Edward A Chapa
JF-Expert Member
- Sep 3, 2014
- 973
- 1,394
Habari ndugu wana JamiiForums samahani nilikuwa nauliza kuna sehemu naweza kupata huduma ya Western union ambayo inakesha 24 hours kwa hapa Dar es salaam ni maeneo gani?
Mmmmh...sidhani...huduma nyingi za kifedha (hususan kwa tanzania) huwa hazikeshi...
Jaribu JK Nyerere airport, kuna mtu aliwahi kwenda kuchukua kule siku ya sikukuu au weekend kama sikosei.
Hapo inabidi usubiri jmosi
Ngoja Nitajaribu airport
Hii huduma ilitakiws iwepo 24/7 kwani ipo Globally na tumepishana masaa na pia holidays hivyo wanapofunga huku kwetu kuwa ni usiku wakati kwa wenzetu ni mchana wanakosea
Ama wanafunga kwa kuwa kwetu ni Muungano wakati wenzetu wapo kazini sio sawa
Uganda ipo huduma Hiyo nakumbuka mwaka 2010 niliwai toa pesa saa 9 usiku
Lakini Tanzania nadhani hakuna jana nimezunguuka usiku mpaka saa 7 sijapata Western union
Tanzania hakuna
Asante kwa kunifahamisha, ila daah kuna pesa nimetumiwa kwa Western union na kesho Holiday sijui itakuwaje.
Nenda benki ya Posta katika matawi yafuatayo, Ubungo plaza, samora katikati ya jiji au kariakoo utapata huduma hiyo.
Next time mwambie aliyekutumia atumie mobile transfer....western union unaweza tumia option ya kumtumia mtu from abroad via voda m-pesa.