Kuoga maji ya baridi

Kuoga maji ya baridi

Barantogwa

Senior Member
Joined
May 3, 2014
Posts
125
Reaction score
152
Watu wa MUNGU, naomba msaada wenu wa kitabibu.

Je, kuna madhara yoyote kiafya kuoga Maji ya baridi baada ya kumaliza mazoezi ya kukimbia umbali mrefu? msaada wenu ni muhimu.
 
Madhara yapo mkuu maana joto la mwili linakuwa juu sana sasa kujimwagia maji baridi kwa ghafla kuna madhara yanaweza kutokea, cha kufanya ni kusubiri kwa mda japo dk 30 kabla ya kuoga.
 
Nijuacho hata gari ikichemka huwa tunaiongezea maji ya baridi siyo ya moto.
 
Mwili unakua na joto la juu ukishatoka kufanya mazoezi, moyo unakua unasukuma damu kwa kasi ili izunguke mwilini kuupoza na kupeleka Oxygen katika kila kona ya mwili, ukioga ghafla maji baridi unaulazimisha upoe kwa haraka na upunguze msukumo wa damu kwa haraka.

Madhara yake unaweza ukapata mshtuko wa moyo, na moyo ukasimama kufanya kazi (ukafa). Unapaswa ukae kwanza mpaka mwili ushuke joto ndio ukaoge.
 
Mwili unakua na joto la juu ukishatoka kufanya mazoezi, moyo unakua unasukuma damu kwa kasi ili izunguke mwilini kuupoza na kupeleka Oxygen katika kila kona ya mwili, ukioga ghafla maji baridi unaulazimisha upoe kwa haraka na upunguze msukumo wa damu kwa haraka.

Madhara yake unaweza ukapata mshtuko wa moyo, na moyo ukasimama kufanya kazi (ukafa). Unapaswa ukae kwanza mpaka mwili ushuke joto ndio ukaoge.
Je, nikioga maji ya moto
 
Je nikioga maji ya moto
Maji ya moto ni mazuri kuoga baada ya mazoezi, kwanza yanasaidia mzunguko wa damu mwilini, pia yanaongezea ngozi joto na kufanya damu isukumwe kwenye ngozi, yanalainisha misuli na kusafisha ngozi ya mwili (kwa kufungua matundu ya ngozi yanayotumika kutolea jasho na uchafu). Ndio maana ukitoka kufanya mazoezi ukaoga maji ya moto unajihisi mwili mwepesi na unajihisi vizuri.
 
Ahsanteni Sana kwa ushauli wenu wataaramu wa mambo ya afya.
 
Mwili unakua na joto la juu ukishatoka kufanya mazoezi, moyo unakua unasukuma damu kwa kasi ili izunguke mwilini kuupoza na kupeleka Oxygen katika kila kona ya mwili, ukioga ghafla maji baridi unaulazimisha upoe kwa haraka na upunguze msukumo wa damu kwa haraka.

Madhara yake unaweza ukapata mshtuko wa moyo, na moyo ukasimama kufanya kazi (ukafa). Unapaswa ukae kwanza mpaka mwili ushuke joto ndio ukaoge.
Ahsante Sana mkuu kwa ushauli wako, Jehovah MUNGU akubaliki.
 
Mwili unakua na joto la juu ukishatoka kufanya mazoezi, moyo unakua unasukuma damu kwa kasi ili izunguke mwilini kuupoza na kupeleka Oxygen katika kila kona ya mwili, ukioga ghafla maji baridi unaulazimisha upoe kwa haraka na upunguze msukumo wa damu kwa haraka.

Madhara yake unaweza ukapata mshtuko wa moyo, na moyo ukasimama kufanya kazi (ukafa). Unapaswa ukae kwanza mpaka mwili ushuke joto ndio ukaoge.

I don't think so!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom