Kurudi JWTZ

Kurudi JWTZ

GEBO.

Member
Joined
Mar 30, 2014
Posts
28
Reaction score
7
Naombeni ushari wana JF.

Mimi niliajiriwa 2004 na JWTZ kama askari baada ya kumaliza form four. Nilifanya mtihani wa form six nikiwa jeshini na kufaulu vizuri, Nikatamani sana kuendelea na elimu ya juu. Nilijitahidi kuomba ruhusa kikosini ilishindikana, nilifika makao kuomba msaada nikakuta msururu mkubwa wa maombi haujajibiwa kwa miaka kadhaa nyuma. Nikaamua kuomba chuo nikapata, Nikaomba mkopo nikapata asilimia mia, Ruhusa nikaikosa. Nikaamua kuacha Jeshi. Nilianza chuo 2009 nikamaliza 2012.

Natamani kurudi jeshini, nilifika Makao makuu nikawaona wanasheria wakaniambia ni vigumu mimi kushinda kesi labda kama nitakuwa na mtu mkubwa kunisaidia. Wana JF msinihukumu kwa makosa niliyoyafanya nisaidieni mawazo.

Karibuni
 
maji yakishamwagika hayazoleki maisha sio jeshini tu
 
haaaw c wewe tu hata mm n hivyo hvyo kaks vuta subira zikitoka zile za proffesional tutajaribu tena! tpdc walitoa je uliomba? coz kule n kutamu kuliko jwtz
 
watu tunatafuta nafasi za jeshi tangia 2010 tunakosa wewe unaacha!!!!huko sahau tena kurudi jipange kivingine maisha sio jeshi tu usikalili kuna fursa nyingi sana.usife moyo.
 
wewe huna uzalendo tafuta kwingine!!wakati wa tahadhari wewe utatuache tena uende kusoma!!
 
mhhhh usife moyo n pm tuchat vizuri fursa zipo japo itabidi uanzie chini kidogo ila on long tun itajipa tu c una jiwe?
 
Naombeni ushari wana JF. Mimi niliajiriwa 2004 na JWTZ kama askari baada ya kumaliza form four. Nilifanya mtihani wa form six nikiwa jeshini na kufaulu vizuri, Nikatamani sana kuendelea na elimu ya juu. Nilijitahidi kuomba ruhusa kikosini ilishindikana, nilifika makao kuomba msaada nikakuta msururu mkubwa wa maombi haujajibiwa kwa miaka kadhaa nyuma. Nikaamua kuomba chuo nikapata, Nikaomba mkopo nikapata asilimia mia, Ruhusa nikaikosa. Nikaamua kuacha Jeshi. Nilianza chuo 2009 nikamaliza 2012. Natamani kurudi jeshini, nilifika Makao makuu nikawaona wanasheria wakaniambia ni vigumu mimi kushinda kesi labda kama nitakuwa na mtu mkubwa kunisaidia. Wana JF msinihukumu kwa makosa niliyoyafanya nisaidieni mawazo. Karibuni

Niaje kaka
 
rudi depo anza upya

Nijuavyo mimi kama kweli uliondoka kama unavyoeleza basi wewe upo ktk orodha ya watu wanaotafutwa kwa utoro hivyo kuwa makini na huyo jamaa anayetaka m-chat. Ushauri kama wengine wewe anza sehemu zipo nyingi tu kuwa mvumilivu na utatoka.
 
We umeenda AWOL halafu unataka wakupokee tena? Sahau kabisa labda ungekua na Godfather wa kukushika mkono. Kwani umesomea fani gani uni?
 
haaaw c wewe tu hata mm n hivyo hvyo kaks vuta subira zikitoka zile za proffesional tutajaribu tena! tpdc walitoa je uliomba? coz kule n kutamu kuliko jwtz

mkuu kila mtu anakusifia huko tpdc, mshahara mkubwa au marupurupu ndo mengi? hasa kwa mimi wa level ya degree. ili nizidishe msuli maradufu wa kujiandaa na oral interview
 
tpdc mshahara mkubwa kaka malupulupu labda likizo kama ukiwa na familia kubwa! mm c mjeda hata nimtafute mtoa mada naona unampanikisha mtoa mada hapo! tutaonana mikindani mtwara getini ntawapekuwa barabara@ nyati
 
Back
Top Bottom