Kuna mahusiano gani kati ya ujio wa Lowassa na ukimya wa wabunge vijana machachari upinzani?

gimmy's

JF-Expert Member
Sep 22, 2011
3,311
3,341
Siasa kwa upande wa wabunge wengi vijana wenye umachachari mkubwa kutoka Chadema wameonekana kua kimya sana mara tu Lowasa alipo hamia upinzani. Kwangu inanipa maswali mengi yasio na majibu hasa ninapotizama siasa za wabunge kama Mnyika,Lema na wengineo.

Mnyika alionesha utofauti mapema kabisa wakati wakumkaribisha Lowasa.Ilichukua muda kidogo kuonekana kundini hata watu wakaanza kuuliza humu mitandaoni wapi alipo Mbunge huyu machachari.Lakini hata baada yakujiunga kundini ile hamasa tunayoijua kwake haipo kabisa.Nasema hili kwani Mh Mnyika anafahamika vizuri juu ya uwezo wake wa ushawishi nakujenga hoja.

Imenilazimu kuhoji na kuhusianisha taswira hii na ujio wa Lowasa kwani kabla ya Lowasa kuhamia upinzani hii hali haikua kwa kiwango hiki.
Tizama mbunge kama Lisu kwa sasa ni ngumu sana kupata matukio yoyote kutoka kwake si mtandaoni,radioni ama Luningani.Ni nadra sana kupata taafifa zake.

Nahoji kwasababu natambua mchango wa wabunge hawa kwa Taifa.Natambua kelele zao hua zinafaida mkubwa kwa serikali.Na hii ndio dhana ya upinzani. Kwa sasa tunaona upinzani umepwaya kwa kiwango kikubwa kiasi ambacho inatia shaka chanzo ni nini. Mbunge pekee ambaye hajatetereka ni ZZK na natumai tutakubaliana sote katika hili.

Je ni ujio wa Lowasa ama Tanzania imepata raisi mchapakazi kiasi ya kwamba wabunge hawa wamekosa kabisa hoja?
 
Hata sijui unahoji kitu gani. Mtu unapokumbwa na gonjwa baya, machachari yatakuwa ni yale yale kama ulipokuwa na afya timamu? Haiwezekani. Ndicho kilichowasibu vijana machachari wa cdm chini ya Dr. Slaa ambae yuko Canada akiugulia taratibu. Kazi yake ya miaka mingi ya kuwafunda hao vijana imekuwa zero.
Kwa msemo mwingine twaweza sema roho zinawasuta.
 
Lowassa anaendelea na kazi yake mdogo mdogo mpaka ifike 2020 kama watakuwa hawajamwelewa basi upinzani utasalia historia kabisa, no more opposition.
 
Hata ungekuwa wewe usingekuwa na sauti mbili kwa mtu mmoja. Lazima uwe kama Lissu, Kubenea na Mbowe.

Ni aibu kwa upinzani na ni kovu kubwa.
 
Lowasa naona tangu ashike hatamu,chadema kawamaliza kabisa,hakuna harakati zozote mie naona,zaidi ya kusikiliza ya majukwani tu,kwa ufupi kwishneee
 
Dawa ni kumtimua. Swali ni nani wa kimvisha mwenzie kengele? Wanatia huruma. Na kwa sasa upande wa pili wanatumia hiyo nafasi kuwamaliza. Mtaji wao ulikuwa sympath ya wananchi ambao kwa sasa hawana habare. Wameshawasoma wamegundua hawasomeki. Watu walifikia kusema kwenye siasa uongo humo nani atawaamini tena. Tunasubiri chama kipya cha upinzani. Meanwhile tunaendelea na chama kimoja
 
Dawa ni kumtimua. Swali ni nani wa kimvisha mwenzie kengele? Wanatia huruma. Na kwa sasa upande wa pili wanatumia hiyo nafasi kuwamaliza. Mtaji wao ulikuwa sympath ya wananchi ambao kwa sasa hawana habare. Wameshawasoma wamegundua hawasomeki. Watu walifikia kusema kwenye siasa uongo humo nani atawaamini tena. Tunasubiri chama kipya cha upinzani. Meanwhile tunaendelea na chama kimoja
We we we we weee wamtimue nani. Labda waondoke wao. Ila tukisimamia ukweli hawa vijana wa upinzani hawaoneshi tena zile harakati za ukombozi.
 
Dawa ni kumtimua. Swali ni nani wa kimvisha mwenzie kengele? Wanatia huruma. Na kwa sasa upande wa pili wanatumia hiyo nafasi kuwamaliza. Mtaji wao ulikuwa sympath ya wananchi ambao kwa sasa hawana habare. Wameshawasoma wamegundua hawasomeki. Watu walifikia kusema kwenye siasa uongo humo nani atawaamini tena. Tunasubiri chama kipya cha upinzani. Meanwhile tunaendelea na chama kimoja
pesa zake atalipa nani, labda wakubali aondoke na ruzuku yote ya chama iwe inaingia kwenye account yake hapo atawaelewa
 
Kiukweli tukiacha maneno ya kinafki Mnyika kawa mpole sana simsemi vibaya ila dah Mnyika kama unaona hili faham inabidi ufanye jitihada kidogo.
 
Kama hata ambao hawakukutana barabarani huachana sijui inakuwaje kwa waliokutana barabarani? Ujio wa EL kwa kweli kwa mimi ninae angalia toka nje (ya chama) sijajua kama imekuwa ni asset au liability-kwa muda mfupi, wa kati na mrefu. Ujio huu una effect gani kwa nyota waliokuwa wanachipukia CDM na kwa jinsi CDM wanavyo endesha siasa zao? CDM wenyewe wataamua wanaelekea wapi. Bahati mbaya mjomba nae kaamua kuwawekea wenzake wingu zito-anapiga siasa pekeyake. Baada ya kujiuliza yote hayo-nawatakia UKAWA mafanikio ili waweze kukabiliana na giza linalozidi kutanda nchini.
 
Kiukweli tukiacha maneno ya kinafki Mnyika kawa mpole sana simsemi vibaya ila dah Mnyika kama unaona hili faham inabidi ufanye jitihada kidogo.
Afadhali mkuu wewe umeliona hili...HAPA KUNA TATIZO SI BURE...hii inaonyesha kabsa kUNA TATZO
 
wamechoka sana, hawana tena sauti na wamekuwa watumishi wa kumdekia kamanda mfuga ng'ombe
 
Siasa kwa upande wa wabunge wengi vijana wenye umachachari mkubwa kutoka Chadema wameonekana kua kimya sana mara tu Lowasa alipo hamia upinzani. Kwangu inanipa maswali mengi yasio na majibu hasa ninapotizama siasa za wabunge kama Mnyika,Lema na wengineo.

Mnyika alionesha utofauti mapema kabisa wakati wakumkaribisha Lowasa.Ilichukua muda kidogo kuonekana kundini hata watu wakaanza kuuliza humu mitandaoni wapi alipo Mbunge huyu machachari.Lakini hata baada yakujiunga kundini ile hamasa tunayoijua kwake haipo kabisa.Nasema hili kwani Mh Mnyika anafahamika vizuri juu ya uwezo wake wa ushawishi nakujenga hoja.

Imenilazimu kuhoji na kuhusianisha taswira hii na ujio wa Lowasa kwani kabla ya Lowasa kuhamia upinzani hii hali haikua kwa kiwango hiki.
Tizama mbunge kama Lisu kwa sasa ni ngumu sana kupata matukio yoyote kutoka kwake si mtandaoni,radioni ama Luningani.Ni nadra sana kupata taafifa zake.

Nahoji kwasababu natambua mchango wa wabunge hawa kwa Taifa.Natambua kelele zao hua zinafaida mkubwa kwa serikali.Na hii ndio dhana ya upinzani. Kwa sasa tunaona upinzani umepwaya kwa kiwango kikubwa kiasi ambacho inatia shaka chanzo ni nini. Mbunge pekee ambaye hajatetereka ni ZZK na natumai tutakubaliana sote katika hili.

Je ni ujio wa Lowasa ama Tanzania imepata raisi mchapakazi kiasi ya kwamba wabunge hawa wamekosa kabisa hoja?
sababu ni kama ifuatavyo
1.bunge halionyeshwi
2.mikutano ya vyama marufuku
3. wabunge wa upinzani marufuku kuongea bungeni
4. wabunge wenye hoja fukuza bungeni
 
Lowasa naona tangu ashike hatamu,chadema kawamaliza kabisa,hakuna harakati zozote mie naona,zaidi ya kusikiliza ya majukwani tu,kwa ufupi kwishneee


lowasa alipokaribishwa ukawa... wazi nilijua anaenda kuua upinzani.

wapinzani wa kweli hawawez kuwa mamluki.
 
Naona tayari umeanzishwa uzi unaooneshea kidole mbunge fulani machachari wa upinzani mwenye mpango wakung'atuka japo haujataja jina lakini umeweza kutoa taswira juu ya mbunge huyo.
 
Mapambano bado yanaendelea hata iweje. Wenye kusema wacha waseme, wenye kutoka wacha watoke, siku si nyingi zijazo Mungu anakwenda kuikumbuka Tanzania. Huu unaofanywa na the so called awamu ya tano ni usanii tu ambao huwa haudumu. Ukombozi wa kweli unakuja Watanzania tusife moyo.
 
Siasa kwa upande wa wabunge wengi vijana wenye umachachari mkubwa kutoka Chadema wameonekana kua kimya sana mara tu Lowasa alipo hamia upinzani. Kwangu inanipa maswali mengi yasio na majibu hasa ninapotizama siasa za wabunge kama Mnyika,Lema na wengineo.

Mnyika alionesha utofauti mapema kabisa wakati wakumkaribisha Lowasa.Ilichukua muda kidogo kuonekana kundini hata watu wakaanza kuuliza humu mitandaoni wapi alipo Mbunge huyu machachari.Lakini hata baada yakujiunga kundini ile hamasa tunayoijua kwake haipo kabisa.Nasema hili kwani Mh Mnyika anafahamika vizuri juu ya uwezo wake wa ushawishi nakujenga hoja.

Imenilazimu kuhoji na kuhusianisha taswira hii na ujio wa Lowasa kwani kabla ya Lowasa kuhamia upinzani hii hali haikua kwa kiwango hiki.
Tizama mbunge kama Lisu kwa sasa ni ngumu sana kupata matukio yoyote kutoka kwake si mtandaoni,radioni ama Luningani.Ni nadra sana kupata taafifa zake.

Nahoji kwasababu natambua mchango wa wabunge hawa kwa Taifa.Natambua kelele zao hua zinafaida mkubwa kwa serikali.Na hii ndio dhana ya upinzani. Kwa sasa tunaona upinzani umepwaya kwa kiwango kikubwa kiasi ambacho inatia shaka chanzo ni nini. Mbunge pekee ambaye hajatetereka ni ZZK na natumai tutakubaliana sote katika hili.

Je ni ujio wa Lowasa ama Tanzania imepata raisi mchapakazi kiasi ya kwamba wabunge hawa wamekosa kabisa hoja?
Watu wamenyanyasika Bungeni na Tulia wewe unasema kitu tofauti
 
Back
Top Bottom