Kumbukumbu yangu ya uhuru wa Tanganyika

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,913
30,255
1544373927339.png




Kitabu hicho hapo juu ni moja ya vitabu katika mradi wa Oxford University Press (OUP) wa kufundisha wanafunzi wa shule za msingi lugha ya Kiingereza lakini pia wakati huo huo kuwafundisha wanafunzi hao historia za nchi zao.

Mradi huu ulichapa vitabu takriban 15 kutoka Afrika ya Mashariki lakini hapakuwa na kitabu chochote kutoka Tanzania. Ndipo OUP waliponiomba niandike kitabu katika mradi huu kwa ajiii ya Tanzania.

Kitabu hiki kilichapwa mwaka wa 2007 na hadi sasa kimeshachapwa mara mbili.

Bahati mbaya sana kitabu hiki hakikutiwa katika mtaala wa Tanzania ingawa OUP wamewafahamisha Wizara ya Elimu kuwa ni kitabu kizuri kitakachowasaidia wanafunzi kusoma Kiingereza na kujua historia ya uhuru wa Tanganyika.

Baada ya kushindwa kuingizwa kitabu hiki katika mtaala OUP walisimamisha kuchapa mswada wangu wa kitabu kuhusu Zanzibar, ''The School Trip to Zanzibar.''

OXFORD UNIVERSITY PRESS WATOA TOLEO LA PILI LA "THE TORCH ON KILIMANJARO" KITABU CHA WATOTO CHA MWANDISHI MOHAMED SAID

1544374305201.png
 
View attachment 961956



Kitabu hicho hapo juu ni moja ya vitabu katika mradi wa Oxford University Press (OUP) wa kufundisha wanafunzi wa shule za msingi lugha ya Kiingereza lakini pia wakati huo huo kuwafundisha wanafunzi hao historia za nchi zao.

Mradi huu ulichapa vitabu takriban 15 kutoka Afrika ya Mashariki lakini hapakuwa na kitabu chochote kutoka Tanzania. Ndipo OUP waliponiomba niandike kitabu katika mradi huu kwa ajiii ya Tanzania.

Kitabu hiki kilichapwa mwaka wa 2007 na hadi sasa kimeshachapwa mara mbili.

Bahati mbaya sana kitabu hiki hakikutiwa katika mtaala wa Tanzania ingawa OUP wamewafahamisha Wizara ya Elimu kuwa ni kitabu kizuri kitakachowasaidia wanafunzi kusoma Kiingereza na kujua historia ya uhuru wa Tanganyika.

Baada ya kushindwa kuingizwa kitabu hiki katika mtaala OUP walisimamisha kuchapa mswada wangu wa kitabu kuhusu Zanzibar, ''The School Trip to Zanzibar.''

OXFORD UNIVERSITY PRESS WATOA TOLEO LA PILI LA "THE TORCH ON KILIMANJARO" KITABU CHA WATOTO CHA MWANDISHI MOHAMED SAID

View attachment 961962
Nina uhakika humo ndani Sykes brothers wametajwa.Ila akina Patrick Kunambi na John Rupia sidhani kama wamekumbukwa.
 
Nina uhakika humo ndani Sykes brothers wametajwa.Ila akina Patrick Kunambi na John Rupia sidhani kama wamekumbukwa.
Sun...
Unapotaka kuzungumza kitu ni bora kwanza ukakijua kwani ikiwa utajiandikia tu
huku somo lenyewe hulijui unajiweka wazi kwa watu kukulaumu.

The Torch on Kilimanjaro nimueleza Mwalimu Julius Nyerere peke yake huwezi
kumkuta Abdul Sykes.

Lakini nina wajibu wa kukufahamisha kuwa ikiwa ni historia ya uhuru wa Tanganyika
na TANU au historia ya Nyerere mwenyewe ni tabu sana tena sana kuwakwepa
Sykes brothers.

Chuo Cha Kivukono katika kitabu chao, Historia ya Chama Cha TANU wamejaribu na
matokeo yake ndiyo haya wewe unawataja hapa kwa nini wanatajwa sana.

Sasa nakuja katika historia ya TANU na kudai uhuru.
Nakuomba usome hapo chini kutoka kitabu cha Abdul Sykes:

''...mkutano huo wa muhimu katika historia ya kudai uhuru wa Tanganyika ulifanyika miezi sita tu baada ya Nyerere kuchukua ofisi kama rais wa TAA. Tarehe 29 Oktoba, ujumbe wa TAA ukiwa na Mmanyema na mtunga mashairi, kiongozi mashuhuri kutoka Jimbo la Ziwa, Abdu Kandoro, Chifu Patrick Kunambi kutoka Morogoro, Jimbo la Mashariki, Japhet Kirilo, Joseph Kimalando, John Rupia na Julius Nyerere, walikutana katika Government House kujadili ile sekula ya serikali na Gavana Edward Twining...''​
''...jibu la Twining kwa ujumbe wa TAA juu ya ile sekulla lilitabiriwa na hoja ya kupinga iliyotayarishwa wajumbe walipokutana katika makao makuu ya TAA kupanga maneno ya kusema mbele ya Gavana. Kunambi aliyekuwa msemaji wa ule ujumbe wa TAA alimwambia Twining; ‘’Je, unajua kitakachotokea bwana mkubwa, ikiwa, kwa mfano serikali itapitisha sheria kuwapiga marufuku madereva wote wenye ujuzi wasiendeshe magari ikawataka wasalimishe leseni zao za udereva na kuyaacha magari yao yaendeshwe na madereva wasio na ujuzi?''​
''...joto la siasa lilikuwa katika kiwango kama hiki wakati wajumbe kumi na saba wa TAA kutoka kwenye matawi majimboni na makao makuu walipokutana mjini Dar es Salaam tarehe 7 Julai, 1954, kujadili katiba mpya ya chama kipya cha siasa - TANU. Jimbo la Mashariki ambalo lilikuwa na wajumbe wengi kushinda yote liliwakilishwa na, ndugu wawili Abulwahid na Ally Sykes, Dossa Aziz, Tewa Said Tewa, Patrick Kunambi, Kasella Bantu, John Rupia, Julius Nyerere na C. O. Milinga; Jimbo la Kaskazini liliwakilishwa na na Joseph Kimalando na Japhet Kirilo; Jimbo la Ziwa liliwakilishwa na Abubakar Kilanga, L. M. Makaranga.''​
 
Sun...
Unapotaka kuzungumza kitu ni bora kwanza ukakijua kwani ikiwa utajiandikia tu
huku somo lenyewe hulijui unajiweka wazi kwa watu kukulaumu.

The Torch on Kilimanjaro nimueleza Mwalimu Julius Nyerere peke yake huwezi
kumkuta Abdul Sykes.

Lakini nina wajibu wa kukufahamisha kuwa ikiwa ni historia ya uhuru wa Tanganyika
na TANU au historia ya Nyerere mwenyewe ni tabu sana tena sana kuwakwepa
Sykes brothers.

Chuo Cha Kivukono katika kitabu chao, Historia ya Chama Cha TANU wamejaribu na
matokeo yake ndiyo haya wewe unawataja hapa kwa nini wanatajwa sana.

Sasa nakuja katika historia ya TANU na kudai uhuru.
Nakuomba usome hapo chini kutoka kitabu cha Abdul Sykes:

''...mkutano huo wa muhimu katika historia ya kudai uhuru wa Tanganyika ulifanyika miezi sita tu baada ya Nyerere kuchukua ofisi kama rais wa TAA. Tarehe 29 Oktoba, ujumbe wa TAA ukiwa na Mmanyema na mtunga mashairi, kiongozi mashuhuri kutoka Jimbo la Ziwa, Abdu Kandoro, Chifu Patrick Kunambi kutoka Morogoro, Jimbo la Mashariki, Japhet Kirilo, Joseph Kimalando, John Rupia na Julius Nyerere, walikutana katika Government House kujadili ile sekula ya serikali na Gavana Edward Twining...''​
''...jibu la Twining kwa ujumbe wa TAA juu ya ile sekulla lilitabiriwa na hoja ya kupinga iliyotayarishwa wajumbe walipokutana katika makao makuu ya TAA kupanga maneno ya kusema mbele ya Gavana. Kunambi aliyekuwa msemaji wa ule ujumbe wa TAA alimwambia Twining; ‘’Je, unajua kitakachotokea bwana mkubwa, ikiwa, kwa mfano serikali itapitisha sheria kuwapiga marufuku madereva wote wenye ujuzi wasiendeshe magari ikawataka wasalimishe leseni zao za udereva na kuyaacha magari yao yaendeshwe na madereva wasio na ujuzi?''​
''...joto la siasa lilikuwa katika kiwango kama hiki wakati wajumbe kumi na saba wa TAA kutoka kwenye matawi majimboni na makao makuu walipokutana mjini Dar es Salaam tarehe 7 Julai, 1954, kujadili katiba mpya ya chama kipya cha siasa - TANU. Jimbo la Mashariki ambalo lilikuwa na wajumbe wengi kushinda yote liliwakilishwa na, ndugu wawili Abulwahid na Ally Sykes, Dossa Aziz, Tewa Said Tewa, Patrick Kunambi, Kasella Bantu, John Rupia, Julius Nyerere na C. O. Milinga; Jimbo la Kaskazini liliwakilishwa na na Joseph Kimalando na Japhet Kirilo; Jimbo la Ziwa liliwakilishwa na Abubakar Kilanga, L. M. Makaranga.''​
👏 Nimekuelewa Mzee wangu.Sasa nami natamani nikipate kitabu hicho,na ni vyema ukafanya utaratibu ili nasi wa mikoani tukipate.
 
👏 Nimekuelewa Mzee wangu.Sasa nami natamani nikipate kitabu hicho,na ni vyema ukafanya utaratibu ili nasi wa mikoani tukipate.
Sun...
Bahati mbaya wasambazaji wa vitabu wanaangalia Dar es Salaam tu.
Mimi ni mwandishi tu sina kauli wapi kitabu kinapekekwa kuuzwa.

Ningependa kitabu hiki kiwepo kila mahali.
 
Mohammed Saidi unazungumziaje hali ya sasa inayoendelea ambapo tunaona teuzi nyingi zinazofanyika waislamu wanateuliwa wachache sana katika nyadhifa mbalimbali kulinganisha na Wakiristo. Je hoja kuwa Waislamu waliosoma na wenye vigezo ni wachache sana ni kweli?

Swali la pili, kwa jinsi unavyoona hali, Je unadhani Waislamu wa Tanganyika na baadae Tanzania wamepata fursa sawa bila ubaguzi ya kufaidi matunda ya uhuru ambao wazee wao walioupigania kwa jasho na damu kama raia wengine wasio waislamu?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom