Kupenda nisipopendwa...

Kupenda nisipopendwa...

Joined
Aug 4, 2019
Posts
20
Reaction score
56
Moyo wangu unaumia sana una kidonda nimempenda mtu ambaye hana mda na mimi. Iko hivi, tumejuana miaka 9 kama marafiki kipindi chote alikuwa ananitaka ila si kuona muda muafaka, na si kutaka kupoteza pia nami nilikuwa nataka nijipange kwanza ndo niwe naye. Well akapata wadada wawili na wamezaa nae mmoja wa kike mwingine wa kiume kaachana na wote.

Mwaka huu nikasema niwe naye, nikimfata nauli ya uber nalipia mwenyewe kama gari najaza mafuta mwenyewe, yeye hajiongezi kama mwanaume. Nina kazi yangu najimudu naye ana kazi nzuri zaidi yangu mie, kipato mara 7 zaidi ya cha kwangu. Hapo kutuma msg mpaka mie nianze, nikipiga wakati mwingine hapokei, najua anakuwa busy na kazi ila hawezi kosa dakika chache za kunipigia, najikuta naumia sana.

Namuwaza nampenda ila naona yeye bado ana umwana mwingi na mimi anaendelea kunichukulia kama mshikaji badala ya mpenzi. Nawaza au sababu mwenzangu ni PhD holder? Au sababu yeye ni familia bora na mie nimetoka usekweni?

Leo nimemblock WhatsApp hapa moyo unaniuma sana yaani naumia sana najikaza.

Tafadhali marafiki nipeni mawazo yenu nsimuunblock wala kumtafuta na akintafuta nsimsikilize.

Ee Mungu wangu naomba unipe mwanaume uliyemuandaa kwa ajili yangu, natumia hajafariki kwenye moto Morogoro.
 
Pole sana. Ukiona mpenzi wako hana muda na wewe ujue hakupendi. Mtu unayempenda huwezi kukosa muda hata kama unafanya nini. Kuwa busy na kazi
Ukiendelea kumng'ang'ania atakumimba kisha atakuacha kama wale wengine.
 
Chimwemwe, huyo PhD holder atakuwa tu mwalimu wa chuo, sasa wewe mpotezee achana nae kabisa hakupendi wala nini, mwanaume anayekupenda hata kama una makosa 100, 000 atafuta sababu moja nzuri ya kubaki na wewe.
Huyo alikuwa anataka game za kishkaji tu keshapata matokeo ndo hayo, Pole mwanamke mwenzangu.
 
Haya mambo ni nadra sana kuyasikia kwa wanawake kwa experience yangu, pole sana mkuu jifunze kuzoea hali na u move on na maisha yako uwe na msimamo ukiamua kuwa kmya utamsahau ila ukiendeleza mawasiliano hukomboki na hali itazidi kuwa mbaya kwako huku mwenzio akiendelea kuyafurahia maisha, huyo hakuhitaji.
 
Hahaha. Unatikisa kiberiti kwa block. Mi unblock apate mtoto wa tatu kwa mama wa tatu tofauti
 
Daah Njoo tufarijiane pm mkuu hata Mimi yamenikuta ya kunikuta huko sina amani kabisa natamani kulia wamenimwagia pombe yangu bar jana binadamu sio wazur.

Tuachane na hapo juu zlkuwa mbwembwe tu all yu nidi tu do is to move on.. utapata atakae kuthamini jamaa anaonyesha hana interest na wewe tenaa baada ya wewe kumkatili first time
 
Back
Top Bottom