Tetesi: Kumekucha: Simba mivurugano bado inaendelea

Labani og

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2020
Posts
22,854
Reaction score
32,657
"Kwa taarifa zilizonazo Kutoka ndani tajiri anafanya Pressing sana huko.

Anataka Kabla hajatoa Pesa ya Usajili Msimu huu Kwanza ile Bilion 67 irekodiwe na itambulike rasmi Kama ni Mkopo anaidai Simba Sports

Baada ya hapo waje Kwenye Pesa ya usajili ambayo ameahidi Juzi Kwamba atafanya Usajili Babu Kubwa nayo anataka irekodiwe na itambulike Kama Deni anawadai Simba Simba Sports.

Taarifa hii imetumwa Kwa wajumbe wote wa Bodi, Kama hamjatambua hela ninayotoa Kama Deni hakuna Pesa ya Usajili itatoka.

Na Kwa Mujibu wa taarifa shida haipo Kwa Kamati ya Fedha na Ukaguzi Kwenye Kutambua haya Madeni.

Shida inaonekana Kwa tajiri yeye Kutaka atumie hela tu halafu Klabu iidhinishe Kama Deni bila ya Kufanyika Ukaguzi.Hapa ndo Kuna Mechi.

Kwa Mfano tajiri anasema ametumia Bil 8 Kwenye Usajili msimu uliopita kwa wachezaji 17 wapya.

Baadhi ya Wajumbe wanataka Kuonyeshwa tulifikaje hapa Kwenye hizi Bil 8 Kwa Usajili wa Kina Omary Omary, Jean Charles Ahoua na wengine?
Taarifa zinasema Pamoja na Kuwepo na Kamati ya Ukaguzi ya ndani Simba Sports wameleta Mkaguzi Mwingine wa nje lakini inasemwa bado tajiri hajaonyesha ushirikiano.

Wingu zito bado limetanda Simba Sports, na hii itakuwa Disappointment Kubwa Kwa Fadlu Davids.

Na Kwa binafsi Yangu naona Kama Simba Sports ikijipanga vizuri sasa hivi wana uwezo wa Kusajili bila MO

Tatizo lipo Kwa hii short notes inawezekanaje? Kuna Sajili nyingi Simba wameshindwa Kuzikamilisha Kwa wakati Kwasababau ya hizi Sintofahamu zinazoendelea.

Tajiri huku nje anasema usajili mkubwa unaenda Kufanyika lakini Kumbe ndani bado una masharti kibao."

Ameandika Mchambuzi Wilson Oruma kupitia ukurasa wake wa Instagram

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
NO REFORMS, NO ELECTION.
 
Makolo ni masikini wa kushinda mechi za dabi,

Na pia ni masikini wa makombe,

Na kubwa zaidi ni masikini wa viongozi,

Chanzo cha yote kwa kuwa makolo wote ni;
"MBUMBUMBU".
 
Dewji ni tapeli sana; huenda ndiyo maana ni tajiri kwa vile anatapeli wengi kujilimbikizia mali mwenyewe.
 
Ramli kama hizi tumezizoe. Lakini ujue Simba ipo juzi, jana, leo, kesho na keshokutwa. Na MO yupo Simba juzi, jana, leo, kesho na keshokutwa! Bila kukusahau na wewe upo juzi, jana, leo, kesho na keshokutwa na nyuzi zako zipo juzi, jana, leo, kesho na keshokutwa! Ahahahahaha!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…