Kumbukizi ya marehemu Edward Moringe Sokoine

Kumbukizi ya marehemu Edward Moringe Sokoine

Papaa Muu

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2018
Posts
243
Reaction score
292
Tarehe na Mwezi kama Leo ya Mwaka 1984, Taifa lilipatwa na majonzi makubwa. Jioni saa 11 kulisambaa taarifa kuwa Waziri Mkuu wa wakati huo Edward Moringe Sokoine amepata ajali na kufariki dunia katika eneo la Dakawa akitokea Dodoma.
_____________
Edward Moringe Sokoine alikuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa Mara ya Kwanza tarehe 13 Februari 1977 akiwa na miaka 38 tu( Alizaliwa August 1,1938). Ndio kusema alikuwa Waziri Mkuu akiwa kijana kwelikweli.

Anasifika kwa uadilifu na Uongozi makini huku nidhamu ikiwa Ndio msimamo wake hadi alipokutwa na Umauti kwenye ajali ya Gari tarehe 12 April 1984 katika eneo la Dakawa, Morogoro akitokea Dodoma.

Hayati Sokoine kama Kiongozi Mkubwa kijana hakuwa mtu wa kujilimbikizia Mali, Majivuno au dharau. Tunapoadhimisha miaka 35 tangu kifo chake, ni vema kutafakari jinsi gani Vijana tunaweza kuendelea kujitoa kwa nchi hii na sio maslahi ya mtu mmoja mmoja!
Kuweka kumbukumbu Sawa:
Hayati Edward M. Sokoine alihudumu kama Waziri Mkuu kuanzia Februari 13,1977 hadi Novemba 7,1980 kisha Februari 24, 1983 hadi 12 April 1984 alipofariki dunia. Hivyo alifariki akiwa na miaka 45 tu.
Kifo cha Sokoine kilimuumiza sana Baba wa Taifa, Mwl Julius K. Nyerere. Katika picha hiyo hapo chini, Mwalimu Nyerere akilia kwa uchungu mbele ya mwili wa Hayati Edward Moringe Sokoine.
https://www.facebook.com/FrancisDaudiTz/
Francis Daudi
Kaka Mkubwa!
12 April 2018.
1069879
 
Tarehe na Mwezi kama Leo ya Mwaka 1984, Taifa lilipatwa na majonzi makubwa. Jioni saa 11 kulisambaa taarifa kuwa Waziri Mkuu wa wakati huo Edward Moringe Sokoine amepata ajali na kufariki dunia katika eneo la Dakawa akitokea Dodoma.
_____________
Edward Moringe Sokoine alikuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa Mara ya Kwanza tarehe 13 Februari 1977 akiwa na miaka 38 tu( Alizaliwa August 1,1938). Ndio kusema alikuwa Waziri Mkuu akiwa kijana kwelikweli.

Anasifika kwa uadilifu na Uongozi makini huku nidhamu ikiwa Ndio msimamo wake hadi alipokutwa na Umauti kwenye ajali ya Gari tarehe 12 April 1984 katika eneo la Dakawa, Morogoro akitokea Dodoma.

Hayati Sokoine kama Kiongozi Mkubwa kijana hakuwa mtu wa kujilimbikizia Mali, Majivuno au dharau. Tunapoadhimisha miaka 35 tangu kifo chake, ni vema kutafakari jinsi gani Vijana tunaweza kuendelea kujitoa kwa nchi hii na sio maslahi ya mtu mmoja mmoja!
Kuweka kumbukumbu Sawa:
Hayati Edward M. Sokoine alihudumu kama Waziri Mkuu kuanzia Februari 13,1977 hadi Novemba 7,1980 kisha Februari 24, 1983 hadi 12 April 1984 alipofariki dunia. Hivyo alifariki akiwa na miaka 45 tu.
Kifo cha Sokoine kilimuumiza sana Baba wa Taifa, Mwl Julius K. Nyerere. Katika picha hiyo hapo chini, Mwalimu Nyerere akilia kwa uchungu mbele ya mwili wa Hayati Edward Moringe Sokoine.
https://www.facebook.com/FrancisDaudiTz/
Francis Daudi
Kaka Mkubwa!
12 April 2018.
View attachment 1069879
alikua htr sana
 
Kesi iliendwashwa kama traffic case na mahakama ilimuhuku Dube miaka mitatu jela kwa uzembe bila fine.
Wabunge walilamika. Lakini mwanasheria mkuu akawaeleza kuwa kwa wakati ule traffic case adhabu ya juu kabisa ilikuwa kifongo cha miaka mitatu. Na wakaambiwa sheria ikitungwa inamuhusu mtu yeyote Yule bila kujali wadhifa wake. Hatuwezi kubadili sheria eti kwa kuwa waziri mkuu amehusika ktk ajali. Nimemnukuu mwanasheria mkuu sikumbuki wakati ule alikuwa nani?
 
Kifo Cha Sokoine hata Mimi kiliniumiza ingawa nilikuwa kijana mdogo nilikuwa namkubali kupitia RTD sikuwahi kumuona uso kwa uso
 
Back
Top Bottom