Christina samamba
Member
- Jul 22, 2022
- 20
- 38
Tatizo hili la kuzuia maiti ya mtu mara baada ya ndugu kushindwa kulipa gharama za hospitalini linawatesa watu wengi sana hususani wenye kipato cha chini, kwasababu si kwamba watu hufanya makusudi kutelekeza maiti za wapendwa wao hospitali bali ni hali ngumu ya maisha na deni kuwa kubwa zaidi ya kipato chao.
Mfano kutoka kwenye chombo cha habari gazeti la Mwananchi la Alhamisi tarehe 23-9-2021 walichapisha kwamba hospitali ya Muhimbili ilishikilia mwili wa marehemu anayeitwa Zena Musa mwenye miaka 30, baada ya ndugu zake kushindwa kulipa deni la shilingi milioni 1.6.
Ingawaje serikali inajitahidi sana kukataza kitendo hiki mfano kutoka kwenye chazo cha habari "Jamii forums" Mheshimiwa Naibu Waziri Wa Afya Dkt Ndugulile naye apiga marufu kitendo hicho cha kuzuia maiti ambapo alisema "ni marufuku hospitali kushikilia maiti kwa kile kinachotajwa hadi pale gharama za matibabu yake zitakapolipwa". Hii ni baada ya mkasa kumpata Bwana Shabani Mtepa mkazi wa Tandahimba Kwa ajili ya huduma ya kujifungua. Alipofika hospitalini hapo alifanyiwa upasuaji kisha akajifungua mtoto mwenye afya njema lakini mama mwenyewe hakuwa na maendeleo mazuri kwani alivuja uchafu mwingi sana Kwa muda wa siku nne mfululizo. Alipofika siku ya tano alirejeshwa theatre kwaajili ya upasuaji mwingine hali iliendelea kuwa tete, kwani tatizo lile lile la kuvuja uchafu liliendelea na madaktari waliamua kumfanyia upasuaji kwa mara tatu hata hivyo hakukuwa na mafanikio yoyote kwahiyo wakaamua kumpa rufaa ya kwenda hospitali ya mkoa wa mtwara (Ligula) kwa matibabu zaidi. Madaktari wa Ligula pia walishindwa kutatua tatizo lililomkaribia mama huyo hivyo waliamua kumsafirisha hadi hospitalini ya Taifa yaani Muhimbili aliendelea kupata tiba hapo muhimbili Kwa siku nne na ilipofika siku ya tano yaani usiku wa kuamkia tarehe 7 Julai 2020 huyu mama aliaga dunia huku akimwachia mumewe mtoto mchanga wa wiki mbili.
Baada ya hapo ndipo kijana shabani Mtepa alipoanza kufuatilia maiti ya mkewe ili akahifadhi kwenye makazi ya milele lakini akakutana na kigingi cha kutakiwa alipe kiasi milioni 1,470,800 huku akiwa na hali ngumu ya maisha.
Hata kaburi lililoandaliwa kumpumzisha mwili wa marehemu lilifukiwa baada ya kuzuiliwa Kwa mwili huo.
Kutoka kwenye chazo cha habari gazeti la mwananchi la alhamisi tarehe 23 septamba 2021 Pia Kwa kuonyesha tatizo ni kubwa Muheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan alimwagiza Dkt Gwajima kuangalia namna gani utaratibu utaandaliwa kuondoa kadhia ya maiti kuzuiliwa hospitalini.
"Tunaambiwa mtu asiende kuzikwa mpaka deni limelipwa, lakini si deni la serikali nataka muweke mpango mnzuri wa kulipa deni bila kuzuia maiti" alisema Rais Samia. Moja kati ya mpango mzuri ni kutoa gharama za matibabu wakati matibabu yakiendelea. Siyo siku mgonjwa amefariki dunia unadaiwa shilingi milioni 3 huku, anafanya mpango namna gani? Taratibu za mazishi? Hii sio sawa, naomba muweke mpangilio mzuri wa kuyashughulikia haya", aliagiza Rais samia.
Licha ya malalamiko yote haya tatizo bado lipo na watu wanazidi kuteseka. Inahitajika serikali kuangalia suala hili kwa jicho pana zaidi kwa kusaidia kuandaa mikakati minzuri na sheria nzuri zitakazoziongoza taasisi hizi za afya katika kutoa huduma iliyo bora. Pia kunahitajika elimu ya kutosha Kwa wananchi ili waweze kufahamu utaratibu uliowekwa na taasisi za afya baada ya watu kushindwa kulipia gharama za hospitali ili waweze kuchukua maiti za wapendwa wao.
Wananchi wengi wamekuwa wakilalamika juu ya tatizo hili kwasababu pia ya kukosa uelewa, kuwa inawezekana kwenda ustawi wa jamii na kupatiwa msaada ambao utawawezesha kupata msahama wa gharama za matibabu utakao pelekea kuwaachiwa kwa maiti za wapendwa wao, ila wananchi wengi hawalitambui hili.
Kwahakika kunahitajika uboreshwaji wa sera za afya na sheria za afya kwa upana zaidi ili kuweza kuwagusa watu wenye hali ngumu. Maana kwa Tanzania watu wenye kutumia bima ya afya wanafika 10%, hii ni baada ya kushindwa kulipa ada za uanachama. Inabidi serikali iangalie namna ya kuwasaidia watu wa hali hii kuweza kupata huduma ya bima kwa kipato chao.
Mfano kutoka kwenye chombo cha habari gazeti la Mwananchi la Alhamisi tarehe 23-9-2021 walichapisha kwamba hospitali ya Muhimbili ilishikilia mwili wa marehemu anayeitwa Zena Musa mwenye miaka 30, baada ya ndugu zake kushindwa kulipa deni la shilingi milioni 1.6.
Ingawaje serikali inajitahidi sana kukataza kitendo hiki mfano kutoka kwenye chazo cha habari "Jamii forums" Mheshimiwa Naibu Waziri Wa Afya Dkt Ndugulile naye apiga marufu kitendo hicho cha kuzuia maiti ambapo alisema "ni marufuku hospitali kushikilia maiti kwa kile kinachotajwa hadi pale gharama za matibabu yake zitakapolipwa". Hii ni baada ya mkasa kumpata Bwana Shabani Mtepa mkazi wa Tandahimba Kwa ajili ya huduma ya kujifungua. Alipofika hospitalini hapo alifanyiwa upasuaji kisha akajifungua mtoto mwenye afya njema lakini mama mwenyewe hakuwa na maendeleo mazuri kwani alivuja uchafu mwingi sana Kwa muda wa siku nne mfululizo. Alipofika siku ya tano alirejeshwa theatre kwaajili ya upasuaji mwingine hali iliendelea kuwa tete, kwani tatizo lile lile la kuvuja uchafu liliendelea na madaktari waliamua kumfanyia upasuaji kwa mara tatu hata hivyo hakukuwa na mafanikio yoyote kwahiyo wakaamua kumpa rufaa ya kwenda hospitali ya mkoa wa mtwara (Ligula) kwa matibabu zaidi. Madaktari wa Ligula pia walishindwa kutatua tatizo lililomkaribia mama huyo hivyo waliamua kumsafirisha hadi hospitalini ya Taifa yaani Muhimbili aliendelea kupata tiba hapo muhimbili Kwa siku nne na ilipofika siku ya tano yaani usiku wa kuamkia tarehe 7 Julai 2020 huyu mama aliaga dunia huku akimwachia mumewe mtoto mchanga wa wiki mbili.
Baada ya hapo ndipo kijana shabani Mtepa alipoanza kufuatilia maiti ya mkewe ili akahifadhi kwenye makazi ya milele lakini akakutana na kigingi cha kutakiwa alipe kiasi milioni 1,470,800 huku akiwa na hali ngumu ya maisha.
Hata kaburi lililoandaliwa kumpumzisha mwili wa marehemu lilifukiwa baada ya kuzuiliwa Kwa mwili huo.
Kutoka kwenye chazo cha habari gazeti la mwananchi la alhamisi tarehe 23 septamba 2021 Pia Kwa kuonyesha tatizo ni kubwa Muheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan alimwagiza Dkt Gwajima kuangalia namna gani utaratibu utaandaliwa kuondoa kadhia ya maiti kuzuiliwa hospitalini.
"Tunaambiwa mtu asiende kuzikwa mpaka deni limelipwa, lakini si deni la serikali nataka muweke mpango mnzuri wa kulipa deni bila kuzuia maiti" alisema Rais Samia. Moja kati ya mpango mzuri ni kutoa gharama za matibabu wakati matibabu yakiendelea. Siyo siku mgonjwa amefariki dunia unadaiwa shilingi milioni 3 huku, anafanya mpango namna gani? Taratibu za mazishi? Hii sio sawa, naomba muweke mpangilio mzuri wa kuyashughulikia haya", aliagiza Rais samia.
Licha ya malalamiko yote haya tatizo bado lipo na watu wanazidi kuteseka. Inahitajika serikali kuangalia suala hili kwa jicho pana zaidi kwa kusaidia kuandaa mikakati minzuri na sheria nzuri zitakazoziongoza taasisi hizi za afya katika kutoa huduma iliyo bora. Pia kunahitajika elimu ya kutosha Kwa wananchi ili waweze kufahamu utaratibu uliowekwa na taasisi za afya baada ya watu kushindwa kulipia gharama za hospitali ili waweze kuchukua maiti za wapendwa wao.
Wananchi wengi wamekuwa wakilalamika juu ya tatizo hili kwasababu pia ya kukosa uelewa, kuwa inawezekana kwenda ustawi wa jamii na kupatiwa msaada ambao utawawezesha kupata msahama wa gharama za matibabu utakao pelekea kuwaachiwa kwa maiti za wapendwa wao, ila wananchi wengi hawalitambui hili.
Kwahakika kunahitajika uboreshwaji wa sera za afya na sheria za afya kwa upana zaidi ili kuweza kuwagusa watu wenye hali ngumu. Maana kwa Tanzania watu wenye kutumia bima ya afya wanafika 10%, hii ni baada ya kushindwa kulipa ada za uanachama. Inabidi serikali iangalie namna ya kuwasaidia watu wa hali hii kuweza kupata huduma ya bima kwa kipato chao.