Kumbe Zanzibar ndivyo ilivyo

Kumbe Zanzibar ndivyo ilivyo

tamimusalim

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2014
Posts
1,822
Reaction score
499
Nilikuwa sijawahi kufika Zanzibar. Ukweli nilikuwa nasikia mambo mengi na majina mengi kuhusu kisiwa hiki kama kisiwa cha marashi. Pia nilikuwa nasikia watu wakisifu uzuri wa kisiwa hiki, kwa upande fulani nilikuwa nasikia wanasiasa hasa wabunge toka Zanzibar wakilalamikia kuhusu kisiwa hiki kimaendeleo.

Ukweli ni kwamba, ukweli serikali ya Tanzania imekisahau kabisa kimaendeleo kisiwa hiki kwani hata miundombinu yake hasa barabara hairidhishi kabisa hasa barabara.

Ukweli zanzibar bado kabisa na ina tofauti kubwa na bara, hasa kimaendeleo. Pia Zanzibar bado ubaguzi upo dhidi ya wabara hili pia nililiona.

Naiomba serikali yetu ijaribu kuangalia Zanzibar kimaendeleo. Hata nyumba ya ghorofa 7 tu hamna zaidi ya jengo la BoT ambalo ndio inasemekana ndio refu Zanzibar.
 
Kwanza Umesema wanatubagua watu wa bara, papo hapo unataka serikali ya Tanzania ambayo kiuhalisia ni ya Tanganyika (bara) iwapelekee maendeleo watu ambao wanawabagua wabara? Tunajipendekeza kwa lipi hasa? Zanzibar itajengwa na Wazanzibar wenyewe kama wameisahau nchi yao, huo ni ujinga wao wenyewe. Hivi sasa Tanganyika ina mambo mengi ya msingi ya kufanya na si kuhangaika na nchi ambayo wananchi wake muda mwingi wamekaa vibarazani na maskani wakinywa kahawa name kuwasengenya Watanganyika.
 
Ya huko waachie wenyewe! ikiboreshwa haitavutia ile inapendeza hivyohivyo
 
Yani wazanzibar hawatupendi wabara kama nini..hebu waende huko mxiuuu hawana lolote hata wakitubagua.wenyewe njaa tuu
 
Kwanza Umesema wanatubagua watu wa bara, papo hapo unataka serikali ya Tanzania ambayo kiuhalisia ni ya Tanganyika (bara) iwapelekee maendeleo watu ambao wanawabagua wabara? Tunajipendekeza kwa lipi hasa? Zanzibar itajengwa na Wazanzibar wenyewe kama wameisahau nchi yao, huo ni ujinga wao wenyewe. Hivi sasa Tanganyika ina mambo mengi ya msingi ya kufanya na si kuhangaika na nchi ambayo wananchi wake muda mwingi wamekaa vibarazani na maskani wakinywa kahawa name kuwasengenya Watanganyika.

ha ha ha ha ha mkuu umetsha ha ha ha
 
Nahisi majengo marefu yapo kitaalamu zaidi kwamba hali halisi ya kisiwa haitawezekana. Nadhani watu wa ujenzi kama wapo watachangia kwa mtizamo huu. Lkn. tukumbuke maendeleo si majengo peke yake.
 
Back
Top Bottom