Kutoka Maktaba ya Mzee Kissinger: Picha ya Karne ya 20 ya Julius Kambarage Nyerere

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,921
30,266
KUTOKA MAKTABA YA MZEE KISSINGER: PICHA YA KARNE YA 20 YA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE

Jana tulipokwenda kumsalimia mwalimu wetu Mzee Kissinger nilimgusia kuhusu picha aliyonipa miaka mingi nyuma ya Mzee Mshume Kiyate akimvisha Julius Nyerere Rais wa Tanganyika kitambi mwezi February 1964.

Hii ilikuwa baada ya maaasi yaliyotokea tarehe 20 January Tanganyika Rifles (TR) walipoasisi na ikabidi Mwalimu akimbie kutoka Ikulu akajifiche mahali pasipojulikana.

Kwa kiasi cha siku tatu hakuna aliyejua Nyerere yuko wapi.
Nyerere alirudi Ikulu baada ya maasi kuzimwa na Jeshi la Wanamaji wa Kiingereza.

Mwalimu katika hotuba yake alisema kitendo kile kilikuwa fedheha kubwa kwa Tanganyika.
Lakini Mwalimu Nyerere alijificha wapi?

Peter Mwimbo aliyekuwa Mlinzi wa Rais katika kitabu cha maisha yake anasema walijificha Kigamboni na aneleza namna alivyomtorosha Mwalimu.

Nilipata kuzungumza na marehemu Mzee Kitwana Kondo ambae alikuwa Ikulu wakati ule.

Maelezo ya Mzee Kitwana Kondo kwangu mimi yanapishana na ya Peter Mwimbo.

Lakini mshtuko mkubwa wa kisa hiki cha maficho ya Julius Nyerere niliyapata kwa Bi. Mwajame Dossa Aziz mtoto wa Dossa Aziz aliyekuwa rafiki mkubwa wa Nyerere miaka hiyo.

Bi. Mwajame amenieleza kuwa baba yake alijenga handaki shambani kwake Ruvu kama tahadhari endapo Nyerere atalazimika kujificha kujiokoa.

Nyerere na Dossa mara kwa mara walikuwa wakienda kwenye shamba hili kwa mapumziko mafupi.

Siku ya maasi Dossa alipopata taarifa kuwa Nyerere baada ya maasi hajulikani alipo yeye haraka alikwenda Ruvu kukagua lile handaki lao.

Dossa kutwa nzima hakuweza kupatika hadi usiku alipokwenda kwenye nyumba yake ya Mtoni kwa Aziz Ali kwa mama yake kuwajulia hali.

Yeye alikuwa akiishi Ruvu na mkewe Bi. Nagla Stein chotara wa Kijerumani.

Hapo Mtoni mama yake alimbana Dossa kutaka kujua usalama wa Nyerere kwani alipita asubuhi kumuaga mama yake kuwa anakwenda kumtafuta Nyerere na wao walimsihi asiende mjini kwani jiji zima la Dar es Salaam lilijaa askari kila kona wakipekua watu na magari.

Dossa alikataa kusema lolote kuhusu Nyerere kama amemuona au la alichowahikikishia ni kuwa Nyerere yuko hai.

Mimi nilizungumza na Mzee Dossa nyumbani kwake Ruvu mbele ya Ally Sykes aliyenipeleka kwake.

Mzee Dossa aliniambia kuwa siku ya maasi alitoka kwenda kumtafuta Nyerere akiendesha Land Rover yake na ndani alikuwa na bunduki yake kanitajia kuwa ilikuwa ''Five Repeater," yaani bunduki hiyo ikipiga risasi tano mfululizo kwa mkupuo mmoja.

Bi. Mwajame anasema baba yake akistahika sana Dar es Salaam na askari wote waliomsimamisha njiani hawakupekua gari yake wakimtambua ni yeye wabafungua njia anapita.

Turudi kwa Prof. Kissinger.

Kissinger alinieleza kuwa baada ya Mwalimu kurejea madarakani TANU ilifanya mkutano mkubwa Viwanja Vya Jangwani.

Baraza la Wazee wa TANU lilikuwa lishavunjwa toka mwezi March 1963 na Mzee Mshume alikuwa Mjumbe.
Mzee Mshume alitoka nyumbani kwake na kitambi.

Alipokutana na Nyerere baada ya kumpa pole kwa yaliyomfika alikichukua kile kitambi akamvisha Nyerere kama kielelezo cha mapenzi yake kwake na mapenzi ya wananchi wenzake.

Picha hii ya Mzee Mshume Kiyate akimvisha Julius Nyerere kitambi haikupata kuoenakana popote baada ya kuchapwa katika gazeti mwaka wa 1964 ikawa kama vile haipo imepotea.

Siku Prof. Kissinger alipokamilisha darasa lake kwangu la historia ya maasi ya TR akaniambia, ''Mohamed picha ya Mzee Mshume na Nyerere ninayo Insha Allah nitakupa.''

Picha yenyewe ndiyo hiyo hapo chini.
Hiyo ndiyo picha ya Karne ya 20 kutoka Maktaba ya Mzee Kissinger.

Picha nyingine ni kaburi la Mzee Mshume Kiyate lililopo Kunduchi kwa hisani ya Alwi Mngazija.

Meya wa Dar es Salaam Kitwana Selemani Kondo alimpa Mzee Kiyate Mshume mtaa kwa kutambua mchango wake kwa TANU, Mwalimu Nyerere na familia yake wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.

Sasa inafikia miaka 40 wenye mamlaka wamekataa kuweka kibao chenye jina la Mshume Kiyate Mtaa wa Tandamti aliokuwa akiishi.

1686838199399.png
1686838273695.png


 
Nilivyoona heading nikajuwa ni Kissinger wa Marekani, kumbe kuna wamatumbi nao wakiitwa Kissinger?

Issue ya mtaa Mzee wangu watu wa karibu si mchange pesa kidogo hapo gerezani vibao viwili haizidi laki 3.

Zoezi la post code waliopewa mitaa wengi wameambiwa wagharamie wenyewe.

Haya majitu ya Ccm huwa hayajari mtu ambaye hayupo
 
KUTOKA MAKTABA YA MZEE KISSINGER: PICHA YA KARNE YA 20 YA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE

Jana tulipokwenda kumsalimia mwalimu wetu Mzee Kissinger nilimgusia kuhusu picha aliyonipa miaka mingi nyuma ya Mzee Mshume Kiyate akimvisha Julius Nyerere Rais wa Tanganyika kitambi mwezi February 1964.

Hii ilikuwa baada ya maaasi yaliyotokea tarehe 20 January Tanganyika Rifles (TR) walipoasisi na ikabidi Mwalimu akimbie kutoka Ikulu akajifiche mahali pasipojulikana.

Kwa kiasi cha siku tatu hakuna aliyejua Nyerere yuko wapi.
Nyerere alirudi Ikulu baada ya maasi kuzimwa na Jeshi la Wanamaji wa Kiingereza.

Mwalimu katika hotuba yake alisema kitendo kile kilikuwa fedheha kubwa kwa Tanganyika.
Lakini Mwalimu Nyerere alijificha wapi?

Peter Mwimbo aliyekuwa Mlinzi wa Rais katika kitabu cha maisha yake anasema walijificha Kigamboni na aneleza namna alivyomtorosha Mwalimu.

Nilipata kuzungumza na marehemu Mzee Kitwana Kondo ambae alikuwa Ikulu wakati ule.

Maelezo ya Mzee Kitwana Kondo kwangu mimi yanapishana na ya Peter Mwimbo.

Lakini mshtuko mkubwa wa kisa hiki cha maficho ya Julius Nyerere niliyapata kwa Bi. Mwajame Dossa Aziz mtoto wa Dossa Aziz aliyekuwa rafiki mkubwa wa Nyerere miaka hiyo.

Bi. Mwajame amenieleza kuwa baba yake alijenga handaki shambani kwake Ruvu kama tahadhari endapo Nyerere atalazimika kujificha kujiokoa.

Nyerere na Dossa mara kwa mara walikuwa wakienda kwenye shamba hili kwa mapumziko mafupi.

Siku ya maasi Dossa alipopata taarifa kuwa Nyerere baada ya maasi hajulikani alipo yeye haraka alikwenda Ruvu kukagua lile handaki lao.

Dossa kutwa nzima hakuweza kupatika hadi usiku alipokwenda kwenye nyumba yake ya Mtoni kwa Aziz Ali kwa mama yake kuwajulia hali.

Yeye alikuwa akiishi Ruvu na mkewe Bi. Nagla Stein chotara wa Kijerumani.

Hapo Mtoni mama yake alimbana Dossa kutaka kujua usalama wa Nyerere kwani alipita asubuhi kumuaga mama yake kuwa anakwenda kumtafuta Nyerere na wao walimsihi asiende mjini kwani jiji zima la Dar es Salaam lilijaa askari kila kona wakipekua watu na magari.

Dossa alikataa kusema lolote kuhusu Nyerere kama amemuona au la alichowahikikishia ni kuwa Nyerere yuko hai.

Mimi nilizungumza na Mzee Dossa nyumbani kwake Ruvu mbele ya Ally Sykes aliyenipeleka kwake.

Mzee Dossa aliniambia kuwa siku ya maasi alitoka kwenda kumtafuta Nyerere akiendesha Land Rover yake na ndani alikuwa na bunduki yake kanitajia kuwa ilikuwa ''Five Repeater," yaani bunduki hiyo ikipiga risasi tano mfululizo kwa mkupuo mmoja.

Bi. Mwajame anasema baba yake akistahika sana Dar es Salaam na askari wote waliomsimamisha njiani hawakupekua gari yake wakimtambua ni yeye wabafungua njia anapita.

Turudi kwa Prof. Kissinger.

Kissinger alinieleza kuwa baada ya Mwalimu kurejea madarakani TANU ilifanya mkutano mkubwa Viwanja Vya Jangwani.

Baraza la Wazee wa TANU lilikuwa lishavunjwa toka mwezi March 1963 na Mzee Mshume alikuwa Mjumbe.
Mzee Mshume alitoka nyumbani kwake na kitambi.

Alipokutana na Nyerere baada ya kumpa pole kwa yaliyomfika alikichukua kile kitambi akamvisha Nyerere kama kielelezo cha mapenzi yake kwake na mapenzi ya wananchi wenzake.

Picha hii ya Mzee Mshume Kiyate akimvisha Julius Nyerere kitambi haikupata kuoenakana popote baada ya kuchapwa katika gazeti mwaka wa 1964 ikawa kama vile haipo imepotea.

Siku Prof. Kissinger alipokamilisha darasa lake kwangu la historia ya maasi ya TR akaniambia, ''Mohamed picha ya Mzee Mshume na Nyerere ninayo Insha Allah nitakupa.''

Picha yenyewe ndiyo hiyo hapo chini.
Hiyo ndiyo picha ya Karne ya 20 kutoka Maktaba ya Mzee Kissinger.

Picha nyingine ni kaburi la Mzee Mshume Kiyate lililopo Kunduchi kwa hisani ya Alwi Mngazija.

Meya wa Dar es Salaam Kitwana Selemani Kondo alimpa Mzee Kiyate Mshume mtaa kwa kutambua mchango wake kwa TANU, Mwalimu Nyerere na familia yake wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.

Sasa inafikia miaka 40 wenye mamlaka wamekataa kuweka kibao chenye jina la Mshume Kiyate Mtaa wa Tandamti aliokuwa akiishi.

Inna li Llahi wa inna Ilayhi rajiun.
 
Nilivyoona heading nikajuwa ni Kissinger wa Marekani, kumbe kuna wamatumbi nao wakiitwa Kissinger?

Issue ya mtaa Mzee wangu watu wa karibu si mchange pesa kidogo hapo gerezani vibao viwili haizidi laki 3.

Zoezi la post code waliopewa mitaa wengi wameambiwa wagharamie wenyewe.

Haya majitu ya Ccm huwa hayajari mtu ambaye hayupo
Dr.
Si suala la fedha.
 
KUTOKA MAKTABA YA MZEE KISSINGER: PICHA YA KARNE YA 20 YA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE

Jana tulipokwenda kumsalimia mwalimu wetu Mzee Kissinger nilimgusia kuhusu picha aliyonipa miaka mingi nyuma ya Mzee Mshume Kiyate akimvisha Julius Nyerere Rais wa Tanganyika kitambi mwezi February 1964.

Hii ilikuwa baada ya maaasi yaliyotokea tarehe 20 January Tanganyika Rifles (TR) walipoasisi na ikabidi Mwalimu akimbie kutoka Ikulu akajifiche mahali pasipojulikana.

Kwa kiasi cha siku tatu hakuna aliyejua Nyerere yuko wapi.
Nyerere alirudi Ikulu baada ya maasi kuzimwa na Jeshi la Wanamaji wa Kiingereza.

Mwalimu katika hotuba yake alisema kitendo kile kilikuwa fedheha kubwa kwa Tanganyika.
Lakini Mwalimu Nyerere alijificha wapi?

Peter Mwimbo aliyekuwa Mlinzi wa Rais katika kitabu cha maisha yake anasema walijificha Kigamboni na aneleza namna alivyomtorosha Mwalimu.

Nilipata kuzungumza na marehemu Mzee Kitwana Kondo ambae alikuwa Ikulu wakati ule.

Maelezo ya Mzee Kitwana Kondo kwangu mimi yanapishana na ya Peter Mwimbo.

Lakini mshtuko mkubwa wa kisa hiki cha maficho ya Julius Nyerere niliyapata kwa Bi. Mwajame Dossa Aziz mtoto wa Dossa Aziz aliyekuwa rafiki mkubwa wa Nyerere miaka hiyo.

Bi. Mwajame amenieleza kuwa baba yake alijenga handaki shambani kwake Ruvu kama tahadhari endapo Nyerere atalazimika kujificha kujiokoa.

Nyerere na Dossa mara kwa mara walikuwa wakienda kwenye shamba hili kwa mapumziko mafupi.

Siku ya maasi Dossa alipopata taarifa kuwa Nyerere baada ya maasi hajulikani alipo yeye haraka alikwenda Ruvu kukagua lile handaki lao.

Dossa kutwa nzima hakuweza kupatika hadi usiku alipokwenda kwenye nyumba yake ya Mtoni kwa Aziz Ali kwa mama yake kuwajulia hali.

Yeye alikuwa akiishi Ruvu na mkewe Bi. Nagla Stein chotara wa Kijerumani.

Hapo Mtoni mama yake alimbana Dossa kutaka kujua usalama wa Nyerere kwani alipita asubuhi kumuaga mama yake kuwa anakwenda kumtafuta Nyerere na wao walimsihi asiende mjini kwani jiji zima la Dar es Salaam lilijaa askari kila kona wakipekua watu na magari.

Dossa alikataa kusema lolote kuhusu Nyerere kama amemuona au la alichowahikikishia ni kuwa Nyerere yuko hai.

Mimi nilizungumza na Mzee Dossa nyumbani kwake Ruvu mbele ya Ally Sykes aliyenipeleka kwake.

Mzee Dossa aliniambia kuwa siku ya maasi alitoka kwenda kumtafuta Nyerere akiendesha Land Rover yake na ndani alikuwa na bunduki yake kanitajia kuwa ilikuwa ''Five Repeater," yaani bunduki hiyo ikipiga risasi tano mfululizo kwa mkupuo mmoja.

Bi. Mwajame anasema baba yake akistahika sana Dar es Salaam na askari wote waliomsimamisha njiani hawakupekua gari yake wakimtambua ni yeye wabafungua njia anapita.

Turudi kwa Prof. Kissinger.

Kissinger alinieleza kuwa baada ya Mwalimu kurejea madarakani TANU ilifanya mkutano mkubwa Viwanja Vya Jangwani.

Baraza la Wazee wa TANU lilikuwa lishavunjwa toka mwezi March 1963 na Mzee Mshume alikuwa Mjumbe.
Mzee Mshume alitoka nyumbani kwake na kitambi.

Alipokutana na Nyerere baada ya kumpa pole kwa yaliyomfika alikichukua kile kitambi akamvisha Nyerere kama kielelezo cha mapenzi yake kwake na mapenzi ya wananchi wenzake.

Picha hii ya Mzee Mshume Kiyate akimvisha Julius Nyerere kitambi haikupata kuoenakana popote baada ya kuchapwa katika gazeti mwaka wa 1964 ikawa kama vile haipo imepotea.

Siku Prof. Kissinger alipokamilisha darasa lake kwangu la historia ya maasi ya TR akaniambia, ''Mohamed picha ya Mzee Mshume na Nyerere ninayo Insha Allah nitakupa.''

Picha yenyewe ndiyo hiyo hapo chini.
Hiyo ndiyo picha ya Karne ya 20 kutoka Maktaba ya Mzee Kissinger.

Picha nyingine ni kaburi la Mzee Mshume Kiyate lililopo Kunduchi kwa hisani ya Alwi Mngazija.

Meya wa Dar es Salaam Kitwana Selemani Kondo alimpa Mzee Kiyate Mshume mtaa kwa kutambua mchango wake kwa TANU, Mwalimu Nyerere na familia yake wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.

Sasa inafikia miaka 40 wenye mamlaka wamekataa kuweka kibao chenye jina la Mshume Kiyate Mtaa wa Tandamti aliokuwa akiishi.

Mkuu hongera kwa nyota ktk historia ya Tanzania
 
Kwa hiyo Nyerere hakutorokea Kigamboni! Naam
Plato...
Mimi sina hakika na hilo.

Kama nilivyokueleza Kitwana Kondo maelezo yake yanapishana na maelezo ya Peter Mbwimbo.
Hii ya kuwapo handaki shambani kwa Dossa Aziz lililojengwa endapo Nyerere atahitaji kujificha kanieleza Bi. Mwajame Aziz mtoto wa Dossa.

Tena mazungumzo yetu alikuwa ananieleza matatizo aliyonayo kuhusu mashamba ya baba yake Ruvu jinsi watu walivyovamia na jinsi yeye anavyohangaika kudai mashamba hayo.

Akaniambia katika shamba moja kuna handaki ambalo baba yake alijenga kwa ajili ya kujificha Nyerere ikiwa itabidi.

Nilipata mshuko mkubwa nikaanza kumuuliza maswali ndipo akanieleza nini kilitokea siku ya maasi na kuwa baba yake aliamua kwenda kumtafuta Nyerere alipoambiwa kuwa hajulikani alipo askari waasi hawakumkuta Ikulu.

Hii ni habari ndefu kidogo.
 
Kama nilivyokueleza Kitwana Kondo maelezo yake yanapishana na maelezo ya Peter Mbwimbo.
Si kila mtu aliyekuwa Ikulu angeweza kujua Nyerere alijificha wapi. Bwimbo akiwa mlinzi yeye ndiye anajua walijificha wapi.


Hizi habari za kina Kitwana haziwezi kuaminiwa. Kitwana alikuwa nani Ikulu hadi ajue rais kajificha wapi?!
 
Si kila mtu aliyekuwa Ikulu angeweza kujua Nyerere alijificha wapi. Bwimbo akiwa mlinzi yeye ndiye anajua walijificha wapi.


Hizi habari za kina Kitwana haziwezi kuaminiwa. Kitwana alikuwa nani Ikulu hadi ajue rais kajificha wapi?!
Gag...
Mimi nimeeleza yale niyajuayo kama alivyonieleza Kitwana Kondo.

Kitwana Kondo alikuwa msaidizi wa Oscar Kambona.

Taarifa yake nimeieleza katika kitabu ch Abdul Sykes.
 
Nilivyoona heading nikajuwa ni Kissinger wa Marekani, kumbe kuna wamatumbi nao wakiitwa Kissinger?

Issue ya mtaa Mzee wangu watu wa karibu si mchange pesa kidogo hapo gerezani vibao viwili haizidi laki 3.

Zoezi la post code waliopewa mitaa wengi wameambiwa wagharamie wenyewe.

Haya majitu ya Ccm huwa hayajari mtu ambaye hayupo
Point
 
Back
Top Bottom