Kuna aina za simu ukiwa unatumia unaweza kukosa vitu vingi

Leo kuna Mwanamke nimekutana naye kituo cha daladala kimsingi nikatokea kuvutiwa naye pamoja na udomozege wangu nikasema leo lazima nifunguke bila ya kujali circumstances ambazo ningekutana nazo.

Picha linaanza kwa salamu mrembo karespond vizuri nikaanza zile stori za changomoto za usafiri wa Dar es Salaam naye akachangia kero zake kiukweli zilikuwa ni conversation fupi zilizokuwa na tija.

Ikafika wakati nikaomba namba ya simu ndio hapo nikawakumbuka wote waliowahi kusema kuna simu na calculator.

Mrembo yupo tayari kutoa nambari za simu lakini simu yangu haipo tayari.

Kwanza nilikuwa nimepunguza mwanga wa screen sasa lile jua la saa sita likafanya nisione chochote kwenye display nikawa naotea sehemu ya kuongeza mwanga kwa tabu sana nikafanikisha kuongeza mwanga.

Nikatoa pattern fresh nikatouch calls ili niweze kunakili namba nayo calls inagoma kurespond natouch back naona inafunguka opera mini nikaona simu ishaniumbua ngoja nirudi analog nataka kutafuta pen na karatasi kwenye kibegi ghafla daladala ambayo alikuwa akiisubiri kwa muda mrefu ishafika kituoni akaniambia next time mrembo kapanda zake gari huyo kasepa zake.

Ilikuwa ni heartbreaking moments wakuu, nipo napambana na mimi nimiliki simu mwaka huu.
simu la mchina
 
Back
Top Bottom