Kuokoka ni nini?,

Kuokoka ni nini?,

Joined
Dec 7, 2012
Posts
23
Reaction score
22
WanaJF habari...
​
Kama mwanaume akimwambia mwanamke akisema…“Unajua mimi nakupenda sana… tena nakupenda saana… Lakini sipo tayari kua bwana wako. Yaani sipo tayari kua mume wako”. Je, mtu huyo atakua anampenda kweli huyo mwanamke? Basi maana ya kuokoka inapatikana kwenye huu mfano. Kwa maana wengi wanamwamini Yesu kua ndie Mwokozi wao lakini hawataki kumkiri na kumkubari awe Bwana wao – (uvuguvugu).

Ni sawa na kumwita mchumba wako "mke wangu" au "mume wangu" lakini hutaki kwenda kujiapiza mbele za Mungu na watu wake (i.e mchungaji/) kwamba "NDIYO NA KUBARI" (YES I DO). Watu kama hawa wanaambatana na
matendo ya mwili ambayo dhahiri nayo ni haya: Uasherati, uchafu, ufisadi, 20kuabudu sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, 21husuda, ulevi, ulafi na mambo mengine yanayofanana na hayo. (wagalatia.5:19-21)

Kwamfano; kuna watu wengi sana wanashudia kuwa "Yesu ni Bwana" lakini kwa miaka yote hiyo hawajawahi sema hivya kwa Yesu mwenyewe kuwa "wewe Yesu ni Bwana wangu". kwahiyo wanashuhudia kwa watu na tena wanaimba kabisa makanisani kuwa Yesu ni Bwana wao lakini kwa muda wote huo hawajawahi hata siku moja kumwambia Yesu kua "kweli wewe Yesu ni Bwana wangu".

Anaekiri kwa Yesu kuwa "Wewe Yesu ni Bwana wangu" ndie alieokoka. lakini yeye anayeshuhudia kwetu tuu na kutuambia sisi kuwa Yesu ni Bwana wake lakini hajamwambia Yesu hayo maneno anayotuambia sisi huyo bado hajaokoka. kwa maana bado hajajiapiza kwa Yesu na kukubali awe Bwana wake.


MSINGI NA MAANA YA KUOKOKA

Ndugu zangu… bila kuficha imeandikwa “kama ukikiri kwa kinywa chako kwamba ‘Yesu ni Bwana’, na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini na hivyo kuhesabiwa haki, tena kwa kinywa mtu hukiri na hivyo kupata wokovu”. Na chini kidogo inasema “Kwa maana, Kila mtu atakayeliitia Jina la Bwana, ataokoka’’ na tena imefafanuliwa waziwazi kabisa kua “Tazama, wakati uliokubalika ndio huu. Tazama, siku ya wokovu ndiyo sasa”. Kwani baada ya Kristo, “mwandamu amewekewa kufa mara moja tu na baada ya kufa akabili hukumu”. (Warumi.10:8-13, 2wakorintho.6:1, waebrania.9:27)

Kuokoka ni kitendo cha wewe kukubali kubatizwa kwa Roho Mtakatifu kwa kumkiri Yesu Kristo kwa kinywa chako kua Bwana na Mwokozi wako, na hivyo unakua umetahiriwa kiroho na kuzaliwa upya (born again) kwa njia ya rohoni (warumi 2:28-29, 10:10,1petro 1:23).

Kuokoka sii kwa dhehebu flani tuu, bali ni kwa wote na madhehebu yote. Lakini wengi sana ni wapagani, kwani “Mtu ye yote ambaye hana Roho wa Kristo, yeye si wa Kristo”. Kuokoka ni kukubali kua “mkristo”. Mkristo maana yake ni “mtu wa Kristo” yaani yule ambae Yesu ni “Bwana na Mwokozi” wake.


Kwahiyo nikisema “mimi nimeokoka”, vilevile ninakua namaanisha kwamba hapa duniani nimeokolewa kutoka katika utawala wa shetani/giza na kupewa utawala wa Mungu kwa kupewa Roho Mtakatifu, ambaye ndiye guarantee ya uzima wa milele (waefeso.1:13-14).

Hivyo Kuokoka pia ni utimilifu wa imani yako kwa kupokea wokovu kwa kumuamini Bwana Yesu, kwani maana ya imani ni “kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni udhahiri wa mambo yasiyoonekana” (Waebrania.11:1)


Kuokoka ni kitendo cha wewe ku-sign kua mwana wa Mungu kwa kukubali kuwa mtakatifu kwa utakaso wa damu ya Yesu na Hivyo wewe kupewa Roho Mtakatifu ambae kwa huyu unapigwa mhuri katika roho yako kama garantii ya wewe kuepuka/kuokolewa na adhabu ya mauti ya milele ndani ya ziwa la moto wa milele. Kwamaana “bila ya utakatifu, hakuna atakae mwona Bwana”. (Waebrania 10:10, 12:14 Waefeso 1:13-14 na Wagalatia 3:26-29)”


KWA KINYWA CHAKO UNABATIZWA KWA ROHO MTAKATIFU

Kutumia mdomo ni muhimu kabisa kwasababu kuna sheria iliwekwa na Mungu kua “Mauti na uzima viko katika uwezo wa ulimi”. Kwahiyo kwa ulimi wako mwenyewe utapata uzima wa milele kwa kukikiri kwa kiny​wa chako kwamba ‘Yesu ni Bwana’. Vivyo hivyo, kwa kinywa chako unaweza kupata mauti ya milele kwa kumkana Kristo au kwa kiburi cha wewe kuto kukiri kua “Yesu ni Bwana” wakati ukiwa hai hapa duniani. (Mithali.18:21).

Vile vile kwa mdomo Adam alidanganywa na hatimae vizazi vyote vikapata mauti. Basi tena kwa mdomo wako unapata wokovu pia. Yaani kama vile kosa la mtu mmoja (Adam) lilivyoleta hukumu kwa watu wote, vivyo hivyo pia kwa tendo la mtu mmoja (Yesu) la haki huleta kuhesabiwa haki kule kuletako uzima kwa wote (Warumi.5:12-19, 10:8-13)


UKISEMA ‘YESU NI BWANA’ LAZIMA UWE NA DHAMIRA YA KWELI

Wengi wanasema na tena wanaimba kila siku makanisani mwao kua “Yesu ni Bwana” lakini hawajatia nia mioyoni mwao. Na kwa watu kama hawa Mungu anasema “Watu hawa wananiheshimu kwa midomo yao, lakini mioyoni mwao wako mbali nami. Huniabudu bure”.(Marko.7:6-7).

Neno Bwana maana yake ni Lord ambayo pia ni “Owner”. Kwa hiyo ukisema “Yesu ni Bwana wangu”…inamaana Mungu anakumiliki, roho yako imezaliwa upya (born again), na mwili wako ni hekalu la Roho Mtakatifu na wala sio wako tena. Kwahiyo lazima awe Bwana, kwani “Kama vile ambavyo mwili pasipo roho umekufa, kadhalika nayo imani pasipo matendo imekufa (1wakorintho.6:13-20, Yakobo 2:26)


KUONGOKA VS KUOKOKA

Kuongoka maana yake ni “kusilimu”. Ni kubadilisha mfumo/imani moja kwenda nyingine. Kwa mfano Mtume Paulo aliongoka kutoka dini ya kiyahudi na baadae kuokoka kwa kupewa Roho Mtakatifu. Lakini wanafunzi 11 wa Yesu wao hawakuongoka bali waliokoka kwa kujazwa na Roho Mtakatifu. Kwa hiyo mtu anaezaliwa kwenye familia ya kikristo yeye haongoki bali anachohitaji ni kuokoka.

Kuongoka ni neno linalotoka na “ongoa” na maana yake ni “convert”. Lakini neno kuokoka (to be saved) ni kitenzi cha nomino “wokovu” ambayo ni “salvation”. (math:18:3,Maten.15:3-11,1tim.3:6)
 

Attachments

KUBATIZWA KWA MAJI VS KWA ROHO
Watu wengi hubatizwa kwa Roho kwa kujazwa na Roho Mtakatifu hata bila ya kubatizwa kwa maji. Hii inatokea sana injili ikihubiriwa sehemu ambazo watu hawayajui makanisa wala hawajawahi kubatizwa kwa maji. Hata familia ya tajiri Kornelio pia ilikua hivyo. Hadi mtume Petro alishangaa akasema "Je, kuna mtu ye yote anayeweza kuzuia watu hawa wasibatizwe kwa maji? Wamempokea Roho Mtakatifu kama sisi tulivyompokea".


Kubatizwa kwa maji ni kwa ajili ya toba, Vilevile ubatizo wa maji ambao kila kanisa hubatiza ni kwa ajili ya kukubali kua mwanfunzi na mfuasi wa injili ya Yesu kristo. Na huu ubatizo hata wale wenye Roho Mtakatifu hubatizwa (Yohana 3:5-6,math.3:11-17). Kwa hiyo kubatizwa kwetu kwa maji ni kwa ajili ya kuipokea injili na kua mwanafunzi wa Yesu. Na ndio maana Yohana mbatizaji alisema "Mimi nawabatiza kwa maji, lakini Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu"


Kwa mfano imeandikwa "Siku hizo Yohana Mbatizaji alikuja akihubiri katika nyika ya Uyahudi, akisema, "Tubuni, kwa maana Ufalme wa Mbinguni u karibu". Kwa hiyo yeyote aliyeikubali injili hii ya ufalme wa Mbinguni alikua mwanafunzi kwa kubatizwa kwa maji.

Yesu (sinless) alibatizwa kwa Maji si kwa ajili ya kupewa Roho Mtakatifu (Yeye alizaliwa nae tayari), bali ilikua ni kwa ajili ya kuchukua injili ya "Ufalme wa Mbinguni/Mungu". Injili ambayo Yohana aliihubiri kuandaa njia kwa ajili ya Bwana Yesu. Na baada ya Yesu kuichukua injili hii kwa kubatizwa kwa maji, "Tangu wakati huo, Yesu alianza kuhubiri akisema: "Tubuni, kwa maana Ufalme wa Mbinguni umekaribia" (math.3:2-17, 4:17)


Baada ya Yesu Kufa msalabani na Kufufuka tena, Roho Mtakatifu akamwagwa duniani, na Kwa njia hiyo ufalme wa Mbinguni ukawa umewasiri duniani. Kwa maana kila mwenye Roho Mtakatifu ana utawala/Ufalme wa Mungu. Na ndio maana pia Yesu alisema '‘Amin, amin nawaambia, kuna watu waliosimama hapa ambao hawataonja mauti kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu ukija katika nguvu"(mark.9:1). Hapa Akina Peter, Mathayo, n.k. walikua wamesimama nae miaka 2000 iliyopita na ndio hao pamoja na wengine waliopokea ufalme wa Mungu/Roho Mtakatifu kabla ya kufa.


KWA WANAOPOTEA… KUOKOKA NI UPUUZI KWAO

Imeandikwa "ujumbe wa msalaba kwa wale wanaopotea ni upuzi, lakini kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu". Na mahali pengine inasema "Mtu ambaye hana Roho wa Mungu hawezi kupokea mambo yatokayo kwa Roho wa Mungu, kwa kuwa ni upuzi kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa sababu hayo yanaeleweka tu kwa jinsi ya rohoni". Lakini ni kwa neema ya Mungu isiyopimika, hata wenye dhambi huielewa injili na hata kuamini na kupata wokovu kwa kujazwa na Roho Mtakatifu (1korith.2:14-31).

Kwani "hata tulipokuwa wafu kwa ajili ya makosa yetu, alitufanya tuwe hai pamoja na Kristo Yesu, yaani, mmeokolewa kwa neema. Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani, wala hii si kwa matendo yenu mema..." (Waefeso.2:1-10). (wengi sana mnayo hii neema likini mioyo ni migumu)


DHAMBI ZA MAUTI VS ZISIZO ZA MAUTI
Kwa mkono wa Yohana, Roho Mtakatifu anafafanua kwa kusema "Kama mtu akimwona ndugu yake anatenda dhambi isiyo ya mauti, inampasa aombe, naye Mungu atampa uzima mtu huyo, yaani, kwa wale ambao dhambi yao si ya mauti. Iko dhambi ya mauti, sisemi kwamba utaomba kwa ajili ya hiyo. Jambo lo lote lisilo la haki ni dhambi, lakini iko dhambi isiyo ya mauti". Kwa walio okoka na watakao okoka; JIEPUSHENI NA UZINZI/UASHERATI (James.1:14-15.2:10-11, 1John.5:16-17, Acts.15:23-29, 1corinth.6:18, Walawi.20, Ephes.5:5, colos.3:5, Hebrews.12:16-17).


TUFANYE NINI ILI TUOKOKE?
Yesu mwenyewe amesema "Je, kuna ye yote miongoni mwenu, ambaye mtoto wake akimwomba samaki, atampa nyoka badala ya samaki? Au mtoto akimwomba yai atampa ng'e? Basi ikiwa ninyi mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, si zaidi sana Baba yenu wa mbinguni atawapa Roho Mtakatifu wale wamwombao?" Na kwa upole kabisa Roho Mtakatifu anasema "LEO, kama mtaisikia sauti Yake, MSIFANYE MIOYO YENU MIGUMU".

Yeyote asie na Mwanga analo Giza. Tumia mdomo wako sasa. Popote pale ulipo chukua dakika mbili. OMBA NA AMINI, ILI UOKOKE LEO.


ONYO! TAFADHALI USIOMBE SALA HII KAMA UNAMZAHA MOYONI MWAKO NA BADO UNAPENDA GIZA ILI USIJE UKAWA MWANA WA IBILISI MALA MBILI ZAIDI. LAZIMA UJIKANE MWENYEWE NA UAMINI KWELI.


OMBA HIVI; "Bwana Yesu ninakuhitaji. Ninakushukuru kwa vile ambavyo ulizifia dhambi zangu msalabani. Naamini kwamba Mungu alikufufua kutoka kwa wafu. Nakiri kua mimi ni mdhambi. Nisamehe dhambi zangu zote nilizozifanya Kwa kuwaza, kunena, na kutenda. Nisaidie kuzishinda dhambi zote. nipokee uwe Bwana na Mwokozi wangu. Nitakase kwa damu yako ya thamani na unibatize kwa Roho Mtakatifu. Andika Jina Langu kwenye kitabu cha Uzima wa Milele. Wewe ni Bwana wangu kuanzia sasa hata milele… Amen".

 
Kuokoka au wokovu ni kile Yesu anafanya ndani yako mara tu ukishampokea. Wokovu ni badiliko linalotokea katika maisha ya mtu kutoka kwenye ujinga, uharibifu, na kupata akili njema. Kabla mtu hajjaokoka huwa chini ya utawala wa ufalme wa shetani lakini akishaokoka huwa chini ya utawala wa ufalme wa Mungu na kuelekezwa na kuendeshwa na ufalme huo.Ndio maana neno la Mungu husema naye alituokoa katika nguvu za giza na kutuingiza katika ufalme wa pendo lake ambao katika huo tuna ukombozi yaani masamaha ya dhambi zetu. Hivyo ukishaokoka unahamishwa kutoka ufalme uliokua unamiliki hapo mwanzo wa giza au shetani na kuhamishiwa kwenye ufalme wa mwana wa pendo lake yaani ufalme waMungu.
 
''Atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa''- Mat 10:22. (Inamaanisha nini?)
 
''Atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa''- Mat 10:22. (Inamaanisha nini?)

Hiyo inamaana pia kwamba mtu anaweza pia akaupoteza wokovu hapa hapa duniani... Yaani anaweza kukata tamaa na kurudi nyuma na hivyo kuupoteza wokovu. KAMA VILE AMBAVYO WAISRAELI WENGI WALI-OKOLEWA KUTOKA MISRI LAKINI WALISHINDWA KUFIKA KAANANI. (kwahiyo nao walishindwa kuvumilia hadi mwisho). hata leo pia wengi wanaokolewa kutoka kwenye utumwa wa dhambi lakini wanashindwa kumalizia safari yao ya wokovu walioupata kwa sababu ya ukaidi na kutokuamini kwao.

pia kama vile ambavyo Kristo akiwa msalabani alivyosema "IMEKWISHA" (Yohana.19:30). lakini tena baada ya kuumba mbingu mpya na Nchi mpya Yesu atesama tena "IMEKWISHA" (ufunuo.21:6)

KWASASA TUNAOPOKEA WOKOVU WA ROHO ZETU... AMAMBAO KWA HUO WOKOVU WA ROHO NI GUARANTEE YA SISI KUPATA WOKOVU WA MIILI YETU. ndio maana imeandikwa "Nanyi ikiwa Roho wa Mungu aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu anakaa ndani yenu, Yeye aliyemfufua Kristo Yesu kutoka kwa wafu ataihuisha pia miili yenu ambayo hufa, kwa njia ya Roho Wake akaaye ndani yenu" (warumi.8:11). na Kuhusu hii miili ya sasa (ambayo bado haijaokolewa) imeandikwa "nyama na damu haviwezi kuurithi Ufalme wa Mungu, wala kuharibika kurithi kutokuharibika" na sehemu nyingine inasema "nia ya mwili ni uadui na Mungu, kwa maana haiitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii. Wale wanaotawaliwa na mwili, hawawezi kumpendeza Mungu."(soma vizuri 1korintho.14).

Lakini kwa wale waliokubali kuokoka imeandikwa "Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani, wala hii si kwa matendo yenu mema. Hii ni zawadi kutoka kwa Mungu, si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu" (waefeso.2:8-9).

Kwahiyo nikisema "mimi nimeokoka", vilevile ninakua namaanisha kwamba hapa duniani nimeokolewa kutoka katika utawala wa shetani/giza na kupewa utawala wa Mungu kwa kupewa Roho Mtakatifu, ambaye ndiye guarantee ya uzima wa milele (waefeso.1:13-14).

Hivyo Kuokoka pia ni utimilifu wa imani yako kwa kupokea wokovu kwa kumuamini Bwana Yesu, kwani maana ya imani ni "kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni udhahiri wa mambo yasiyoonekana" (Waebrania.11:1) na ndio maana imeandikwa "TAZAMA,WAKATI ULIOKUBALIKA NDIYO SASA; TAZAMA SIKU YA WOKOVU NI SASA" (2korintho.6:2).

KWAHIYO YEYE ANAESEMA HAKUNA WOKOVU DUNIANI NI MWONGO TENA ANAMFANYA MUNGU MWONGO KWANI MUNGU ALIMLETA MWANAE ILI TUPATE KUOKOLEWA.
 
WanaJF habari...

Kama mwanaume akimwambia mwanamke akisemaUnajua mimi nakupenda sana tena nakupenda saana Lakini sipo tayari kua bwana wako. Yaani sipo tayari kua mume wako. Je, mtu huyo atakua anampenda kweli huyo mwanamke? Basi maana ya kuokoka inapatikana kwenye huu mfano. Kwa maana wengi wanamwamini Yesu kua ndie Mwokozi wao lakini hawataki kumkiri na kumkubari awe Bwana wao (uvuguvugu).

Ni sawa na kumwita mchumba wako "mke wangu" au "mume wangu" lakini hutaki kwenda kujiapiza mbele za Mungu na watu wake (i.e mchungaji/) kwamba "NDIYO NA KUBARI" (YES I DO). Watu kama hawa wanaambatana na
matendo ya mwili ambayo dhahiri nayo ni haya: Uasherati, uchafu, ufisadi, 20kuabudu sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, 21husuda, ulevi, ulafi na mambo mengine yanayofanana na hayo. (wagalatia.5:19-21)

Kwamfano; kuna watu wengi sana wanashudia kuwa "Yesu ni Bwana" lakini kwa miaka yote hiyo hawajawahi sema hivya kwa Yesu mwenyewe kuwa "wewe Yesu ni Bwana wangu". kwahiyo wanashuhudia kwa watu na tena wanaimba kabisa makanisani kuwa Yesu ni Bwana wao lakini kwa muda wote huo hawajawahi hata siku moja kumwambia Yesu kua "kweli wewe Yesu ni Bwana wangu".

Anaekiri kwa Yesu kuwa "Wewe Yesu ni Bwana wangu" ndie alieokoka. lakini yeye anayeshuhudia kwetu tuu na kutuambia sisi kuwa Yesu ni Bwana wake lakini hajamwambia Yesu hayo maneno anayotuambia sisi huyo bado hajaokoka. kwa maana bado hajajiapiza kwa Yesu na kukubali awe Bwana wake.


MSINGI NA MAANA YA KUOKOKA

Ndugu zangu bila kuficha imeandikwa kama ukikiri kwa kinywa chako kwamba Yesu ni Bwana, na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini na hivyo kuhesabiwa haki, tena kwa kinywa mtu hukiri na hivyo kupata wokovu. Na chini kidogo inasema Kwa maana, Kila mtu atakayeliitia Jina la Bwana, ataokoka na tena imefafanuliwa waziwazi kabisa kua Tazama, wakati uliokubalika ndio huu. Tazama, siku ya wokovu ndiyo sasa. Kwani baada ya Kristo, mwandamu amewekewa kufa mara moja tu na baada ya kufa akabili hukumu. (Warumi.10:8-13, 2wakorintho.6:1, waebrania.9:27)

Kuokoka ni kitendo cha wewe kukubali kubatizwa kwa Roho Mtakatifu kwa kumkiri Yesu Kristo kwa kinywa chako kua Bwana na Mwokozi wako, na hivyo unakua umetahiriwa kiroho na kuzaliwa upya (born again) kwa njia ya rohoni (warumi 2:28-29, 10:10,1petro 1:23).

Kuokoka sii kwa dhehebu flani tuu, bali ni kwa wote na madhehebu yote. Lakini wengi sana ni wapagani, kwani Mtu ye yote ambaye hana Roho wa Kristo, yeye si wa Kristo. Kuokoka ni kukubali kua mkristo. Mkristo maana yake ni mtu wa Kristo yaani yule ambae Yesu ni Bwana na Mwokozi wake.


Kwahiyo nikisema mimi nimeokoka, vilevile ninakua namaanisha kwamba hapa duniani nimeokolewa kutoka katika utawala wa shetani/giza na kupewa utawala wa Mungu kwa kupewa Roho Mtakatifu, ambaye ndiye guarantee ya uzima wa milele (waefeso.1:13-14).

Hivyo Kuokoka pia ni utimilifu wa imani yako kwa kupokea wokovu kwa kumuamini Bwana Yesu, kwani maana ya imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni udhahiri wa mambo yasiyoonekana (Waebrania.11:1)


Kuokoka ni kitendo cha wewe ku-sign kua mwana wa Mungu kwa kukubali kuwa mtakatifu kwa utakaso wa damu ya Yesu na Hivyo wewe kupewa Roho Mtakatifu ambae kwa huyu unapigwa mhuri katika roho yako kama garantii ya wewe kuepuka/kuokolewa na adhabu ya mauti ya milele ndani ya ziwa la moto wa milele. Kwamaana bila ya utakatifu, hakuna atakae mwona Bwana. (Waebrania 10:10, 12:14 Waefeso 1:13-14 na Wagalatia 3:26-29)


KWA KINYWA CHAKO UNABATIZWA KWA ROHO MTAKATIFU

Kutumia mdomo ni muhimu kabisa kwasababu kuna sheria iliwekwa na Mungu kua Mauti na uzima viko katika uwezo wa ulimi. Kwahiyo kwa ulimi wako mwenyewe utapata uzima wa milele kwa kukikiri kwa kinywa chako kwamba Yesu ni Bwana. Vivyo hivyo, kwa kinywa chako unaweza kupata mauti ya milele kwa kumkana Kristo au kwa kiburi cha wewe kuto kukiri kua Yesu ni Bwana wakati ukiwa hai hapa duniani. (Mithali.18:21).

Vile vile kwa mdomo Adam alidanganywa na hatimae vizazi vyote vikapata mauti. Basi tena kwa mdomo wako unapata wokovu pia. Yaani kama vile kosa la mtu mmoja (Adam) lilivyoleta hukumu kwa watu wote, vivyo hivyo pia kwa tendo la mtu mmoja (Yesu) la haki huleta kuhesabiwa haki kule kuletako uzima kwa wote (Warumi.5:12-19, 10:8-13)


UKISEMA YESU NI BWANA LAZIMA UWE NA DHAMIRA YA KWELI

Wengi wanasema na tena wanaimba kila siku makanisani mwao kua Yesu ni Bwana lakini hawajatia nia mioyoni mwao. Na kwa watu kama hawa Mungu anasema Watu hawa wananiheshimu kwa midomo yao, lakini mioyoni mwao wako mbali nami. Huniabudu bure.(Marko.7:6-7).

Neno Bwana maana yake ni Lord ambayo pia ni Owner. Kwa hiyo ukisema Yesu ni Bwana wanguinamaana Mungu anakumiliki, roho yako imezaliwa upya (born again), na mwili wako ni hekalu la Roho Mtakatifu na wala sio wako tena. Kwahiyo lazima awe Bwana, kwani Kama vile ambavyo mwili pasipo roho umekufa, kadhalika nayo imani pasipo matendo imekufa (1wakorintho.6:13-20, Yakobo 2:26)


KUONGOKA VS KUOKOKA

Kuongoka maana yake ni kusilimu. Ni kubadilisha mfumo/imani moja kwenda nyingine. Kwa mfano Mtume Paulo aliongoka kutoka dini ya kiyahudi na baadae kuokoka kwa kupewa Roho Mtakatifu. Lakini wanafunzi 11 wa Yesu wao hawakuongoka bali waliokoka kwa kujazwa na Roho Mtakatifu. Kwa hiyo mtu anaezaliwa kwenye familia ya kikristo yeye haongoki bali anachohitaji ni kuokoka.

Kuongoka ni neno linalotoka na ongoa na maana yake ni convert. Lakini neno kuokoka (to be saved) ni kitenzi cha nomino wokovu ambayo ni salvation. (math:18:3,Maten.15:3-11,1tim.3:6)
Pitia huku usome kwa kina@nsanzu
 
Back
Top Bottom