Kumekucha Zimbabwe...

Nachukia magaidi,wachonganishi, na matapeli wa maneno.

Mkuu magaidi si ndo wale nchini kwetu wanatoa kucha na meno kwa raia wasema kweli? Vilevile taasisi yao ya poliCCM wanapiga bomu raia?
 
Mugabe mkuu wa nchi tangu 1980? nusu ya vijana wamekuwa wakimbizi South,uchumi alioachiwa ni less than 20% ya aliopewa na wakoloni etc then huyu ni hero? kweli tunafikiria na kuona tofauti
 
Hawa ni viongozi wachache waliobaki hapa Afrika ambao wana uwezo wa kuongea mambo bila unafiki.Bravo Mugabe kiboko ya Tony Blair.
 
Mugabe mkuu wa nchi tangu 1980? nusu ya vijana wamekuwa wakimbizi South,uchumi alioachiwa ni less than 20% ya aliopewa na wakoloni etc then huyu ni hero? kweli tunafikiria na kuona tofauti


Ni kweli mkuu unayosema lakini akija mzalendo ataongoza nchi lakini sio kumpa yule Morgan ambaye puppet kafanana na mkuu wetu wa kaya kasoro yeye hajaruhusu ndoa tu za jinsia moja.
 
Sikujua na madikteta kama Mugabe wanaungwa mkono na wengi!
 
Ni kweli mkuu unayosema lakini akija mzalendo ataongoza nchi lakini sio kumpa yule Morgan ambaye puppet kafanana na mkuu wetu wa kaya kasoro yeye hajaruhusu ndoa tu za jinsia moja.
Kubali tuu Bob nchi imemshinda ile tuache siasa au uzalendo wa rangi tuu,miaka 33 mkuu wa nchi bado mnakuja na excuses tuu?vipi na under Mugabe millions of Zimbabwean end up refugees in South? explain it to me au ni mzungu ndio kafanya hivyo?
 
Kubali tuu Bob nchi imemshinda ile tuache siasa au uzalendo wa rangi tuu,miaka 33 mkuu wa nchi bado mnakuja na excuses tuu?vipi na under Mugabe millions of Zimbabwean end up refugees in South? explain it to me au ni mzungu ndio kafanya hivyo?


Wanakuwa refugees because of economic sanctions na wala sio vita, na hii ni kutokana na kutetea maslahi ya wanyonge. Kwani leo hii Mugabe angesema awakumbatie Whiteman na kuwa puppet kama mkuu wako angepungukiwa nini?
 

Nahisi huelelewi hata kidogo kiini cha mgogoro wa Zimbabwe..........kumbuka huwezi ukawa hakimu na muda huo huo ni mwendesha mashtaka..............ni kuulize je unatambua kabla Zimbabwe haijapata uhuru walikubaliana nini na MALIKIA(UK)??????????? Je waliyokubaliaana Waingereza waliyatakeleza?????...ni ukajijengea tabia ya kusoma na kuelewa kabla ya kuropoka????...wewe unaona ni ufahari kusaidiwa chakuala???Na Unahisi MDC inaweaza ku solve matatizo ya ZImbabwe????kwa taarifa yako MDC ni pandikizi la Waingereza na washirika wake na hawana agenda yoyote inayoweza leta mabadiliko dhabiti Zimbabwe........

kama unaona nipiga propaganda hapa ntashukuru ukaniprove me wrong kwa fact, naizungumzia Zimbabwe nayoijui tena saana.....Namjua Morgan Richard Tsvangirai na narudia tena ni pandikizi la Mangaribi na hana agenda yoyote kwa Wazimbabwe.....
 


Uzuri na friends toka Zim.
Nazungumzia njaa ya Zim.Wazungu hawakuhama na mashamba.Yako yameota mbuga.
Lancaster agreement kila msomi anajua.

Economic sanctions sio sanctions unazofikiria.Ni target kwa elites wa Mugabe ambao walishiriki kwenye torture.

Huyu huyu Mugabe aliua yapata 20,000 watu wa Matabeleland.
Usimtetee huyu dikteta kwa kuwa ni mweusi mwenzetu
 
Miaka 33 in power?wakimbizi,umaskini na vurugu ndio vimeongezeka Zimbabwe lakini bado mnamtetea na visingizio kibao,huyu jamaa ndio tatizo Zimbabwe naamini...he must go!!
 
uchwara,

..sasa mbona Malawi napo kulikuwa na njaa?

..tukubali tu kwamba nchi za magharibi walitaka kufanya "regime change" hapo Zimbabwe lakini wakashindwa.

..Mugabe angekuwa keshaondoka kama siyo watu wa west kujaribu kumuondoa baada ya kumdhalilisha.

..wakati anaua Wandebele nchi za magharibi zilikaa kimya kwasababu Mugabe kipindi hicho alikuwa mwema kwa wale wazungu walowezi. tena waliendelea kumtunukia madegree kibao toka Cambridge, na hata kumpa hadhi ya Knight commander of the order of the Bath na Malkia Elizabeth.

..hata Congo, Kagame ameua mamilioni ya wananchi wa Congo akipewa msaada wa kifedha toka WB na IMF, na silaha toka nchi za magharibi. Zimbabwe/Mugabe waliokuwa wakijaribu kuwatetea Wacongo wakiwekewa vikwazo vya uchumi na silaha.

cc: Prodigal Son
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…