Mbunge wa Nzega aingia matatani
Fidelis Butahe
MBUNGE wa Jimbo la Nzega mkoani Tabora, Lucas Selelii amelaumiwa kwa kauli anazodaiwa kutamka kwamba kila mtu anayetaka ubunge akagombee kwao na kwamba, mgombea wa Jimbo la Nzega lazima awe mkristo ili kuepusha kuibua suala la Mahakama ya Kadhi.
Selelii alinadaiwa kusema kauli hizo alipozungumza na baadhi ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye hafla fupi aliyoiandaa baada ya kuwaita ili kubadilishana mawazo hivi karibuni na pia kwenye hafla ya siku ya wanawake duniani iliyofanyika mjini Nzega.
Alipoulizwa jana kwa njia ya simu, mbunge huyo alikiri kusema kwamba watu wa makabila mengine wanaotaka ubunge Nzega wasichaguliwe, lakini alikana kuzungumzia suala la udini.
Habari zilizolifikia Mwananchi kutoka kwa baadhi ya viongozi wa CCM mkoani Tabora zilisema, mbali na ukabila pia mbunge huyo alikuwa akiwashawishi watu mbalimbali kutokubali kumpigia kura mgombea ambaye sio muumini wa dhehebu la kikristo.
Mtoa habari wetu, alisema Selelii alidai wabunge wote waliokuwa wa Jimbo la Nzega walikuwa ni wenyeji wa mkoa huo, hivyo aliwataka wananchi wa wilaya hiyo kuhakikisha kuwa jimbo hilo halichukuliwi na mtu ambaye sio mwenyeji wa Tabora.
"Maneno hayo aliyazungumza wakati akiongea na viongozi mbalimbali wa CCM, ambapo pamoja na mambo mengine alitutaka tusikubali kumpitisha mtu ambaye sio mwenyeji wa mkoa wa Tabora ili miaka yote wabunge wa hapa Nzega wawe ni kabila la Wanyamwezi," walisema watoa habari hizo.
Walifafanua kuwa hivi karibuni katika sherehe za siku ya wanawake duniani ambazo kimkoa zilifanyika katika kanisa la AICC lililopo eneo la Kariakoo, Selelii alitoa fedha taslimu Sh 270,000 kuwasaidia wanawake hao.
Lakini anadaiwa kwamba katika hotuba yake kwa wanawake hao aliwataka pia kutomchagua mbunge Muislamu kwani ataliibua upya suala la Mahakama ya Kadhi kauli ambayo Selelii amekana kuitamka.
Akizungumza na Mwananchi, Selelii alisema yeye alitamka wazi kwamba hatakubali kuona Jimbo la Nzega likichukuliwa na mtu kutoka nje ya Mkoa wa Tabora, kwa sababu kila mtu anatakiwa akagombee sehemu ambayo ni mwenyeji.
"Suala la udini mimi sikulizungumza kabisa, huo ni uongo, mtu wa dini yeyote anaweza kugombea isipokuwa awe ni mwenyeji wa mkoa wa Tabora, kama sio mwenyeji wa Tabora labda ametokea Bukoba akagombee hukohuko Bukoba hapa Nzega watagombea Wanyamwezi tu kila mtu ana kwao bwana," alisema Selelii .
Source: Mwananchi News
Fidelis Butahe
MBUNGE wa Jimbo la Nzega mkoani Tabora, Lucas Selelii amelaumiwa kwa kauli anazodaiwa kutamka kwamba kila mtu anayetaka ubunge akagombee kwao na kwamba, mgombea wa Jimbo la Nzega lazima awe mkristo ili kuepusha kuibua suala la Mahakama ya Kadhi.
Selelii alinadaiwa kusema kauli hizo alipozungumza na baadhi ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye hafla fupi aliyoiandaa baada ya kuwaita ili kubadilishana mawazo hivi karibuni na pia kwenye hafla ya siku ya wanawake duniani iliyofanyika mjini Nzega.
Alipoulizwa jana kwa njia ya simu, mbunge huyo alikiri kusema kwamba watu wa makabila mengine wanaotaka ubunge Nzega wasichaguliwe, lakini alikana kuzungumzia suala la udini.
Habari zilizolifikia Mwananchi kutoka kwa baadhi ya viongozi wa CCM mkoani Tabora zilisema, mbali na ukabila pia mbunge huyo alikuwa akiwashawishi watu mbalimbali kutokubali kumpigia kura mgombea ambaye sio muumini wa dhehebu la kikristo.
Mtoa habari wetu, alisema Selelii alidai wabunge wote waliokuwa wa Jimbo la Nzega walikuwa ni wenyeji wa mkoa huo, hivyo aliwataka wananchi wa wilaya hiyo kuhakikisha kuwa jimbo hilo halichukuliwi na mtu ambaye sio mwenyeji wa Tabora.
"Maneno hayo aliyazungumza wakati akiongea na viongozi mbalimbali wa CCM, ambapo pamoja na mambo mengine alitutaka tusikubali kumpitisha mtu ambaye sio mwenyeji wa mkoa wa Tabora ili miaka yote wabunge wa hapa Nzega wawe ni kabila la Wanyamwezi," walisema watoa habari hizo.
Walifafanua kuwa hivi karibuni katika sherehe za siku ya wanawake duniani ambazo kimkoa zilifanyika katika kanisa la AICC lililopo eneo la Kariakoo, Selelii alitoa fedha taslimu Sh 270,000 kuwasaidia wanawake hao.
Lakini anadaiwa kwamba katika hotuba yake kwa wanawake hao aliwataka pia kutomchagua mbunge Muislamu kwani ataliibua upya suala la Mahakama ya Kadhi kauli ambayo Selelii amekana kuitamka.
Akizungumza na Mwananchi, Selelii alisema yeye alitamka wazi kwamba hatakubali kuona Jimbo la Nzega likichukuliwa na mtu kutoka nje ya Mkoa wa Tabora, kwa sababu kila mtu anatakiwa akagombee sehemu ambayo ni mwenyeji.
"Suala la udini mimi sikulizungumza kabisa, huo ni uongo, mtu wa dini yeyote anaweza kugombea isipokuwa awe ni mwenyeji wa mkoa wa Tabora, kama sio mwenyeji wa Tabora labda ametokea Bukoba akagombee hukohuko Bukoba hapa Nzega watagombea Wanyamwezi tu kila mtu ana kwao bwana," alisema Selelii .
Source: Mwananchi News