Kuna Siri gani Katika miujiza hii?

Ciprofloxacin.

JF-Expert Member
Apr 15, 2015
1,583
2,696
Wanajamvi imenilazimu kuanzisha mjadala mzito juu ya watumishi wa Mungu ,kwanza kabla sijaendelea nataka niweke wazi kuwa mimi ni muumini mzuri wa Mungu na ninamwabudu Mungu na siyo mungu, Nadhani mnanielewa hapo.
Sababu ya mjadala huu ni baada ya Nabii Geordavie kuvunja ndoa ya mtu, nabii huyo anadaiwa kutembea na mke wa mtu Pamela Geoffrey aliyekuwa secretary wake, ushahidi mzito uliotolewa na mtoto wa Pamela mahakani unadai kuwa, mtoto huyo alikuwa akimwona mama yake akiingia kwenye gari na nabii huyo na kisha linaanza kutikisika.
Mume wa Pamela pia alionyesha ushahidi wa msg za mapenzi mahakamani ambazo nabii alikuwa akimtumia Pamela kwenye simu ya pamela, hakimu aliridhika na kuvunja ndoa, soma zaidi habari hiyo hapa: globalpublishers/nabii geordavie avunja ndoa ya mtu. com
Hoja yangu hapa ni kuwa, hawa watu hata Yesu alisema kuwa siku ya mwisho atawakataa, Mathayo 7:22.Wengi siku hiyo watakuja kwangu wakisema, BWANA tulifanya unabii kwa jina lako, Na kutoa pepo kwa jina lako, Nami nitawajibu. Ondokeni kwangu nyie watenda maovu.
Hawa manabii feki wanatoa wapi uwezo wa kuombea wagonjwa na wakapona? au jina la Yesu hata kama likitamkwa na mwenye dhambi linafanya kazi? Na utajiri huo wanautoa wapi wakati hawafanyi biashara yoyote?
Nini chanzo cha miujiza hiyo na siri yake ni nini?
CC:mshana jr ,mzizimkavu, rakims na wadau wengine tujadili hili jambo, hawa watu ni hatari na wamevunja ndoa nyingi za watu na mbaya zaidi wana wafuasi wengi balaa. ni yaleyale ya Joseph Kibwetere wa Uganda ambaye hadi leo hajulikani alipo baada kuua wafuasi wake wote.
 
Some times mfalme huamua kupoteza kibaraka mmoja ili ufalme wake uendelee kukua na.kusimama, ndiyo maana pepo mkubwa humtoa mdogo ili kuendelea kuaminsha watu kuwa kuna huwepo wa miujiza ya Mungu hapo…………
 
Tutaaminije habari za kusikia. Yesu kutoa tahadhari sio guarantee ya sisi kuamini habari zisizo na ukweli
Kwani anachofundisha ni kibaya? Mbona hata Yesu wanasema alitembea na Mary Magdalena sasa tuamini au tusiamini
 
Back
Top Bottom