Kutoka viwanja vya Sinoni-Arusha: Mkutano wa Mgombea Urais wa CHADEMA, Edward Lowassa - Okt 8, 2015

Nanyaro Ephata

JF-Expert Member
Jan 22, 2011
1,221
1,788
Leo mkutano mkubwa wa hadhara katika viwanja vya shule ya Sekondari Sinoni, Mkutano huu utarushwa live na ITV.

Maandalizi ya mkutano yamekamilika na Lowassa anatarajiwa kupokelewa katika uwanja wa ndege wa Arusha na msafara wake kuelekea uwanjani.

Mkutano wa leo utaweka msimamo na mwelekeo wa Taifa kuhusu uchaguzi kwa hizi siku zilizobaki.Mwenyekiti wa chama Taifa na kamanda wa anga Mh Freeman Mbowe atatoa mwelekeo na msimamo wa chama kabla ya siku ya uchaguzi.

Mkutano utaanza saa nane kamili.Mapokezi ya Mh Rais saa tano pale Kisongo uwanja wa Ndege

Nipo uwanjani kukuletea yale yote yanayojiri pamoja na picha

Stay tuned!!!!!!

Updates

Wananchi wa Arusha na viunga vyake wakiendelea kumwagika viwanjani hapa Kwa hiyari yao wenyewe. hajalipiwa mtu hapa. Hakuna Lori wala basi lililoleta mtu.

Uwanja umeshatapika na mambo ndiyo bado hata hayajaanza. Hakika Lowassa ni Rais wa awamu ya Tano.


Endelea kufuatilia huu Uzi Kwa updates zaidi kwani mambo ndiyo kwaaaanza bado.

Lowasaaaaaaaaa...Mabadiliko!!

Usiondoke baki hapohapo.

Updates

Taarifa za hivi punde zina sema Rais mtarajiwa Edward Ngoyai Lowassa akiwa na Timu nzima ya UKAWA watakuwa viwanjani hapa kuanzia majira ya Saa10 Jioni.

Endelea kufuatilia huu Uzi Kwa Updates zaidi...

Updates


Mkutano ameshaanza. Mbatia anazungumza.

Anasema Arusha imepewa heshima ya kuhutubiwa na Mzee Kingunge Ngombale Mwiru.

Anasema Ccm wameuza hisa za TBI zenye thamani ya shilingi177Bil ili zisaidie kampeni zao

Wiki ijayo watauza tena 50% za NBC zenye dhamani ya 412bil

Jk katumia 4trilion kwa safari za nje fedha ambazo zingetosha kujenga vyuo vya ufundi 200 kwa thamani ya bil 20 kila kimoja

Ccm badala ya kufanya kampeni inabebwa na dola kwa kufanya haramu.

Kikwete amefanya ccm haramu kwa kutumia fedha za watanzania kwenye kampeni

Lowassa amesema kipaumbele chake cha kwanza hadi tatu ni elimu.

Elimu ya Lowassa itasaidia kwa kuanzisha vyuo vya ufundi ili ziweze kumsaidia.

Mkamate sana elimu usimwache aende zake maana ndiyo uzima wako. Maneno ya mithali

Tarehe 25/10 tuhakikishe rais wetu ni Lowassa.. Magufuli asipate kura hata moja

Mbowe:
Naomba nimlete kwenu mgeni wenu wa siku ya leo ambaye ana kadi namba 8 ya ccm. Anataka kuzungumza na watu wa Arusha

Watu wanashangilia babu babu babu babu babu

Tangu ccm imeanza kampeni imefanya vituko,kampeni zao zimetawaliwa na matusi,kimepoteza dira

Ccm haisemi sera tena bali kusema watu kwenye mikutano yao

Lazima mtu anayesemwa sana awe ni mtu mzito sana,ndio maana watu wazima wanamsema sana

Mimi ni mtu wa mabadiliko

Ninaamini kwa dhati ya moyo wangu kuwa mabadiliko Tanzania ni sasa

Wakati tunaanzisha TANU tulikuwa tunatafuta chombo cha kumkomboa Mtanganyika

ASP na TANU vimefanya jitihada kubwa kuboresha maisha ya watanzania,na kwa kuwa viliamini katika mabadiliko viliungana

Tunaendelea na mabadiliko hadi sasa,lakini katika awamu hii ya nne,kuna dalili kuwa baada ya ccm kukaa madarakani kwa nusu karne imeishiwa pumzi

Ccm ilirithi pumzi ya asp na Tanu ila sasa pumzi imekwisha

Mkapa alichukua kutoka kwa Mwinyi wakati uchumi ukikuwa kwa 4%

Kikwete karithi unaokuwa kwa 7asilimia,miaka 10 baadae na kwa taarifa za serikali yenyewe uchumi unakuwa chini ya 7%

Maana yake ni kwa miaka 10 hii tumeganda!

Ili kuondoa umasikini lazima uchumi ukue kwa 10%kitaalam
Kwa miaka kumi ccm uchumi umekuwa kwa single digit

Uchaguzi ni kura,sio maneno

Tarehe 25 kazi ni moja tu,unachukua kichinjio unaweka Lowasa

Naomba marafiki zangu wa ccm,wengine tangu wakati wa kupigania uhuru,wasibabaike,sijawaacha kwa sababu nawachukia,nimeondoka kwa sababu sikubaliani na uongozi unaovunja katiba ya chama,taratibu,na kanuni.

Uongozi unaodhalilisha wagombea Urais wa chama chao,na wanaendelea kana kwanba hakuna lililotokea

Anaaga wanachi kwa kumtia moyo.

Nawatakieni mafanikio katika harakati za kuleta mabadiliko

Uwanja unalipuka Kwa kushangilia. babu babu babu babu.

Sumaye
Watanzania wameamua kuwa sasa ni mwaka wa mabadiliko

Wameamua hivyo kwa kuwa ccm imeshindwa kuleta maisha bora

Watoto hawatibiwi bure

Ccm imeahidi vijana ajira,na kikwete aliahidi vijana kuwa tatizo la ajira litakuwa ajira,Je tatizo hilo limeisha?

Elimu imeharibiwa na ccm

Wananchi wanajibu kuwa hakuna haja ya kuchagua ccm tena

Rais lazima awe mwadilifu,awe mtumishi mwema,na awe kimbilio la watu

Kwenye mizani kuna rushwa kubwa,wizara ya magufuli imenunua bot ya miaka 30 kwa gharama ya boti mpya

Wizara ya ujenzi inaongoza kwa ufisadi,Je ni Magufuli ni mwadilifu?

Ameshindwa kupambana na ufisadi wizarani kwake ataweza kwa nchi?

Lazima rais awe msikivu,je Magufuli ni msikivu?

Kigamboni aliwaambia watu wapige mbizi Maana yake wafe.

Hatutaki Rais mbambe

Sumaye anamaliza Kwa kushangiliwa vilivyo.

Sasa Lowassa anataka kuzungumza na Watanzania.

Wimbo unapigwa anacheza

Lowassa

Namshukuru sana mzee Ngombale ndie aliyekuwa nguzo ya ccm,kuondoka kwake ni pigo kwa ccm

Nimekuja kuomba kura

Wananchi wanaitikia Kwa shangwe. Umepataaaaaaa. Uwanja mzima kelele na vifijo

Wananchi wanaimba Rais Rais Rais Rais Lowassa

Kwa huu umati ikulu nimefika

Kwanini nagombea urais

Nimechoshwa na umaskini

Naomba kura nyingi ili niweze kushinda.

Nimeomba kuwa rais kwasababu nimechoka na umaskini.

Nitaanza na elimu ili kuondoa hali ya umaskini. Vipaumbele vyangu vya kwanza elimu pili elimu tatu elimu. Ukimpa mtoto wako elimu umemsaidia kimaisha. Nimesema elimu kuanzia nursery hadi chuo kikuu bure.

Wanasema haiwezekani mimi nasema inawezekana kabisa tuna fedha nyingi sana nchi hii kuanzia gesi mpaka madini na utalii. Hakuna mwanafunzi kulipa mchango wa aina yoyote. Nitazingatia maslahi ya mwalimu ili awe na moyo na kazi yake.

Eneo la pili ni eneo la kilimo nitaiboresha na mkulima akitaka kuuza mazao yake popote auze. Tuwape wananchi uhuru wafurahie matunda ya nchi yao wakale raha.

Eneo la tatu ndugu zangu wa bodaboda, mama ntilie na machinga watakuwa rafiki wa serikali yangu. Naahidi nikiingia ikulu baada ya wiki moja atakayewasumbua nakula nao sahani moa. Nitaanzisha benki kwa ajili wa wamama kupata mikopo.

Nikichaguliwa kuwa rais kila wilaya kutakuwa na hospitali za rufaa zenye vifaa vya kisasa kuwasaidia wagonjwa.

Nimekusudia kuongoza Tanzania kwakuwa nia ninayo sababu ninayo na uwezo ninao. Serikali yangu itakuwa ya mchakamchaka

Lema

Kamanda Lema, Kiboko ya CCM Arusha anazungumza sasa.

Wananchi wanamshangilia Lema Lema Jembe Jembe.

Lema anazungumza

Mh rais hawa watu ni watu wangu wananipenda nami nawapenda sana. Nimekamatwa na kuteswa kwa ajili a watu hawa, nimeenda jela kwa ajili ya watu hawa, nimejenga hospitali bado tunawapigania watu wangu.

Nakuhakikishia tayari tuna kura laki mbili na sitini na tayari hao walikusainia wakati wa udhamini. Mh rais una kura nyingi sana.

Nakuomba uwasiliane na Lubuva umwambie mpango wa kuchelewesha vifaa ukome tunahitaji kura za haki.


Wakuu mkutano imeisha na watu wanaanza kuondoka viwanjani hapa.

Ni dhahiri shahiri CCM wana kazi nzito kuanzia ngazi ya Udiwani mpaka Urais ndani na nje ya Arusha.

WanaArusha wameionyesha Arusha na Tanzania kwamba Mabadiliko hayakwepeki na CCM lazima itoke.



Shukrani za dhati ziwafikie makamanda Kwa kuwezesha Updates za Leo.

chakii Mungi Molemo Emma sweetlady Filipo Crashwise na wengine wote walioshiriki.


Tukutane Oktoba 25.

==========================


Chanzo: Mtanzania
 
Last edited by a moderator:
Mwa mujibu wa Lema kupitia account yake ya FB amesema mkutano utakuwa live kupitia ITV.
 
Hii itasaidia kumsikia Kingunge anachotaka kuzungumza kwa dk40 kuhusu JK na CCM yetu kama alivyodai.Kumbuka Kingunge ni mwanachama wa muda mrefu sana ndani ya CCM pengine kuliko wengine waliobaki.Tunawaomba UKAWA wafanye hima mkutano uwe live

Mkutano utakuwa Live ITV
 
Vizuri Nanyaro.

Tuletee kila kinachojiri mkuu na diwani wa kata ya Levolosi hakikisha kifaa chako kina moto wa kutosha mkuu.
 
Pamoja sana kamanda nitajitahidi niskie hizo fimbo za kingunge teh teh pia picha ni muhimu zaidi
VIVA UKAWA!!!
 
Hii itasaidia kumsikia Kingunge anachotaka kuzungumza kwa dk40 kuhusu JK na CCM yetu kama alivyodai.Kumbuka Kingunge ni mwanachama wa muda mrefu sana ndani ya CCM pengine kuliko wengine waliobaki.Tunawaomba UKAWA wafanye hima mkutano uwe live

Uwe na power bank ya kuwezesha TV kuwaka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…