Kuna tatizo gani Wizara ya Fedha?

Kuna tatizo gani Wizara ya Fedha?

pepopunda

Member
Joined
Sep 16, 2013
Posts
13
Reaction score
7
Itakumbukwa kwamba Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2013/2014 ilipitishwa na Bunge mapema zaidi kuliko ilivyokuwa inafanyika hapo awali.

Kusudio la kupitisha bajeti mapema ilikuwa kuziwezesha wizara na Taasisi za umma kutekeleza mipango yake ya maendeleo kwa wakati mwafaka.

Hata hivyo,kusudio hilo linaonekana kama mchezo wa kuigiza.Wizara nyingi na Taasisi zake mpaka sasa hawajapata kile kilichopita kwenye bajeti na hakuna maelezo yoyote yanayotolewa ili wananchi waweze kujua tatizo hili la kitaifa.

Je,inawezekana ilikuwa bajeti hewa?Kama jibu ni ndio wananchi wamwajibishe nani kwa hadaa hii?Big Results Now ni ndoto ya mchana?Tujadili
 
wewe acha habari zako bana. watanzania mkiambiwa hamna serikali mnafikiri watu wanaowaambia hawana akili.serikali iliyopo ni ya kisanii hamna mfano na ile kitu uliona inawatoa povu wabunge wa ccm pale bungeni na kuishia kuwapiga vejembe na mipasho wabunge wa chadema walivyojaribu kuwachallenge ilikuwa ni kiini macho tuu ile. hii ni kota ya pili inaishia lakini wizara zote ni kama hazipo na kazi zote zinazohitaji fedha zimesimama. jibu rahisi tu ni kwamba serikali haina fedha na imefilisika!!!!!! ndio mtanishangaa lakini ukweli ndio huo.
 
Swali naomba jibu. Hivi jamani Waziri wa Fedha huko hai? Mbona kawa bubu na masuala nyeti ya kiuchumi yanayoendelea km vimashine, nk ? Nini kimekusibu? Au ndio bigresultsnow hangover?
 
Bajeti ni maandishi kwenye karatasi kama maandishi mengine tu. Huku kwenye taasisi subirini kwanza.

Pesa wanatumia viongozi wa nchi kutalii nje ya nchi. Kabla mwisho wa mwaka wa fedha haujaisha mtaletewa 10% ya bajeti yenu.

Kuweni watulivu. Mkibisha mtapigwa tu!
 
Back
Top Bottom