Kundi la vijana Tanzania ( jobless & graduates)

Kundi la vijana Tanzania ( jobless & graduates)

Saint Ivuga

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2008
Posts
55,028
Reaction score
59,657
Sipo hapa kulaumu,
Ila kuna jambo najaribu kuliweka mezani...
Kuna kundi kubwa sana la vijana nadhani ndio nguvu kazi ya taifa, hawa vijana toka kipindi cha JK walikuwa wanalalamika ajira hakuna, uchaguzi ukapita salama* na sasa hivi ni awamu nuingine mpya.

Ni wazi hili kundi limesahaulika kabisa, na mkuu wetu sidhani kama ana mpango wowote wa kuwasaidia hawa vijana kwa nionavyo mimi.
Kinachotokea ni mchaka mchaka kama headmaster anavyoongoza shule ya sekondary. Kwanza huwezi kunyanyua ulimi wako kujibishana na headmaster never.

Sasa nini mstakabali wa hili kundi?
Wakalime? Haiwezekani wote kwenda kulima. Hapa kinachotakiwa ni kila mtu binafsi kwa uwezo wake akomae tu kivyake vyake.

Sasa swali linakuja mambo yakizidi kuwa mabaya nini kitatokea kwa sababu ni wazi mwenye shibe tayari ameshamsahau mwenye njaa, kutokana na mtizamo wake anajiona yupo sahihi sana ila watu wanaumia huku akiwa hana hata interest ya kutaka kujua hali halisi.

Kigezo chake anasema watu walikuwa wapigaji.
Kasahau yeye alikuwa ndani ya huo mfumo kuliko sisi vijana ambao hata hatujui kitu, kwanza tulikuwa hata hatujui kuwa kuna wafanyakazi hewa, yeye alikuwa kwenye system kwa muda mrefu sana aliona na anajua.
Hao wapigaji na watu wa madili anaodhani wanaumia sasa hivi wala hata hawaumii.

Wanaoteseka ni kundi lingine kabisa ambalo hata halijawahi kuwa kwenye system, wale wapigaji anaowasema yeye sasa hivi wamejitune na wanaendelea na maisha yao ya kawaida sana na hakuna hata mmoja anayeisoma namba.

Hapa ninachokiona ni wrong approach to wrong person.
Kila kitu kipo wazi, graduate yupo kitaa anakula vumbi unamuambia alizoea upigaji, kuna uhalisia hapo?

Je nini hatima ya hili kundi kubwa sana hapa Tanzania ?
Mtizamo wa Saint Ivuga sio mtizamo wa JF
 
Mi naona huku ni kutengeneza tabaka LA watu wengi (vijana) kutokupata ajira serikalini LA msingi serikali iliangalie hili kwa ufasadha kabla haijawa balaaa
 
Ila katka kumbukumbu zangu,ulikuwa Team
*CCM*
Umehama lin mkuu?
 
Ila katka kumbukumbu zangu,ulikuwa Team
*CCM*
Umehama lin mkuu?
Sijawahi kundi ccm. Ila nina kadi ya ccm kama wewe na nina kadi ya chadema pia ( wewe huna)
Lete bandiko lololte kuthibitisha.
 
To be honest vijana tunasafari ndefu sana hasa katika wakati huu matamko ni mengi yasiyotekelezeka alisema anahakiki watumishi leo kaja anasema anafumua mfumo wa utumishi ulikuwa wa kipigaji lakini akumbuke nayeye alikuwa ndani huo huo mfumo enzi akiwa waziri basi naye alikuwa mpigaji au? Anasema vijana tujiajiri je yeye aliwahi kujiajiri?
 
Sipo hapa kulaumu,
Ila kuna jambo najaribu kuliweka mezani...
Kuna kundi kubwa sana la vijana nadhani ndio nguvu kazi ya taifa, hawa vijana toka kipindi cha JK walikuwa wanalalamika ajira hakuna, uchaguzi ukapita salama* na sasa hivi ni awamu nuingine mpya.

Ni wazi hili kundi limesahaulika kabisa, na mkuu wetu sidhani kama ana mpango wowote wa kuwasaidia hawa vijana kwa nionavyo mimi.
Kinachotokea ni mchaka mchaka kama headmaster anavyoongoza shule ya sekondary. Kwanza huwezi kunyanyua ulimi wako kujibishana na headmaster never.

Sasa nini mstakabali wa hili kundi?
Wakalime? Haiwezekani wote kwenda kulima. Hapa kinachotakiwa ni kila mtu binafsi kwa uwezo wake akomae tu kivyake vyake.

Sasa swali linakuja mambo yakizidi kuwa mabaya nini kitatokea kwa sababu ni wazi mwenye shibe tayari ameshamsahau mwenye njaa, kutokana na mtizamo wake anajiona yupo sahihi sana ila watu wanaumia huku akiwa hana hata interest ya kutaka kujua hali halisi.

Kigezo chake anasema watu walikuwa wapigaji.
Kasahau yeye alikuwa ndani ya huo mfumo kuliko sisi vijana ambao hata hatujui kitu, kwanza tulikuwa hata hatujui kuwa kuna wafanyakazi hewa, yeye alikuwa kwenye system kwa muda mrefu sana aliona na anajua.
Hao wapigaji na watu wa madili anaodhani wanaumia sasa hivi wala hata hawaumii.

Wanaoteseka ni kundi lingine kabisa ambalo hata halijawahi kuwa kwenye system, wale wapigaji anaowasema yeye sasa hivi wamejitune na wanaendelea na maisha yao ya kawaida sana na hakuna hata mmoja anayeisoma namba.

Hapa ninachokiona ni wrong approach to wrong person.
Kila kitu kipo wazi, graduate yupo kitaa anakula vumbi unamuambia alizoea upigaji, kuna uhalisia hapo?

Je nini hatima ya hili kundi kubwa sana hapa Tanzania ?
Mtizamo Saint Ivuga sio mtizamo wa JF
subiri mwakani mwezi wa pili
 
Graduate halafu hana ajira - anatakiwa afungwe. Graduate alisoma nini kama hawezi kujiajiri kwenye nchi yenye fursa kama Tanzania? Kila siku nasema, wahindi wanapiga mzigo na matokeo yake yanaonekana, sisi waswahili tunataka tukiamka tukute BMW hapo mlangoni.
 
Vuteni subila vijana wenzangu, mkiona mnacheleweshewa ajila mjiajili.

Poleni sana vijana wenzangu, Hata hivyo nadhani kwa yule alokuwa chuo akijifunza kuajIliwa alikosea saana. Elimu humwezesha mtu kufunguka na kupanuka ubongo ili aweze kukabiliana na changamoto za maisha, na hizi ndo changamoto zenyewe.

Poleni sana vijana wenzangu, nawashauli kuanza kujiajili kama ni kuajiliwa kutakukuta njiani na maisha yatakuwa matamu saana.
 
Graduate halafu hana ajira - anatakiwa afungwe. Graduate alisoma nini kama hawezi kujiajiri kwenye nchi yenye fursa kama Tanzania? Kila siku nasema, wahindi wanapiga mzigo na matokeo yake yanaonekana, sisi waswahili tunataka tukiamka tukute BMW hapo mlangoni.

Mkuu kwa Elimu gani ya kujiajiri?huko shuleni si wanafundishwa kukariri tu makanuni ?lets face it Elimu ya Tanzania sio relevant tena,ndio maana nilisoma humu JF waliohitimu wengi chuo hawako competent kny soko la ajira,Unaweza kusema ni wazembe hawawezi kujiajiri wakati ni mfumo unaowatoa hivo,The system failed them.
 
Nyie vijana wenzangu mnasikitisha sana, tuliomo kwa ajila tunatafuta gia ya kutoka nyie mnalazimisha kuingia!!!!????. Mkajiajili huko achana na utegemezi. Kwani mtu asiye na ajila anakufa kesho??!!! Acheni uvivu wa kufikili.

Nyie hata mkiajiliwa hamtokuwa na ubunifu, njia mbadala na ufanisi mtafanya kazi kwa mazoea Yale mloyakuta sehemu husika. Hamfai kuajiliwa kwa wakati huu wa mabadiliko.
 
Ndugu Rebecca: kama mfumo wa elimu umefeli wewe/yeye kama mwanafunzi by then kwa nini asijitambue yeye anataka nini na anatia juhudi gani kupata atakacho? Sitaki amini kwamba 1+1=2 lakini mwalimu anasema ni tatu na wewe unakubali.

Hata hivyo kwa sasa elimu yetu ni "student centred leaning" means mwanafunz anaamua cha kujifunza. Soo kama mwanafunz katoka chuo akiwa kilaza hivyo ndivyo alivyoamua kuwa. Namaanisha kama ametoka chuo akitaka kuajiliwa hivyo ndivyo alivyopenda kuwa.

Hainiingii akilini kwamba nifeli maisha yangu then nimlaum mtu. Basi let them wait till they get employed.
 
Graduate halafu hana ajira - anatakiwa afungwe. Graduate alisoma nini kama hawezi kujiajiri kwenye nchi yenye fursa kama Tanzania? Kila siku nasema, wahindi wanapiga mzigo na matokeo yake yanaonekana, sisi waswahili tunataka tukiamka tukute BMW hapo mlangoni.
kama na wewe ulishawahi kujiajiri UBARIKIWE ila kama unakuja hapa kukejeli watu ilhali unachoshauri huna experience nacho ULAANIWE
 
Mbaya zaidi hao vijana tayari wanawatoto tayari yaani utegemezi juu ya utegemezi. Sometimes najiuliza hivi haya mambo ya umasikiri na maisha mabovu yataisha kweli kwa watu watu vijana wetu?

Umenichekesha mkulu analaumu vijana wasiojua lolote kuwa ni wapigaji...noma sana hiyo.
 
Back
Top Bottom