Kutoka kwa JR Farhan, Mchambuzi wa Soka la Kibongo wa Clouds Media

DullyJr

JF-Expert Member
Apr 10, 2011
13,979
11,816
Yanga wana kikosi kizuri sana cha kushindana ligi ya ndani hilo halina ubishi, lipo dhahiri shahiri wala hatupingi ila kuna tatizo mahali kwenye michuano ya kimataifa.

Mfano Simba walienda kambi nchini Misri wakapata mechi nzuri za kiushindani sana, ambazo 60% ya timu hizo ndio unakutana nazo kwenye michuano hii.

Walipotoka kule wakaenda Sudan baada ya ligi kusimama, wakapata mechi na Al Hilal na Asante Kotoko ya Ghana zote hizo ni michezo migumu, wamegusa Afrika Magharibi na Afrika ya Kati.

Wachezaji wameingiza kitu mpaka hapo! Hata ligi iliposimama Simba wakaenda Zanzibar wakapata tena mechi nzuri mpaka na Kipanga ambaye ametoa sare na Club Africain ya Tunisia , vuta picha hapo.

Kifupi ni kuwa kila wakipata upenyo wao wanatoka kwenda kupata mechi za kipimo sahihi kuendana na kasi za kimataifa, wachezaji hawapati presha kwakuwa wamezoea mechi kubwa.

Tofauti na Yanga, timu hii kusafiri nje ya nchi ilikuwa Morocco ambapo wakarejea mapema, mara ya mwisho walienda Nigeria wakafungwa na Rivers hawajawahi kusafiri tena, they need competitive games.

Kocha Mwinyi Zahera amesema kitu kikubwa sana kuwa wachezaji wao wana presha sana, hawapo sawa kwakuwa mechi nzito na za kiushindani kama hizi hawajakutana nazo kama timu, presha ipo juu.

Kama dhamira ni kufanya vyema kimataifa basi tukubali kuwa hizi mechi dhidi ya Mbuni na Friends Rangers pale AVIC TOWN haziwezi kutusaidia, mnapaswa kupata mechi kweli kweli ili kufanya vyema kimataifa.

Chochote ambacho Yanga watakifanya kimataifa kwangu ni bonus tu ila timu kama timu bado haijapata test sahihi ya kufanya makubwa kimataifa, sad truth.

"Simba and Yanga are equal but not the same", wanafanana ila hawapo sawa.

VISIT MOROGORO
 
Maoni ya mdau wa 1.......


Maneno ni mengi sana ungeandika tu kwa ufupi kuwa UTOPOLO YANANUNUA MECHI KWA KUHONGA MAREFA, TIMU, WACHEZAJI PINZANI NA WANAOJIITA WACHAMBUZI KTK LIGI ZA NDANI TU,HUKO NJE "HAWAJIWEZI" in voice of Jemedar Said
 
Mdau wa pili.....Kipindi mnyama karudi kutoka misri akafungwa na gongowazi kwenye ngao ya hisani ikaonekana gongowazi wapo vizuri wakasifiwa kwamba bora wao wameweka kambi kigamboni na timu ipo vizuri kuliko alienda misri, ghafla mmeanza kuhamisha goli bora alienda misri kuliko aliebaki kigamboni, unakuja kugundua wachambuzi wengi wanachambua mpira kwa kuwafurahisha watu flani sio utaalamu unasemaje mimi niwaombe muda mwingine mnyamaze hamta pungukiwa chochote mmekuwa kama machizi fresh zinakuja na kuondoka
 
Itoshe kusema MUWAPE NAFASI YA KUFANYA MAMBO YAO kama wana pigwa goli ni WAO na Mungu wao
 
Kwa ule waliocheza kwa mkapa juzi juzi?labda wabadilike ila wasipobadilika wanakwenda kufa.watu wanaangalia mmechezaje
Wachambuzi hua wanaenda na upepo hayo anayo yasema ikitokea Yanga akashinda huko Sudan utasikia wanavyo badili gia
 
Mafanikio hayaji kwa bahati mbaya.wenzenu wanahangaika na mechi za kirafiki za kimataifa nyie mmejifungia zenu kigamboni mnadhani mtakuwa sawa na wenzenu?
Angalia goli alilowafunga chama de agosto utaona kabisa huyu mchezaji ni wa level za kimataifa.ana uzoefu
 
Mafanikio hayaji kwa bahati mbaya.wenzenu wanahangaika na mechi za kirafiki za kimataifa nyie mmejifungia zenu kigamboni mnadhani mtakuwa sawa na wenzenu?
Angalia goli alilowafunga chama de agosto utaona kabisa huyu mchezaji ni wa level za kimataifa.ana uzoefu
Mwaka jana Simba ilienda Morocco ikatolewa round ya kwanza kwenda pre season nje sio sababu mpira wa Africa una vitu vingi ambavyo Yanga wana lack wajifunze tu hapo ila hizo mambo za pre season ni siasa huyo Farhan kipindi Yanga inashida alikua ana andika makala za kuipamba leo hio draw amegeuza maelezo
 
Mwaka jana Simba ilienda Morocco ikatolewa round ya kwanza kwenda pre season nje sio sababu mpira wa Africa una vitu vingi ambavyo Yanga wana lack wajifunze tu hapo ila hizo mambo za pre season ni siasa huyo Farhan kipindi Yanga inashida alikua ana andika makala za kuipamba leo hio draw amegeuza maelezo
Hauwezi kupambana kimataifa Kama haufanyi mazoezi ya kimataifa.changamoto mpya ni muhimu.wewe unacheza na mbuni unakwenda kupambana na kocha aliyebeba kombe la shirikisho afrika utamuweza?
 
Tatizo tunamaliza maneno as if yanga amesha disqualify tayariii.

Hata huyo simba mwenyewe last year alienda Pre season Morroco na mwishowe alishindwa kwenda makundi CAFCL.

Hizo hoja za kwenda Pre season sijui wapi na kucheza timu gani sijuii..hazina nguvu kiivo..

Timu nyingi za ulaya huwa zinaenda bara la Amerika au Asia kuweka kambi ya pre season na huwa zinacheza timu ambazo average kwao..

Swala la yanga ni swala la kawaida unless mtu uongee kimahaba ila kimpira mechi bado ipo open sana.
 
Wewe unacheza na mbuni fc, mbuni akiingia tu anaanza kukuogopa then unafurah eti umemfunga!!
Simba anaenda cheza na al hillal tena kwao, unafikiri mentality ya wachezaji itakuaje apo
 
Wachambuzi wengi ni janja janja. Ngoja hao yanga wapindue meza utawasikia:
" Yanga ni timu kubwa, yenye miaka mingi na uzoefu wa kutosha, walichokifanya ni kuangalia makosa na kuyasahihisha, unapokutana na timu kubwa yenye uzoefu kama hii tegemea lolote na leo tumeona walitoa droo nyumbani na sasa wameshinda ugenini."
 
Back
Top Bottom