Kuna Athari Kuzima Gari Kwenye Foleni

Marumeso

JF-Expert Member
Oct 3, 2009
1,410
1,313
Wakuu. Kutokana na mlolongo wa foleni barabarani kuna wakati najikuta nasimama foleni kwa muda mrefu huku injini ya gari ikiunguruma.

Kutokana na hali hii kuna wakati nashawishika kuzima gari ili 'kuokoa' wese.

Je hii zima washa ya gari haina madhara kwenye gari wakuu.
 
Kwa ushauri wa haraka, rudi uanze kumiliki bodaboda, gari sio size yako. Hukuwa umejiandaa kumiliki gari au utakuwa miongoni mwa walioongwa magari.
duuh mkuu. nimehongwa tena? we kiboko!
 
Wakuu. Kutokana na mlolongo wa foleni barabarani kuna wakati najikuta nasimama foleni kwa muda mrefu huku injini ya gari ikiunguruma.

Kutokana na hali hii kuna wakati nashawishika kuzima gari ili 'kuokoa' wese.

Je hii zima washa ya gari haina madhara kwenye gari wakuu.
Kwa upande wangu naweza kusema ndio kunaweza kuwa na hatari au laa.

Inategemeana aina ya gari na unalizima kwa hali gani.

Mfano gari yenye turbo na haijafungwa turbo timer au haina kabisa usifanye hivyo.

Hata kama gari haina turbo usiizime kwa gafla.mfano umetoka nayo huko speed wangu wangu unafika tuu kwenye foleni nakuizima sio vizuri au ukitaka iache kwanza silensa kwa mda kidogo then ndio uizime
 
Back
Top Bottom