Kuomba ushauri wa biashara ya usafirishaji mizigo kwa gari aina ya canter

Kuomba ushauri wa biashara ya usafirishaji mizigo kwa gari aina ya canter

Riziki Omary

Member
Joined
Oct 9, 2020
Posts
5
Reaction score
4
Habarini wanajamvi samahanini naomba kuuliza kidogo juu ya hili swala.

Ninampango wa kununua CANTER USED ilio katika hali nzuri ili niweze kufanya biashara ya usafirishaji ambapo katika biashara mimi nitakaa kama Tandu kushoto. Sasa naombeni msaada wenu wa A,B,C juu ya hii biashara

1. Naomba kujua ni aina gani ya Canter ni nzuri na imara kwaajili ya biashara ya usafirishaji mizigo kwa canter kulingana na mazingira yetu ya hapa TZ na ukubwa(Tani) ngapi ni mzuri ambao gari itakua rahis kuchora kijiweni

2. Je ni nini vya kuzingatia hasa vya kiufundi endapo nitaenda nunua gari hii used ili nisije nikanunua gari mbovu, je ni vipi hasa vya msingi natakiwa kuzingatia wakat nakagua gari ili nisije nikashikishwa?

3. Ni njia gani nzuri ya kuifanya biashara hii ya gari ya mizigo canter iweze kunilipa

4. Kwa haraka haraka Canter ilio katika hali nzuri je naweza kuipata kwa gharama ya used SHINGAPI, hii iwe gari ambayo direct inaingia mzigoni sio ya kupita kwa fundi

5. Kama ndugu yeyote analo la kuchagia ambalo ni la muhimu anaweza kuniongezea.

NB kijiwe cha mzigo na plan KIBAIGWA AU DODOMA MJINI
 
Well, kwenye aina nzuri ya canter nakushauri uchukue canter box yenye Engine ya 4d33 ya top cover jembamba, engine hizo ni imara sana na zina nguvu kibongo bongo inabeba hadi tani 5, pia spea zake zipo.

Ukienda kununua gari used kwanza kabisa angalia budjet yako kama inatosha upate gari ipi, unaweza ukanunua body alafu ukanunua engine separate ukaja kuivalisha ukapata gari nzuri... Au unanunua gari ambayo ipo full, ambapo utaangalia body iwe nzur, ubora wa engine, angalia gearbox na dif kama hauelewi nenda na fundi pia cha muhimu hio gari kama ilikuwa inatumika kibiashara nenda TRA na mmiliki wakutolee tax clearance ili usije ukauziwa gari yenye madeni ya kodi za mapato. Pia na LATRA nenda ujue kama hio gari inakubalika kupata kibali au kama inacho kibali, kagua na madeni ya polisi kupitia plate number nk..

njia nzuri ya kuifanya biashara hii unaweza kwanza kufanya uchunguz kwa wazoefu wa hio kaz ili wakuelezee ikoje pia tafuta dereva atakayeweza kukupa michongo ya kupata kijiwe kizur cha kaz.

Kununua canter used unaweza chagua ununue gari full au ununue body alafu ukanunua engine gearbox ukavisha yoote ni maamuzi yako. Ila kama unataka gari full uwe angalau kuanzia Milion 22 na kitu,,, au ukanunua mashine 4d33 ya Milion 11.5 alafu ukanunua body Milion 6-8 ukavisha ukapata gari nzuri kwa milion 20...

Anyway nimekupa experience yangu ya maswali uliyouliza i hope nimekufumbua macho kiasi.
 
Well, kwenye aina nzuri ya canter nakushauri uchukue canter box yenye Engine ya 4d33 ya top cover jembamba, engine hizo ni imara sana na zina nguvu kibongo bongo inabeba hadi tani 5, pia spea zake zipo.

Ukienda kununua gari used kwanza kabisa angalia budjet yako kama inatosha upate gari ipi, unaweza ukanunua body alafu ukanunua engine separate ukaja kuivalisha ukapata gari nzuri... Au unanunua gari ambayo ipo full, ambapo utaangalia body iwe nzur, ubora wa engine, angalia gearbox na dif kama hauelewi nenda na fundi pia cha muhimu hio gari kama ilikuwa inatumika kibiashara nenda TRA na mmiliki wakutolee tax clearance ili usije ukauziwa gari yenye madeni ya kodi za mapato. Pia na LATRA nenda ujue kama hio gari inakubalika kupata kibali au kama inacho kibali, kagua na madeni ya polisi kupitia plate number nk..

njia nzuri ya kuifanya biashara hii unaweza kwanza kufanya uchunguz kwa wazoefu wa hio kaz ili wakuelezee ikoje pia tafuta dereva atakayeweza kukupa michongo ya kupata kijiwe kizur cha kaz.

Kununua canter used unaweza chagua ununue gari full au ununue body alafu ukanunua engine gearbox ukavisha yoote ni maamuzi yako. Ila kama unataka gari full uwe angalau kuanzia Milion 22 na kitu,,, au ukanunua mashine 4d33 ya Milion 11.5 alafu ukanunua body Milion 6-8 ukavisha ukapata gari nzuri kwa milion 20...

Anyway nimekupa experience yangu ya maswali uliyouliza i hope nimekufumbua macho kiasi.
Kaka asante sana hii comment yako naifanyia lamination
 
Well, kwenye aina nzuri ya canter nakushauri uchukue canter box yenye Engine ya 4d33 ya top cover jembamba, engine hizo ni imara sana na zina nguvu kibongo bongo inabeba hadi tani 5, pia spea zake zipo.

Ukienda kununua gari used kwanza kabisa angalia budjet yako kama inatosha upate gari ipi, unaweza ukanunua body alafu ukanunua engine separate ukaja kuivalisha ukapata gari nzuri... Au unanunua gari ambayo ipo full, ambapo utaangalia body iwe nzur, ubora wa engine, angalia gearbox na dif kama hauelewi nenda na fundi pia cha muhimu hio gari kama ilikuwa inatumika kibiashara nenda TRA na mmiliki wakutolee tax clearance ili usije ukauziwa gari yenye madeni ya kodi za mapato. Pia na LATRA nenda ujue kama hio gari inakubalika kupata kibali au kama inacho kibali, kagua na madeni ya polisi kupitia plate number nk..

njia nzuri ya kuifanya biashara hii unaweza kwanza kufanya uchunguz kwa wazoefu wa hio kaz ili wakuelezee ikoje pia tafuta dereva atakayeweza kukupa michongo ya kupata kijiwe kizur cha kaz.

Kununua canter used unaweza chagua ununue gari full au ununue body alafu ukanunua engine gearbox ukavisha yoote ni maamuzi yako. Ila kama unataka gari full uwe angalau kuanzia Milion 22 na kitu,,, au ukanunua mashine 4d33 ya Milion 11.5 alafu ukanunua body Milion 6-8 ukavisha ukapata gari nzuri kwa milion 20...

Anyway nimekupa experience yangu ya maswali uliyouliza i hope nimekufumbua macho kiasi.
Bwana G_Kanakafumu inaonekana we ni mjuzi wa haya mambo, naomba pia uniongezee ufahamu.

Nina mpango wa kununua Misubish Fuso, Long Base au Tandam kama wanavyoiya au Double Dif, Zile zinazofanyiwa modification ya body na kuweka zile Flats/ bomba naweza pia kununua Engine na Body separate? Bei itakuwaje ukilinganishanna Full?
 
Back
Top Bottom