambapo hatua za haraka zinahitajika

(v) Pale ambapo imeshindikana kusikilizwa kwa mtuhumiwa.

(vi) Pale ambapo mgogoro unahusiana na mambo ya kiutawala/Uongozi (purely administrative matters).

(vii) Pale ambapo hakuna haki ya mtu itapindishwa.

(viii) Pale ambapo kuzingatiwa ama kutozingatiwa kwa misingi hiyo hakutoleta tofauti yoyote katika maamuzi.

(ix) Pale ambapo mtoaji wa uamuzi hana sifa ya kuwa na kasoro.

Sheria inayoeleza sifa za watu wanaounda kamati ya Uchunguzi haijataja kuwa mwanahabari yoyote hatakiwi kuwa sehemu ya kamati ya uchunguzi, pia exceptions (vizuizi) za misingi ya asili ya haki zimeweka wazi kuwa panapotokea vikwazo vya wazi vya kutopata maelezo ya mtuhumiwa misingi hii haitozingatiwa, kamati ilieleza wazi namna Mh. Makonda alivyokuwa akikwepa kutoa maelezo kwa kuwakimbia wajumbe waliotumwa kumuhoji.

Ukitazama kwa makini maneno ya Dr. Mwakyembe kuamua kukwepa wajibu wake kisa Rules of Natural Justice utagundua kuwa kauli yake haina mashiko na haitegemewi kutoka kwa mtu mwenye elimu hafifu ya sheria. Mh. Waziri atambue kuwa kamati ile ilitazama misingi hiyo na ikatazama pia vizuizi vya kuzingatiwa kwa misingi hiyo kama nilivyotaja hapo juu ambapo ni wazi kabisa utaona issue ya Makonda ni ya kiutawala kabisa (purely administrative matter) ambapo swali lililotakiwa kujibiwa na kamati ni Je Makonda alitumia madaraka yake vibaya? Jibu la kamati likawa ni Ndio likatoa na evidence (ushahidi).

Kwa heshima na taadhima tunamwomba Mh. Mwakyembe kutuomba ladhi kwa kutufanya wajinga wa sheria.
 
Dr Mwakyembe tafadhali mwambie DAUDI ALBERT BASHITE alete vyeti tumkague please! Yaani tuwe na mkuu wa mkoa tena wa Dar es salaam aliyefeli kidato cha nne yaani ZERO! aibu aibu aibu
 
Hata kwenye kesi nyingine Zach madai kuna wakati Mahakama inatoa "ex parte " decisions/ judgement (maamuzi ya upande mmoja ) endapo mtuhumiwa atapewa taarifa za shitaka alafu akakataa kutumia fursa yake ya kujitetea.

Bashite alipewa nafasi ya kusikilizwa lakini hakuitumia. Kwanini kamati ionekane ina mapungufu kwa kutoa ex parte decision?

My take: Mwakyembe kama mbobezi wa sheria anajua fika kamati hakuna ilipokosea bali ameamua kuwa mchumia tumbo (anatetea kibarua).
 
Mwakyembe bwana... Sijuhi ni ile sumu imetua kwenye medula oblangata au ndo hulka yake tu...
Hivi alitaka DAB apigwe pingu ili ahojiwe na kamati ya NAPE??
Mbona walimtafuta na kilichowatokea ni cha kufedhehesha mno..!!
Natangaza rasmi kudharau PHD ya Mwakyembe..!!
No wonder alikusudia kuifuta TLS..
The man is retarding at a suprisingly quicker speed.!!
 
Nimeona aibu hata kuambatanisha picha yake
Tatizo sio Mwakyembe atoe maamuzi ama kupitia mapendekezo ya kamati ya Nape. Ndugu Faru John unataka kuniaminisha kuwa wewe umesahau kilichofukuzisha kazi nape? mbona watanzania tunapenda kuzunguka ama kuwatafutia watu lawama? mbona jibu rahisi tu, ni kwamba issue ya makondo ina baraka za Jpm, sasa wewe unataka kuniambia kuwa Mwakyembe ana mamlaka kuliko baba jescca?. Mwakyenbe kweli in jipu sikatai lakini kwa hili la Makonda mnamuonea bure. Makonda ni unteachable kwa magufuli.
 
Hata kwenye kesi nyingine Zach madai kuna wakati Mahakama inatoa "ex parte " decisions/ judgement (maamuzi ya upande mmoja ) endapo mtuhumiwa atapewa taarifa za shitaka alafu akakataa kutumia fursa yake ya kujitetea.

Bashite alipewa nafasi ya kusikilizwa lakini hakuitumia. Kwanini kamati ionekane ina mapungufu kwa kutoa ex parte decision?

My take: Mwakyembe kama mbobezi wa sheria anajua fika kamati hakuna ilipokosea bali ameamua kuwa mchumia tumbo (anatetea kibarua).
Mwakyembe kajitoa fahamu kwa kumwogopa Daud kisa atamchongea atumbuliwe jipu
 
Mwakyembe bwana... Sijuhi ni ile sumu imetua kwenye medula oblangata au ndo hulka yake tu...
Hivi alitaka DAB apigwe pingu ili ahojiwe na kamati ya NAPE??
Mbona walimtafuta na kilichowatokea ni cha kufedhehesha mno..!!
Natangaza rasmi kudharau PHD ya Mwakyembe..!!
No wonder alikusudia kuifuta TLS..
The man is retarding at a suprisingly quicker speed.!!
Mwakyembe ni msomi feki na PhD yake ni feki pia hamna kitu pale sasa anaishi kwa sauti ya makonda bila makonda yy hawezi kitu
 
Mwakyembe kama mbobezi wa sheria anajua fika kamati hakuna ilipokosea bali ameamua kuwa mchumia tumbo (anatetea kibarua

Huyu bwana ile sumu waliomuwekea bado inamtafuna kidogo kidogo na ndio maana ana toa taarifa zisizokuwa na maana yeyote!! He is not cabinet material because he has no intergrity!!
 
PhD ya Mwakyembe ichunguzwe, - hata kama ni ya halali lakini ni wazi kuwa AKILI zake zishachoka (namshauri akapumzike tu kuliko kuendelea kuidharaulisha taaluma ya sheria)

Namuomba asijaribu kum'beba huyo Bashite ambaye tayari yuko kwenye mapigo ya kuuacha wokovu na pia ana laana ya kumpiga mh mzee jaji Warioba.
 
Mwakyembe bwana... Sijuhi ni ile sumu imetua kwenye medula oblangata au ndo hulka yake tu...
Hivi alitaka DAB apigwe pingu ili ahojiwe na kamati ya NAPE??
Mbona walimtafuta na kilichowatokea ni cha kufedhehesha mno..!!
Natangaza rasmi kudharau PHD ya Mwakyembe..!!
No wonder alikusudia kuifuta TLS..
The man is retarding at a suprisingly quicker speed.!!
Naungana nawe. PhD ya Bw. Mwakiyembe ifutwe.
 
Dr. Harrison Mwakyembe ametoa majibu alipoulizwa amefikia wapi kuhusu kuifanyia kazi ripoti ya Uchunguzi uliofanywa juu ya kinachoelezwa kuwa ni Uvamizi wa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam katika kituo cha habari cha Clouds Media Group (CMG).

Alipokuwa akitoa majibu Daktari huyu mwenye PhD ya sheria kama kawaida yake hakusahau kujinadi kuwa yeye ni gwiji na mkongwe ktk taaluma ya sheria ambapo hawezi kushughulika na Ripoti iliyokiuka misingi asili ya utoaji haki (RULES OF NATURAL JUSTICE). Mh. Waziri akaendelea kueleza kuwa ukitazama tu kamati ya Uchunguzi iliundwa na watu wenye interests(maslahi) na uchunguzi yaani Wanahabari pia msingi mwingine uliokiukwa kwa mujibu wake ni haki ya kusikilizwa ambapo alisema kamati yenyewe ilikiri kwa maneno yake kuwa haikuweza kumpata Mh. Mkuu wa mkoa.

KWANINI NIMEANDIKA MAKALA HII?

Jibu ni jepesi tu, Jibu lenyewe ni kuwa Rules of Natural Justice zina exceptions(ukomo). Ukomo wenyewe ni katika maeneo yafuatayo

(i)Haizingatiwi panapokuwa na haraka ya kuwepo uamuzi (emergency cases) mfano penye hati hati ya kupotea kwa amani na utulivu endapo maamuzi yatacheleweshwa.

(ii) Pale ambapo sheria haikutaja kuzingatiwa kwa misingi hiyo.

(iii) Pale ambapo kuzingatiwa kwa misingi hiyo kutahatarisha maslahi ya Umma.

(iv) Pale ambapo hatua za haraka zinahitajika

(v) Pale ambapo imeshindikana kusikilizwa kwa mtuhumiwa.

(vi) Pale ambapo mgogoro unahusiana na mambo ya kiutawala/Uongozi (purely administrative matters).

(vii) Pale ambapo hakuna haki ya mtu itapindishwa.

(viii) Pale ambapo kuzingatiwa ama kutozingatiwa kwa misingi hiyo hakutoleta tofauti yoyote katika maamuzi.

(ix) Pale ambapo mtoaji wa uamuzi hana sifa ya kuwa na kasoro.

Sheria inayoeleza sifa za watu wanaounda kamati ya Uchunguzi haijataja kuwa mwanahabari yoyote hatakiwi kuwa sehemu ya kamati ya uchunguzi, pia exceptions (vizuizi) za misingi ya asili ya haki zimeweka wazi kuwa panapotokea vikwazo vya wazi vya kutopata maelezo ya mtuhumiwa misingi hii haitozingatiwa, kamati ilieleza wazi namna Mh. Makonda alivyokuwa akikwepa kutoa maelezo kwa kuwakimbia wajumbe waliotumwa kumuhoji.

Ukitazama kwa makini maneno ya Dr. Mwakyembe kuamua kukwepa wajibu wake kisa Rules of Natural Justice utagundua kuwa kauli yake haina mashiko na haitegemewi kutoka kwa mtu mwenye elimu hafifu ya sheria. Mh. Waziri atambue kuwa kamati ile ilitazama misingi hiyo na ikatazama pia vizuizi vya kuzingatiwa kwa misingi hiyo kama nilivyotaja hapo juu ambapo ni wazi kabisa utaona issue ya Makonda ni ya kiutawala kabisa (purely administrative matter) ambapo swali lililotakiwa kujibiwa na kamati ni Je Makonda alitumia madaraka yake vibaya? Jibu la kamati likawa ni Ndio likatoa na evidence (ushahidi).

Kwa heshima na taadhima tunamwomba Mh. Mwakyembe kutuomba ladhi kwa kutufanya wajinga wa sheria.
Hivyo kwani imethibitishwa pasi shaka Kama ameshapona ugonjwa wake?
 
Amjibu na huyu sisi hatukumwelewa jana
Hata mambo yanayohusu sheria hatuyajui
 

Attachments

  • f23db26e3569c1420717e851f24fdb7d.mp4
    2.4 MB · Views: 19
Tena
 

Attachments

  • f23db26e3569c1420717e851f24fdb7d.mp4
    2.4 MB · Views: 17
Huo ndio ukweli MTU wangu,hongera kwa kuchambua na kusema wazi juu ya aibu hii.Nadhani hawa watawala,niwaite hivyo wanafikiri watanzania wa miaka kumi nyuma ndo hawa wa Leo pasi kujua kuwa kifikra wameamka,na no aibu na DOA kubwa kulifumbia macho tukio kama like.Swali ni je! Kapuku kama Mimi nifanye tukio kama la RC,si wangeninyang'anyia kama Mpira wa kona?.Ifike mahala waambiwe ukweli,na kama washauri wake hawawezi Fanya hivyo,bora kujiengua kuliko kuendelea na udhalimu huu,kwa watanzania.
 
binafsi katika mambo ya sheria mwakyembe ni mtu wa kujitapa tu lakini hana jipya. ni huyuhuyu aliyesema lissu akichaguliwa TLS ataifuta.pia ni huyuhuyu mwakyembe hakumuhoji lowasa wakati wa sakata la richmond.....
 
Watu huweka taaluma zao mfukoni ili tu mkono uende kinywani ma-daktari na ma-profesa wengi watanzania wako hivyo njaa tu ndio inawasumbua.
 
Back
Top Bottom