Apitakujilamba
JF-Expert Member
- Sep 27, 2013
- 205
- 83
Habari zenu wana jamvi
Mapenzi ni jambo gumu sana hapa duniani na ndio maana mwimbaji mmoja aliimba mapenzi kizungu zungu, leo naomba nije na kisa ambacho kimeshawahi kunitokea kama kijana.
Kuna kipindi nilikuwa na uhusiano na dada fulani, ilitokea tu tulikutana sehemu tukaanzisha urafiki wa kawaida tu, lakini baada ya muda tukajikuta tumekuwa marafiki zaidi. Mara nyingi kwenye mahusiano kunakuwa na siri kubwa baina ya wapendanao, kila mmoja anajua ndani yake kwa nini yupo kwenye uhusiano huo.
Mimi nilimpenda yule dada, lakini mara nyingi napendelea kumtafiti mtu kiundani kabla ya kufall moja kwa moja, tuliendelea na urafiki wetu huku nikiendelea kumdadisi kama huyu dada atanifaa kwenye maisha. Nilikuwa najaribu kumuuliza vitu vingi lakini alikuwa ananijibu partially kwa hiyo sikufanikiwa kupata majibu. Lakini mara nyingi tunasema time will tell, baada ya muda nilikuja kugundua kuwa alikuwa na jamaa yake ila wamekorofishana. Na niligundua hilo baada ya jamaa kuamua kurudisha uhusiano kwa huyo dada. Dada alikuwa anakataa kurudisha uhusiano lakini huyo jamaa alimtumia dada yake huyu rafiki yangu kuwaunganisha tena (dada mtu ndiye alimuunganishia jamaa kabla na ndio hivyo baada ya kugombana alitumika tena kuwaunganisha).
Baada ya muda mambo yakabadilika, maana mawasiliano na yule dada yakapungua, kitu kizuri yule dada alikuwa huru kuniambia kitu gani kimetokea. Kiukweli yule mdada alianza uhusiano na mimi kwa nia ya kutaka kupunguza maumivu yake lakini baada ya kuwa na urafiki nami akajikuta ameingia kwenye mtihani achague yupi, arudi kwa jamaa au aendelee na mimi. Nakumbuka siku moja nilikuwa nae mjini mara tukakutana na mdogo wake yule jamaa, aaaah yule mdogo mtu akaripoti kwa jamaa..... siku walioonana na huyu dada alichezea kipigo cha haja.
Baada ya kumuona dada hana maamuzi ni kama aelewi nini afanye nilibidi mimi nifanye maamuzi ingawa yalikuwa magumu maana nilikuwa nimeshampenda yule dada. Aisee niliamua kutompigia simu na wala kutopokea simu yake kwa kipindi kirefu tu. Alijaribu kunitafuta bila ya mafanikio, nilifanya kila njia nisimuone wala asinione. Ofcourse nilitengeneza mazingira ya dada kuendelea na jamaa yake kwa amani. Baada ya mwaka mmoja, yule dada aliniandikia email kwamba anaolewa na anaomba niende kwenye haruc yake. Nilimtakia kila la heri na kumhaidi kwamba nitahudhuria lakini siku hiyo nilipata udhuru sikuhudhuria.
Baada ya ndoa, mawasiliano yakawa ya kawaida maana nikajua tayari ameolewa kwa hiyo haina shida kwangu wala kwake. Kwa hiyo siku akijisikia kupiga simu atapiga mi nitapokea. Nakumbuka siku moja nikampigia simu nikamtania nikamwambia nimeoa ila samahani nilikuwa cjakutaarifu uhudhurie mmmmh yule dada alibadilika sauti ikabadilika na hapo hapo akakata simu na hakupokea tena.
Baada ya kitambo kidogo sikumbuki nilimpigia au alinipigia lakini nikamwambia kuna siku nilikutania ila mi bado sijaoa nikashangaa dada kafurahi utafikiri nini nikashangaa nikasema yaaani umeolewa halafu hutaki mi nioe. Nilijaribu kumdadisi vizuri maana yule dada hanifichagi kitu, akaniambia siku ile nilivyomwambia vile siku nzima alikuwa analia, nilimuuliza kwa nini jibu lilikuwa anajuta kwa maamuzi aliyofanya.
Hapo lawama zikaanza kuniangukia, kwamba mimi ndio nimesababisha mpaka ameolewa na mtu ambaye hafurahiii ndoa. Alinilaumu kwa kutopokea simu zake kipindi hicho na alinitafuta bila ya mafanikio, kiukweli nilimwambia nilikuwa nakupa muda wa kufikiri maana ulikuwa hauna jibu sahihi. Alinieleza mengi ambayo yanamfanya haione ndoa chungu, lakini nilimtia moyo amwombe mungu maana WE HAVE OUR DREAM BUT GOD CREATES DESTINY.
Mapenzi ni jambo gumu sana hapa duniani na ndio maana mwimbaji mmoja aliimba mapenzi kizungu zungu, leo naomba nije na kisa ambacho kimeshawahi kunitokea kama kijana.
Kuna kipindi nilikuwa na uhusiano na dada fulani, ilitokea tu tulikutana sehemu tukaanzisha urafiki wa kawaida tu, lakini baada ya muda tukajikuta tumekuwa marafiki zaidi. Mara nyingi kwenye mahusiano kunakuwa na siri kubwa baina ya wapendanao, kila mmoja anajua ndani yake kwa nini yupo kwenye uhusiano huo.
Mimi nilimpenda yule dada, lakini mara nyingi napendelea kumtafiti mtu kiundani kabla ya kufall moja kwa moja, tuliendelea na urafiki wetu huku nikiendelea kumdadisi kama huyu dada atanifaa kwenye maisha. Nilikuwa najaribu kumuuliza vitu vingi lakini alikuwa ananijibu partially kwa hiyo sikufanikiwa kupata majibu. Lakini mara nyingi tunasema time will tell, baada ya muda nilikuja kugundua kuwa alikuwa na jamaa yake ila wamekorofishana. Na niligundua hilo baada ya jamaa kuamua kurudisha uhusiano kwa huyo dada. Dada alikuwa anakataa kurudisha uhusiano lakini huyo jamaa alimtumia dada yake huyu rafiki yangu kuwaunganisha tena (dada mtu ndiye alimuunganishia jamaa kabla na ndio hivyo baada ya kugombana alitumika tena kuwaunganisha).
Baada ya muda mambo yakabadilika, maana mawasiliano na yule dada yakapungua, kitu kizuri yule dada alikuwa huru kuniambia kitu gani kimetokea. Kiukweli yule mdada alianza uhusiano na mimi kwa nia ya kutaka kupunguza maumivu yake lakini baada ya kuwa na urafiki nami akajikuta ameingia kwenye mtihani achague yupi, arudi kwa jamaa au aendelee na mimi. Nakumbuka siku moja nilikuwa nae mjini mara tukakutana na mdogo wake yule jamaa, aaaah yule mdogo mtu akaripoti kwa jamaa..... siku walioonana na huyu dada alichezea kipigo cha haja.
Baada ya kumuona dada hana maamuzi ni kama aelewi nini afanye nilibidi mimi nifanye maamuzi ingawa yalikuwa magumu maana nilikuwa nimeshampenda yule dada. Aisee niliamua kutompigia simu na wala kutopokea simu yake kwa kipindi kirefu tu. Alijaribu kunitafuta bila ya mafanikio, nilifanya kila njia nisimuone wala asinione. Ofcourse nilitengeneza mazingira ya dada kuendelea na jamaa yake kwa amani. Baada ya mwaka mmoja, yule dada aliniandikia email kwamba anaolewa na anaomba niende kwenye haruc yake. Nilimtakia kila la heri na kumhaidi kwamba nitahudhuria lakini siku hiyo nilipata udhuru sikuhudhuria.
Baada ya ndoa, mawasiliano yakawa ya kawaida maana nikajua tayari ameolewa kwa hiyo haina shida kwangu wala kwake. Kwa hiyo siku akijisikia kupiga simu atapiga mi nitapokea. Nakumbuka siku moja nikampigia simu nikamtania nikamwambia nimeoa ila samahani nilikuwa cjakutaarifu uhudhurie mmmmh yule dada alibadilika sauti ikabadilika na hapo hapo akakata simu na hakupokea tena.
Baada ya kitambo kidogo sikumbuki nilimpigia au alinipigia lakini nikamwambia kuna siku nilikutania ila mi bado sijaoa nikashangaa dada kafurahi utafikiri nini nikashangaa nikasema yaaani umeolewa halafu hutaki mi nioe. Nilijaribu kumdadisi vizuri maana yule dada hanifichagi kitu, akaniambia siku ile nilivyomwambia vile siku nzima alikuwa analia, nilimuuliza kwa nini jibu lilikuwa anajuta kwa maamuzi aliyofanya.
Hapo lawama zikaanza kuniangukia, kwamba mimi ndio nimesababisha mpaka ameolewa na mtu ambaye hafurahiii ndoa. Alinilaumu kwa kutopokea simu zake kipindi hicho na alinitafuta bila ya mafanikio, kiukweli nilimwambia nilikuwa nakupa muda wa kufikiri maana ulikuwa hauna jibu sahihi. Alinieleza mengi ambayo yanamfanya haione ndoa chungu, lakini nilimtia moyo amwombe mungu maana WE HAVE OUR DREAM BUT GOD CREATES DESTINY.