Kuna mgomo baridi ndani ya chuo cha Sekomu?

WilsonKaisary

JF-Expert Member
Apr 4, 2017
392
935
sekomu-png.828701
Hivi Tanzania kuna sera au sheria za kumlinda mtumishi yeyote awe wa serikalini au katika kampuni au shirika binafsi? Kama zipo je zinafuata au waathirika wakizihitaji zichukue hatua yake inawezekana? Kwa nini watumishi wengi huvumilia miezi kadhaa bila kupokea mshahara wao? Na ukizingatia ni haki yake, nini kinaacho waogepesha? Je ni kukosa uthubutu au uoga au ubovu wa taasisi zetu za sheria na kusimamia sera zetu ndio unaosababisha?

Kama msomi tu hana uthubutu au hajitambui au ni muoga kudai haki zake, je kwa HOUSE GIRL au HOUSE BOY itakuaje?

Staff ya Chuo cha Sebastian Kulowa Memorial University na wanafunzi wake wote wapo kwenye COMA yani sintofahamu, wanafunzi hawajui lini wanafanya mitihani na hawajui lini watafunga chuo, huku ma-lecture hawajui lini watalipwa sababu iliyopo nyuma ya pazia kuwa hawana vigezo.

Ilikuaje utawala wa chuo au maaskofu waliajiri watu wasio na vigezo? Ni aibu kwa taasisi zinazohusika na kuandaa taifa la kesho linakuwa na uzembe kama huu.

Wizara ya elimu, sayansi na teknolojia kama taasisi husika inapaswa kuingilia kati katika swala hili, na inapaswa tambua kuwa wanafunzi wengi walio chuoni hawana fedha za kujikimu (wategemea BOOM) na muda wa kukaa chuoni unazidi kuongezeka kwa uzembe wa utawala wa chuo.

Wizara ya ajira, nayo inapaswa kuwajibika kama wizara inayosimamia maslahi ya watumishi binafsi na seikalini, ma-lecture waalipwe fedha zao tena na fidia juu.

Wanafunzi wa SEKOMU wakiandamana kesho na kesho kutwa wanatumiwa defender za FFU bila hata kuwasikiliza kwa nini walikuwa au wameandamana, kundi la watu haliwezi kuandamana bila sababu maana sio kundi la vichaa au wenda wa zimu lazima serikali ikubali kusikiliza sauti za wananchi wake bila kujali itkadi ya aina yoyote.

Chuoni kuna mgomo wa chini chini, staff ipo kwenye mgomo baridi. Mgomo huo unaathiri wanafunzi bila hatia yoyote.


MTANZANIA AWE AMESOMA AU HAJASOMA BADO ATAENDELEA KUWA MTUMWA.
HII INATHIBITISHWA NA STAFF YA SEKOMU.
 

Attachments

  • SEKOMU.png
    SEKOMU.png
    9 KB · Views: 107
Aisee poleeni sana. Mimi nime-graduate hapo 2015, Chuo hicho kinaendesha kibabe sana na wanajiamini kweli. Sijui kwa nini? Nakumbuka sisi tuliletewa defender hapo tukidai hela yetu halali ya tahadhari... Dah.
Ndo siku hiyo nilikichukia chuo hicho..hata kama wangetangaza kusoma bure siwezi.
Poleni sana!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom